BUNGE LAMWIDHINISHA KANJA KUWA INSPEKTA MKUU

Hatimaye bunge la kitaifa limemwidhinisha Douglas Kanja kuwa inspekta mkuu wa polisi, na sasa anasubiri uteuzi rasmi wa Rais William Ruto. Kanja aliyetueliwa mnamo tarehe 25 mwezi Julai, aidha amepewa mamlaka ya kutoa amri kwa maafisa wa idara ya kitaifa ya polisi. Kanja alilazimika kuondoka kwenye wadhifa huo aliokuwa akishikilia na kumpisha naibu wake wa […]

MGOMO WA UASU WAZIMWA, MAHAKAMA YAAGIZA MAZUNGUMZO

Ni afueni kwa wanafunzi wa vyuo vikuu baada ya mahakama ya uajiri na leba kusitisha mgomo wa wafanyakazi wa vyuo vikuu vya umma ambao umeanza hii leo kupitia muungano wa UASU. Jaji wa mahakama hiyo Jacob gakeri, ametoa agizo hilo baada ya mabaraza ya vyuo vikuu na shirikisho la uajiri nchini FKEkuwasilisha kesi mahakamani. Aidha, […]

RUTO AAGIZA UPATANISHI KWA MAHAKAMA, POLISI

Kama njia mojawapo ya kuleta upatanishi na uwiano, Rais William Ruto ametoa wito kwa idara ya mahakama na ile ya polisi kukumbatia ushirikiano kuhusiana na masuala ya kitaifa, akirejelea vuta nikuvute ambayo imeshuhudiwa baina ya idara hizo katika siku za hivi karibuni. Kupitia taarifa, Rais Ruto amezitaka idara hizo huru kukumbatia uwiano wanapotafuta usuluhishi wa […]

FORD KENYA YAKANA KUVUNJWA

Chama cha Ford Kenya kimepinga madai ya kuvunjiliwa mbali na kujiunga na kile tawala cha UDA, na kusisitiza kwamba mizizi yake katika siasa za humu nchini ni imara. Kupitia kwa katibu wake mkuu ambaye pia ni mbunge wa Tongaren John Chikati, Ford Kenya imesema kwamba haina mpango wa kujiunga na UDA na badala yake kusisitiza […]

SERIKALI KUSAKA SULUHU KWA ‘CHOKORAA’

Serikali ya kitaifa na ile ya kaunti ya Mombasa zinafanya mazungumzo kuhusiana na mbinu ya kuzihudumia familia za mitaani, hatua ambayo huenda ikaleta afueni kwa familia hizo. Haya ni kulingana na kamishna wa kaunti hiyo Mohammed Noor, ambaye amesema kwamba familia za mitaani ni miongoni mwa vyanzo vya kudorora kwa usalama kwenye kaunti hiyo. Noor […]

WAKAZI WEBUYE ‘HAWATAKI’ TRELA

Wakaazi wa eneobunge la webuye magharibi wanataka serikali kupiga marufuku trela za kusafirisha mizigo dhidi ya kutumia barabara ya Bokoli hadi matisi, wakisema malori hayo yamechangia kuharibika kwa barabara hiyo mbali na kuhatarisha maisha yao. Wakiongozwa Edward Kimakwa, wamesema barabara hiyo ni ndogo kwa trela hizo, wakidai zimechangia kwa visa vya ajali. Aidha, wameibua hofu ya kupata […]

MATOKEO YA DIMBA LA KLABU BINGWA BARANI ULAYA

Timu ya Bayern Munich iliicharaza Dynamo Zagreb mabao 9-0 katika uga wao wa nyumbani- Allianz Arena. Kwenye mechi hiyo ya kukata na shoka, Harry Kane alifunga mabao matano huku Leroy Sane, Michael Olise, Raphael Guerreiro na Leon Goretzka wakifunga bao moja kwa kila mmoja. Mabingwa watetezi Real Madrid walifunga VfB Stuttgart mabao 3-1 na kufufua […]

TIMU YA ASTON VILLA IMESHIRIKI MASHINDANO YA KLABU BINGWA BARANI ULAYA KWA MARA YA KWANZA

Klabu ya Aston Villa ni miongoni mwa timu ambazo zimecheza kwa mara ya kwanza katika ligi ya klabu bingwa barani Ulaya. Aston Villa hapo jana waligaragazana na timu ya Uswizi ya Young Boys na kuwachapa kichapo takatifu cha mabao 3-0 ugenini. Villa walijikatia tiketi ya kushiriki mashindano hayo baada ya kumaliza katika nafasi ya 4 […]

TIMU YA CHELSEA IMEFUFUA AZMA YA KUMSAJILI VICTOR OSIMHEN KUTOKA GALATASARAY

Chelsea imefufua azma ya kumsajili Victor Osimhen kutoka Galatasaray baada ya kuanzisha makubaliano na timu ya Napoli kabla ya Januari. Victor Osimhen alikuwa Napoli kabla ya kuenda Galatasaray kwa mkopo. Osimhen, ambaye ni mchezaji wa kimataifa wa Nigeria, alikuwa miongoni mwa walengwa wakuu wa Chelsea. Napoli walikuwa tayari kumwachilia aende msimu wa joto baada ya […]

GOR MAHIA KUGARAGAZANA NA YANGA SC YA TANZANIA JANUARI, 2025 KWENYE UGA WA SIAYA

Gor Mahia sasa watamenyana na Yanga SC ya Tanzania siku ya kuzindua uga wa Siaya miezi mitatu zijazo. Hii ni kwa mujibu wa gavana wa kaunti ya Siaya James Orengo kupitia ukurasa wake wa X, maarufu Twitter. Gavana huyo alidokeza amefanya mazungumzo na rais wa klabu ya Yanga SC Hersi Said na kufikia makubaliano. Mechi […]