AFUENI YA MASOMO WEBUYE EAST

Ni afueni kwa wanafunzi wa vyuo vya anuai na vile vya utabibu katika eneo bunge la Webuye Mashariki baada ya hazina ya ustawishaji eneo bunge hilo kuzindua basari ya shilingi milioni 5 kufadhili masomo yao. Akizungumza baada ya kuzindua zoezi hilo afisini mwake mjini Webuye, mbunge wa eneo hilo Martin Wanyonyi amekariri kuwa fedha hizo […]

MZIGO WA WAFANYIKAZI HEWA WAMLEMEA MLIPA USHURU

Mkenya mlipa ushuru ameendelea kuathirika baada ya tume ya utumishi wa umma (PSC) kugundua wafanyikazi hewa 17,000 wanaogharimu serikali mabilioni ya fedha kila mwaka. Waziri wa utumishi wa umma, Justin Muturi, amewasilisha mswada wa 2024 wa usimamizi na maendeleo ya utumishi wa umma, unaolenga kuondoa wafanyikazi hewa, kufanya ukaguzi wa mishahara kila robo mwaka, na […]

UTEKELEZAJI WA CBC WAKUMBWA NA MVUTANO WA MALIPO

Utekelezwaji wa mtaala wa umilisi (CBC) unakabiliwa na changamoto, huku Kenya ikikumbwa na ucheleweshaji wa kukamilika kwa Mradi wa Kuboresha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQIP), unaofadhiliwa na Benki ya Dunia. Ingawa muda wa mwisho wa kukamilika uliongezwa na fedha kugawanywa, mradi huo bado haujakamilika kutokana na mvutano kati ya serikali na wakandarasi kuhusu malipo […]

FAMILIA YAFURUSHA POLISI MWEA

Wakazi wa Mwea kaunti ya Kirinyaga wamepatwa na mshangao baada ya kituo cha polisi cha Riandira kufungwa na maafisa wote 6 wa polisi waliokuwa wakihudumu kituoni humo kuhamishwa kuhusiana na malimbikizi ya shilingi milioni 2 za kodi. Maafisa hao wamefuurushwa na familia ya mfanyabiashara Mwangi Thuita aliyewataka waanze kulipa kodi kabla ya kifo chake mnamo […]

WAKAZI MUMIAS WAMTETEA SALASYA

Wakazi wa eneo la Mumias Mashariki wamejitokeza kukosoa hatua ya mbunge wao Peter Salasya kufurushwa na hata kujeruhiwa na kundi la mashabiki na wahuni kutoka uwanja wa michezo wa Nyayo jijini Nairobi siku 2 zilizopita, wakikariri kuwa mbunge huyo ana haki ya kujieleza kama kiongozi aliyechanguliwa. Wakizungumza na wanahabari, wakazi hao wamesema hawataruhusu kiongozi wao […]

WAWANIAJI WAJITETEA WAKILENGA IEBC

Ukosefu wa uaminifu wa wakenya katika tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC kuendesha uchaguzi huru na wa haki ndilo suala linalofaa kuangaziwa kwa dharura. Haya ni kwa mujibu wa Erastus Ethekon, anayewania uwenyekiti wa tume hiyo akizungumza akiwa mbele ya jopokazi linaloendesha mahojiano ya wawaniaji wa wadhifa huo. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

MSHUKIWA WA MAUAJI AZUILIWA KWA SIKU 10

Mahakama ya Kirinyaga imeamuru mshukiwa wa mauaji ya mpenzi wake, Brian Wambugu Mwangi, kuzuiliwa kwa siku kumi kwa uchunguzi zaidi. Washukiwa wengine wawili pia wamekamatwa kusaidia uchunguzi, huku ikibainika kuwa Nelima, mama wa watoto wawili, alikuwa amehamia Ngurubani kutafuta riziki. Mwili wa marehemu Grace Nelima, 23, ulipatikana ndani ya tanki la maji taka Machi 15, […]

VIJANA 100 WA MAGENGE LIKONI WAJISALIMISHA

Vijana 100 waliokuwa wakijihusisha na uhalifu wamejisalimisha kwa polisi huko Likoni, kaunti ya Mombasa, wakiahidi kuachana na uhalifu. Kamanda wa Polisi wa Pwani, Ali Nuno, ameahidi kuwasaidia kupata njia mbadala za kujikimu, huku mashirika ya kiraia yakiwasihi kujiunga na vyuo vya TVET vinavyogharamiwa na serikali ya kaunti. Serikali ya kaunti imeahidi kuwapa ajira wale watakaohitimu. […]

LAMINE AFUNGA BAO LA KIPEKEE

Lamine Yamal alifunga bao zuri lakini pia alikosa penalti katika usiku mwingine wa ukuaji wa nyota wa Barcelona wakati Uhispania ilitinga nusu fainali ya Ligi ya Mataifa. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 17 alifurahi sana wakati wa sare ya 3-3 dhidi ya Uholanzi Jumapili kwenye uwanja uliouzwa wa Mestalla huko Valencia, hata kama aliishia […]

NAIROBI THUNDER WAAMBULIA KICHAPO

Mabingwa watetezi wa Ligi ya Kitaifa ya Kikapu ya Kenya (KNBL) Nairobi City Thunder waliambulia kichapo cha 80-73 dhidi ya wapinzani wao Mamlaka ya Bandari ya Kenya (KPA) katika mpambano wa dhamira ya juu katika Ukumbi wa Michezo wa Nyayo Stadium. Mechi hiyo ilizikutanisha timu hizo mbili pendwa kushinda taji la msimu huu katika pambano […]