ATHARI ZA UKAME KWA UZALISHAJI WA CHAI, MAPATO YA TAIFA

Uzalishaji wa chai nchini Kenya umeshuka kwa asilimia 13.55 katika miezi miwili ya kwanza ya mwaka 2025, hali iliyochangiwa na ukame usio wa kawaida kulingana na Bodi ya Chai ya Kenya. Afisa Mkuu Mtendaji wa Bodi hiyo, Willy Mutai, amesema kwenye taarifa iliyotolewa jijini Nairobi kwamba uzalishaji kwa kipindi hicho ulikuwa kilo milioni 98.9, ikilinganishwa […]

VIJANA WATAJWA KIINI CHA MAGEUZI KATIKA SEKTA YA UTALII

Waziri wa Utalii na Wanyamapori, Rebecca Miano, ameelezea mafanikio ya vijana katika sekta ya utalii kama ishara ya juhudi za serikali kuwawezesha na kukuza ajira endelevu. Akizungumza katika hafla ya East Africa Future Leaders Challenge iliyofanyika Strathmore University, Miano amesema wizara yake inaendeleza mafunzo ya ujuzi, ujasiriamali, na ushirikishwaji wa vijana katika uchumi wa utalii. […]

5 WAUAWA MANDERA

Maafisa wa usalama wameimarisha doria katika eneo la Bur Abor kaunti ya Mandera kufuatia kisa ambapo wachimbaji migodi 5 wameuawa na wenzao 2 kujeruhiwa na watu wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la Al-Shabaab. Waathiriwa wamevamiwa ghafla mapema leo baada ya kuwasili katika eneo hilo, wakimininiwa risasi huku wachimbaji migodi 25 wakifanikiwa kutoroka. Tukio hilo limethibitishwa […]

RAIS ATAKIWA KUSITISHA UBOMOAJI

Rais William Ruto ametakiwa kuagiza kusitishwa kwa ubomoaji wa makazi na nyumba ambao umekuwa ukiendelea katika eneo la Athi River kaunti ya Machakos. Kulingana na seneta wa kaunti hiyo Agnes Kavindu, hatua hiyo ni ukosefu wa heshima kwa familia zilizotumia fedha zao kujenga nyumba hizo ilhali baadhi ya ubomoaji unaendelea bila notisi kutolewa. Imetayarishwa na […]

UPINZANI WASHINIKIZA MASHAURIANO NA RUTO

Viongozi wa upinzani wakiongozwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua na makamu wa rais wa zamani Kalonzo Musyoka wamemtaka Rais William Ruto kuwashirikisha kabla ya kuwateua makamishna wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC. Kupitia taarifa baada ya mkutano jijini Nairobi, viongozi hao wamesema mashauriano hayo yatahakikisha pande zoet zinaafikiana kuhusu orodha ya mwisho […]

WAHALIFU MARALAL KUKABILIWA

Oparesheni kali inapangwa kuendeshwa katika eneo la Maralal kufuatia ongezeko la visa vya utovu wa usalama, ili kuwadhibiti wahalifu. Naibu wa Rais Prof.Kithure Kindiki amesema tayari amekutana na viongozi wa idara ya usalama na kwamba wale wanaovuruga amani Samburu watashughulikiwa vikali. Kindiki ametoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa miradi ya serikali katika kaunti hiyo, […]

MWANAMKE AUAWA, WATATU WAAJERUHIWA BARINGO

Uchunguzi umeanzishwa baada ya mwanamke wa makamo kuawa na watu wengine watatu kujeruhiwa baada ya msafara kuvamiwa na majambazi katika eneo la Moinonin, Kaunti ya Baringo. mkuu wa polisi, wa Loruk, Edward Serem, amethibitisha kuwa majambazi wamefyatua risasi licha ya msafara huo kusindikizwa na polisi. Tukio hili linajiri chini ya wiki moja baada ya watu […]

“WAZIRI AWEKWE DARASANI”

Pana haja ya kumsaidia waziri mteule Hannah Cheptumo kupata ufahamu wa kina kuhusu suala la mauaji yanayowalenga wanawake nchini na dhuluma za kijinsia kijumla kabla ya kuapishwa na kuanza majukumu yake kama waziri wa masuala ya kijinsia. Ni wito wake seneta maalum Gloria Orwoba akizungumza katika bunge la seneti, ambako amewataka wabunge kumhamasisha waziri huyo […]

RUTO AAPA KULINDA JESHI

Rais William Ruto amehimiza juhudi za Pamoja katika kuhakikisha usalama wa taifa, na kuwataka wakenya kujiepusha na mijadala kuhusu jeshi la ulinzi kiholela. Rais ameyasema haya katika chuo cha kutoa mafunzo ya kijeshi eneo la Lanet kaunti ya Nakuru ambako ameongoza hafla ya kufuzu kwa wanajeshi wa kiwango cha Cadet. Amesema serikali itafanya kila iwezalo […]

TEUZI ZA RUTO ZAIDHINISHWA

Bunge la kitaifa limewaidhinisha mawaziri wateule Geoffrey Ruku wa utumishi wa umma na Hannah Cheptumo wa jinsia kuwa mawaziri baada ya kupigwa msasa, wakisubiri kuapishwa rasmi ili kuanza majukumu yao. Wakati wa vikao vya bunge, wabunge wamemtaka Cheptumo kuwaomba wanawake msamaha kuhusiana na kauli zake siku ya Jumatatatu alipokuwa akihojiwa kwamba wengi wa wanawake huuawa […]