LIVERPOOL WAKARIBIA KUTWAA TAJI LA EPL

Liverpool wako hatua chache kutwaa taji la Ligi Kuu ya Uingereza baada ya ushindi wa 2–1 dhidi ya West Ham, bao la ushindi likifungwa na Virgil van Dijk dakika za mwisho. Luis Diaz alifungua ukurasa kabla ya Andrew Robertson kujifunga, lakini Van Dijk akaamua matokeo kupitia kona ya Alexis Mac Allister. Liverpool sasa wanaongoza kwa […]

AMBROSE RACHIER AREJEA KUONGOZA GOR MAHIA

Ambrose Rachier amechaguliwa tena kuwa mwenyekiti wa klabu ya Gor Mahia baada ya uchaguzi mkali uliofanyika katika uwanja wa Nyayo Wakili huyo wa jijini alipata kura 658 dhidi ya mpinzani wake pekee, aliyekuwa mweka hazina wa klabu hiyo, Dolfina Achieng’, aliyepata kura 456. Rachier alichukua uongozi wa K’Ogalo mwaka 2008 na tangu wakati huo ameiongoza […]

KENYA U-20 KUKABILI KUNDI GUMU AFCON MISRI

Timu ya taifa ya vijana wa chini ya miaka 20 itakabiliana na Nigeria, Tunisia na Morocco kwenye kundi gumu katika michuano ya AFCON ya mwezi huu nchini Misri. Kenya, chini ya kocha Salim Babu, itashiriki kwa mara ya kwanza huku wapinzani wao wakiwa na uzoefu mkubwa. Nigeria ni mabingwa mara saba na wamewahi kushiriki Kombe […]

KUNA MANUFAA MENGI YA KIUCHUMI KUFUATIA MAGUEZI YA AU, RAIS RUTO

Bara la afrika kwa jumla limepata fursa za kipekee za biashara wiki hii baada ya umoja wa afrika kufanya mageuzi makubwa ya kitaasisi, mageuzi ambayo yanaashiria enzi mpya ya muungano wa  kiuchumi kwa bara la afrika. Rais wiliam Ruto ambaye walihutubu wakati wa ufunguzi wa Shirikisho la Wafanyabiashara Duniani uliofanyika jijini Nairobi, amesema kuwa ni fursa ya kukumbatiwa na […]

LIVERPOOL WAENDELEZA MAZUNGUMZO NA SALAH

Liverpool wanaendelea na mazungumzo ya kumpa mkataba mpya Mohamed Salah huku viongozi hao wa Premier League wakizidi kuamini kwamba atasalia Anfield msimu ujao. Mkataba wa mchezaji huyo wa kimataifa wa Misri mwenye umri wa miaka 32 unamalizika mwishoni mwa msimu huu pamoja na wachezaji wenzake wa Liverpool Virgil van Dijk na Trent Alexander-Arnold. Wakati Alexander-Arnold […]

MENENGAI OILERS WAIMARISHA KIKOSI CHAO

Kocha mkuu wa Menengai Oilers Gibson Weru anasema timu yake imeimarisha maandalizi kabla ya mpambano wao wa fainali ya Kombe la Kenya unaotarajiwa kwa kasi dhidi ya wapinzani wao Kabras Sugar Jumamosi hii katika Uwanja wa Maonyesho wa ASK mjini Kakamega. Weru anasisitiza kuwa timu yake haitatishwa na Kabras, ambao wamesalia bila kushindwa katika michuano […]

OMALLA YUKO HURU KUICHEZEA GOR MAHIA

Mshambulizi wa Gor Mahia Benson Omalla yuko huru kuichezea klabu hiyo tena baada ya kupokea Cheti chake cha Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kutoka kwa klabu ya Al Safa FC ya Lebanon. Katika taarifa iliyotolewa jana, mabingwa hao mara 21 wa Ligi Kuu ya FKF walisema mshambuliaji huyo wa zamani wa Western Stima yuko vizuri baada […]

ECHOES OF WAR: WANAFUNZI WA BUTERE GIRLS WASUSIA

Hamu ya wanafunzi wa Butere Girls kuonyesha uwezo wao wa kuigiza imezimwa mapema leo, kufuatia uamuzi wao kususia kuigiza mchezo wenye utata wa Echoes of War ulioandikwa na aliyekuwa seneta wa Kakamega Cleophas Malala. Wanafunzi hao ambao wamenyimwa kipaaza sauti walipokuwa jukwani mbali na wananchi kuzuiwa kuingia kwenye ukumbi, badala yake wameimba wimbo wa taifa […]

ECHOES OF WAR: MCHEZO WAMWEKA MALALA PABAYA

Huku tamasha za kitaifa za michezo ya kuigiza zikiendelea jijini Nakuru, aliyekuwa seneta wa Kakamega Cleophas Malala ameishutumu idara ya polisi kwa madai ya kutumiwa kumhangaisha kutokana na mchezo wa kuigiza aliouandika wa Echoes of War, ambao umeratibiwa kuwasilishwa na shule ya Butere Girls mapema leo kwenye tamasha hizo. Hii ni baada ya polisi jana […]

MULONGO ATETEA ‘UKATAJI HARAMU’

Waziri wa mazingira Deborah Mulongo amepuzilia mbali tetesi kwamba serikali inaendesha ukataji miti haramu katika misitu ya umma nchini, akisema kuna porojo zinazoendelezwa hasa katika mitandao ya kijamii kuhusiana na malori kuingia na kutoka kwenye misitu ya umma yakiwa na viapnde vya miti iliyokatwa. Ameyasema haya akiwa mbele ya bunge la seneti kujibu maswali, ambako […]