SERIKALI YASITISHA MKATABA WA BARABARA NA KAMPUNI YA KIFARANSA

Serikali ya Kenya imesitisha mkataba wa euro bilioni 1.3, sawa na takriban shilingi bilioni 190.8, uliokuwa umeafikiwa na muungano wa kampuni kutoka Ufaransa ukiongozwa na Vinci SA, kwa ajili ya upanuzi wa barabara ya kilomita 140 kutoka Nairobi hadi Nakuru. Mkataba huo ulisainiwa mwaka 2020 jijini Paris wakati wa ziara ya rais wa wakati huo […]

LAWAMA ZA UONGOZI UON

Utata wa uongozi wa chuo kikuu cha Nairobi sasa umechukua mkondo tofauti, viongozi wa wanafunzi chuoni humo wakimlaumu waziri wa elimu Julius Ogamba kwa madai ya kuhitilafiana na uongozi wa chuo hicho. Haya yamejiri baada ya Ogamba kuwahamisha wanachama 4 wa baraza la usimamizi wa chuo hicho hadi katika vyuo vikuu vingine 3 ambavyo ni […]

WAZEE WA MITAA KUJUA HATMA

Hatma ya wasimamizi wa vijiji kuanza kupokea malipo yao ya kila mwezi itabainika hivi karibuni kutokana na maoni yatakotolewa na wakenya kwenye vikao vya ukusanyaji wa maoni vinavyoongozwa na wizara ya usalama wa kitaifa. Vikao hivyo vitaandaliwa hapo kesho katika kaunti 10 ikiwemo Kakamega, Nairobi, Uasin Gishu, Nakuru, Mombasa na Machakos. Kwenye pendekezo hilo, wazee […]

KUPPET YAIKABA TSC

Muungano wa kutetea maslahi ya walimu wa shule za upili na vyuo vya kadri KUPPET umeitaka tume ya kuwaajiri walimu TSC kutatua changamoto wanazopitia walimu wa shule za sekondari msingi JSS, ukiwemo ukosefu wa vifaa muhimu. Wakizungumza katika eneo la Gisambai kaunti ya Vihiga, viongozi wa KUPPET wakiongozwa na mwenyekiti Omboko Milemba na kaimu katibu […]

UTEUZI WA TUME

Wakenya 6 zaidi wanahojiwa hii leo katika kinyang’anyiro cha kujaza nafasi za makamishna wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC. Miongoni mwa walihojiwa tayari hii leo ni wakili Mary Kigen, ambaye ameahidi kutumia ujuzi wake wa kisheria kuboresha utendakazi wa IEBC. Haya yanajiri huku waziri mteule wa utumishi wa umma Geoffrey Ruku na mwenzake […]

HATMA YA ‘WANYAKUZI’ WA ARDHI, MAAFISA

Watu 8 wakiwemo maafisa wawili wa wixzara ya ardhi wanaotuhumiwa na kuongoza misururu ya unyakuzi wa ardhi watasalia korokoroni kwa siku 4 zaidi ili kuiwezesha idara ya DCI kukamilisha uchunguzi dhidi yao. Akitoa uamuzi huo, hakimu Robinson Ondieki amesema kuwa iwapo uchunguzi huo hautakamilika ndani ya siku hizo, wataachiwa huru kwa dhamana ya shilingi elfu […]

MBOLEA YA URUSI: SERIKALI YAVUNJA KIMYA

Serikali imepinga madai kwamba ilipokea mbolea ya bure kutoka kwa serikali ya Urusi na kisha kuipakia upya na kuwauzia wakulima nchini jinsi ilivyoibuliwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua. Kulingana na katibu katika wizara ya kilimo Paul Rono, Urusi ilitoa tu malighafi magunia elfu 600 ya kutengeneza mbolea, nayo Kenya ikatoa kandarasi kwa kampuni moja […]

MAAFISA 37 WA POLISI WAHUKUMIWA KWA UKATILI

Waathiriwa wa ukatili unaotekelezwa na maafisa wa polisi wameanza kupata haki, huku maafisa 37 wa polisi wakihukumiwa na kutumikia vifungo mbalimbali gerezani. Kulingana na mwenyekiti wa Tume ya Kutathmini Utendakazi wa Polisi, Issack Hassan, jumla ya kesi 267 dhidi ya polisi zimewasilishwa kwa tume hiyo, ambapo 106 kati ya hizo tayari zimekamilishwa mahakamani. Imetayarishwa na […]

TAHADHARI YA KIPINDUPINDU: WATU 6 WAFARIKI

Wakenya wametakiwa kuchukua tahadhari kufuatia mlipuko wa kipindupindu ambao tayari umeua watu sita na kuwaathiri wengine 100 katika maeneo mbalimbali nchini. Msemaji wa serikali Isaac Mwaura amesema serikali inachukua hatua kuhakikisha ugonjwa huo unadhibitiwa, huku akisisitiza umuhimu wa usafi wa mazingira na matumizi ya maji safi ili kuzuia maambukizi zaidi. Imetayarishwa na Janice Marete

UCHUNGUZI WA AJALI YA KWAMBIRA WAANZA, WATU 3 WAFARIKI

Uchunguzi umeanza kufuatia ajali iliyotokea katika eneo la Kwambira, barabara ya Nairobi-Nakuru, ambapo watu watatu wamepoteza maisha na wengine kujeruhiwa vibaya. Ajali hii inafuatia nyingine ya wiki iliyopita katika eneo hilo ambapo watu watano walikufa baada ya gari lao kupoteza mwelekeo. Polisi wamewataka madereva kuwa waangalifu na kufuata sheria za trafiki ili kuepuka ajali zaidi. […]