TEAM KENYA YAJIANDAA KWA MBIO KULE GUANGZHOU

Timu ya Kenya inakamilisha mazoezi yake ya makazi leo katika Uwanja wa Ulinzi Sports Complex kabla ya Mashindano ya Dunia ya Mbio za kupokezana kijiti mjini Guangzhou, Uchina, Mei 10-11.  Timu hiyo ilipiga kambi katika uwanja huo wa kijeshi siku mbili tu baada ya mchujo wa kitaifa Aprili 11-12 ingawa walikuwa wakitembelea msitu wa Karura […]

MUDAVADI AANZA ZIARA MAREKANI KUFUNGUA FURSA ZA KIUCHUMI KWA WAKENYA

Katika juhudi za kuwafaidi Wakenya kiuchumi na kuimarisha nafasi ya Kenya kimataifa, Waziri Mkuu Musalia Mudavadi ameanza ziara rasmi mjini Washington, Marekani, kufuatia mwaliko wa serikali ya Marekani. Mudavadi anatarajiwa kufanya mazungumzo na viongozi waandamizi akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio na Mwenyekiti wa Kamati ya Masuala ya Kigeni Brian Mast, kwa lengo […]

KERRA: MHASIBU KORTINI KWA TENDA ZA UFISADI

Katika juhudi za kupiga vita ufisadi nchini, mhasibu msaidizi wa KeRRA, Esther Wanjiru Chege, amefikishwa mahakamani Kajiado pamoja na washukiwa wawili kwa tuhuma za kutoa tenda za serikali kwa kampuni zinazohusishwa na mumewe. Kwa mujibu wa EACC, Wanjiru alitumia nafasi yake vibaya, akitoa kandarasi kwa kampuni tatu za mumewe, huku pia akimiliki mali isiyolingana na […]

SERIKALI YAPUNGUZA BAJETI YA MWAKA WA KIFEDHA

Hazina ya Kitaifa imetangaza marekebisho ya bajeti ya matumizi ya kawaida kwa mwaka wa kifedha wa 2025/2026, ikipunguza bajeti hiyo kwa takriban shilingi bilioni 10. Kulingana na ripoti ya Business Daily, bajeti hiyo sasa inasimama kwenye shilingi trilioni 1.73, ikiwa ni sehemu ya hatua za serikali kupunguza matumizi. Hatua hii inafuatia uamuzi wa Baraza la […]

BANDARI YA KISUMU YAENDELEA KUNG’ARA

Bandari ya Kisumu inazidi kuimarika kama kitovu cha biashara, baada ya kushuhudia ongezeko kubwa la meli na mizigo mwaka huu. Kwa mujibu wa KPA, bandari hiyo imeshughulikia tani 280,381 za mizigo mwaka 2025, ikilinganishwa na tani 116,578 mwaka uliopita. Zaidi ya meli 67 zimezuru bandari hiyo, ikiwa ni pamoja na MV Orion II ambayo hivi […]

RUTO AINGIA SOUTHRIFT

Wakazi wa eneo la Southrift wameratibiwa kunufaika na uzinduzi wa miradi ya maendeleo kwenye ziara ya Rais William ambayo imeanza hii leo. Akizungumza katika eneo la Ntulele kaunti ya Narok ambako amezindua rasmi soko, Rais Ruto amewahimiza wakazi kukumbatia mshikamano wa taifa. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WAKENYA WACHUNGULIA IEBC MPYA

Mchakato wa kubuniwa upya kwa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC umepiga hatua kubwa, Rais William Ruto akipokezwa rasmi ripoti ya jopokazi lililoendesha zoezi la kuwapiga msasa wanaowania kuhudumu kama mwenyekiti na makamishna wa tume hiyo. Akizungumza katika Ikulu ya Nairobi, Rais Ruto amelipongeza jopokazi hilo, akiahidi kuhakikisha wanaoteuliwa kuhudumu ni watu walio na […]

WETANG’ULA ATOA WITO KWA POLISI, DPP

Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang’ula, ameendelea kuitaka idara ya usalama kuendesha uchunguzi wa kina kwenye mauaji ya aliyekuwa mbunge wa Kasipul Ong’ondo Were, akitaka waliohusika kuwajibishwa mara moja. Akiwahutubia wanahabari katika hifadhi ya Lee alikoongoza tume ya huduma za bunge kuomboleza kifo hicho, Wetang’ula ameshutumu mauaji hayo na kushinikiza uchunguzi wa kina. Aidha, […]

MWANGA WA TUMAINI NGARA

Wakazi wa eneo la Ngara Railway Southern Zone wamepata afueni baada ya mahakama kuu kutoa agizo la kuzuia mpango wa kufurushwa kutoka makazi yao. Kwenye kesi hiyo, wakazi hao, wengi wao wakiwa wafanyakazi wa zamani wa shirika la Reli na wakongwe, wanahoji kuwa wameishi katika eneo hilo kwa miongo ambako wamewalea Watoto na wajukuu. Kesi […]

WASHUKIWA WATATU WA TUKIO LA KIATU DHIDI YA RUTO WAACHILIWA BILA MASHITAKA

Watu watatu waliokamatwa kwa kudaiwa kumtupia kiatu Rais William Ruto wakati wa hafla ya umma huko Migori, wameachiwa bila mashitaka baada ya uchunguzi kubaini kuwa kitendo hicho hakikuwa cha makusudi. Tukio hilo lilitokea Mei 5, wakati wa ziara ya rais ya kikazi ya siku tatu kaunti ya Migori. Maafisa wa usalama walichukua hatua haraka na […]