KWANINI NG-CDF, NGAF

Wengi wa wakenya wanaojitokeza katika vikao vya kukusanya maoni ya wakenya kuhusu ujumuishaji kwenye katiba hazina za NG-CDF na NGAF wameendelea kutetea hazina hizo, wakitaka zihalalishwe kwa misingi kwamba zinawafaidi. Zoezi hilo limeingia siku yake ya mwisho huku mamia ya wakazi wa eneo bunge la Teso Kaskazini kaunti ya Busia wakijitokeza katika ukumbi wa TSC […]

IEBC: WENGI WA WAKENYA WANAPENDELEA AMADI- TIFA

Asilimia 41 ya wakenya wanapendekeza aliyekuwa msajili wa idara ya mahakama Anne Amadi ateuliwe kuwa mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC. Haya ni kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wa shirika la TIFA, wengi wa wanaomuunga mkono Amadi wakiwa wenyeji wa Nairobi na Nyanza. Kuhusiana na tajriba, asilimia 23 ya wakenya wanapendelea […]

‘MAZURI YA MGENI’ NAROK

Shughuli za kibiashara na masomo zinatarajiwa kuimarika katika kaunti ya Narok kufuatia uzinduzi wa mradi wa umeme wa Last Mile unaolenga kuunganisha makazi 15,000 na nguvu za umeme. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Rais William Ruto ambaye yuko kwenye ziara ya eneo la Southrift amewataka wakenya kushitikiana na serikali yake ili kufanikisha utekelezaji wa miradi […]

ONG’ONDO: UFICHUZI MPYA

Uchunguzi katika mauaji ya aliyekuwa mbunge wa Kasipul Ong’ondo Were umechukua mkondo mpya, waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen sasa akidai kwamba wandani wa mbunge huyo ni miongoni mwa waliohusika kumwangamiza. Murkomen ameyasema haya katika kaunti ya Meru ambako ametoa hakikisho kuwa serikali inafanya kila iwezalo kumlinda kila mkenya. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

NCHI TANO ZAJIANDAA KWA MICHUANO YA NDONDI

Nchi tano zimethibitisha kushiriki katika mashindano ya kimataifa ya ndondi ya ‘Challenge Omar Bongo Ondimba’ yaliyopangwa kufanyika Libreville, Gabon kuanzia Mei 30-Juni 11. Nazo ni Congo Brazzaville, Cameroon, Angola, Zimbabwe, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Tarehe ya mwisho ya usajili, iliyopangwa awali Aprili 28, imeongezwa hadi Mei 16, 2025.  PESA ZA ZAWADI zitatolewa kwa […]

CHRISTIANO AMETAJWA KWA KIKOSI CHA TIMU YA TAIFA YA URENO

Cristiano dos Santos, mtoto mkubwa wa mshindi mara tano wa tuzo ya Ballon d’Or Cristiano Ronaldo, ameitwa kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ureno cha Vijana wasiozidi umri wa miaka 15. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 14, ambaye kama babake anachezea Al-Nassr ya Saudi Arabia, pia amewahi kuwa na […]

OLUOCH AOMBOLEZA PAUL OTULA

Kocha mkuu wa mpira wa vikapu wa timu ya Chuo Kikuu cha Africa Nazarene Michael Oluoch amemuomboleza marehemu rais wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu nchini Paul Otula, akimtaja kama nguzo katika chama cha mpira wa vikapu nchini. Oluoch anasema kufariki kwa Otula sio tu pigo kwa udugu wa mpira wa vikapu bali kwa taasisi […]

NG-CDF YAELEZWA KUWA MKOMBOZI WA ELIMU VIJIJINI

Wakenya wametakiwa kuunga mkono mswada wa marekebisho ya Katiba unaolenga kuidhinisha rasmi Hazina ya Maendeleo ya Maeneobunge (NG-CDF) kuwa sehemu ya Katiba. Wakazi wa eneobunge la Malindi, Kaunti ya Kilifi, wameeleza kuwa hazina hiyo imekuwa msaada mkubwa kwa jamii, hasa kwa kuwasaidia wanafunzi wanaotoka katika familia maskini kupata elimu. Aidha, wamesema kuwa fedha za NG-CDF […]

INTERMILLAN WAINGIA KWENYE FAINALI YA LIGI YA MABINGWA

Davide Frattesi aliweka Inter Milan katika fainali ya Ligi ya Mabingwa siku ya Jumanne kwa bao la ushindi katika muda wa ziada ambalo liliwapa Waitaliano hao ushindi mnono wa 4-3 dhidi ya Barcelona, ​​kwa jumla ya 7-6. Kikosi cha Simone Inzaghi kitamenyana na Arsenal au Paris Saint-Germain mwishoni mwa mwezi huu mjini Munich, ambapo watajihisi […]

MAANDALIZI YA MASHINDANO YA KIP KEINO YATIA KASI

Huku saa zikiyoyoma kuelekea mashindano ya Kip Keino Classic ya Mei 31, maandalizi katika Uwanja wa Kitaifa wa Nyayo yameshika kasi—na mkurugenzi Barnaba Korir anataka kasi hiyo iongezeke. Korir, ambaye pia anahudumu kama mwenyekiti wa Maendeleo ya chipukizi wa shirikisho la riadha nchini (AK), amemtaka mwanakandarasi kuzingatia kuendesha kazi hiyo kwa saa 24 ili kuhakikisha […]