MSHUKIWA WA NYAMA YA PUNDA AKAMATWA KIRINYAGA
Mshukiwa mmoja ametiwa mbaroni baada ya kunaswa kwa nyama ya punda wapatao 20 katika soko la Red Soil, eneo la Mwea Mashariki, Kaunti ya Kirinyaga na anatarajiwa kufikishwa mahakamani. Inadaiwa kuwa punda hao waliibwa na kuchinjwa kinyume cha sheria, kabla ya nyama hiyo kuanza kusafirishwa kuelekea soko la Kiamaiko, jijini Nairobi. Imetayarishwa na Janice Marete
English 














































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































