MASHIRIKA YAKOSOA OMBI LA RAIS RUTO

Mashirika ya kijamii yamemkosoa Rais William Ruto kwa kusalia kimya wakati ambapo wakenya wamedhulumiwa, ikiwemo wakati wa maandamano na kufurushwa kwa wanaharakati kutoka nchini Tanzania. Katika kikao na wnahabari mjini Machakos, mashirika hayo chini ya mwavuli wa Okoa Uchumi yameelezea kutoridhinishwa na kimya hicho, yakisema ni ishara kwamba ombi la Rais kutaka asamehewe ni unafiki. […]

ODINGA ATOA ARDHI KWA SERIKALI

Mpango wa serikali kujenga makazi ya bei nafuu kwa wakazi wa Kisumu umepigwa jeki, baada ya kinara wa ODM Raila Odinga kutoa hisani ya ekari 5 za shamba la kifamilia katika eneo la Kirembe ili kufanikisha ujenzi wa nyumba hizo. Akiwa kwenye ziara yake, Rais Ruto amempongeza Odinga kutokana na hisani hiyo, akisema serikali itawekeza […]

UTATA WA MUHURI WATATULIWA

Mwanasheria mkuu wa serikali Dorcas Oduor amesisitiza kuwa muhuri wa serikali ungali unahifadhiwa katika afisi yake ilivyo kisheria, akizima madai kwamba muhuri huo ulihamishiwa kwenye afisi ya mkuu wa utumishi wa umma Felix Koskei. Kwa mujibu wa Oduor, madai hayo yanalenga kuleta mgawanyiko serikalini. Ameyasema haya alipofika mbele ya kamati ya kurahisisha kesi za ardhi […]

MAHAKAMA YASITISHAI MCHAKATO WA IEBC

Mahakama kuu imetoa maagizo ya kusitisha kwa muda kuchapisha kwenye gazeti rasmi la serikali majina ya makamishna na mwenyekiti wa tume ya IEBC pamoja na kuapishwa kwao, ingawa ikaliruhusu bunge la kitaifa kuwapiga msasa 7 hao akiwemo mwenyekiti mteule Erastus Ethekon. Kwenye uamuzi wake, jaji Lawrence Mugambi amewasilisha kesi hiyo kwa mahakama ya upeo ili […]

KENGEN KUSAKA NJIA MBADALA YA UZALISHAJI

Shirika la kuzalisha umeme KenGen limesema inapanga kupunguza utegemezi wa umeme wa maji nchini ili kuimarisha ustahimilivu wa nishati, likisema umeme wa aina hiyo unaweza kuathiriwa na mvua isiyotabiriwa. Afisa mkuu mtendaji wa shirika hilo Peter Njenga amesema uwezo wa umeme wa maji nchini Kenya unakadiriwa kuwa megawati 840, ambao unachukua asilimia 24 ya uzalishaji […]

“HATUNA DENI LA SHULE!” SERIKALI YATANGAZA

Serikali imetangaza kuwa haina deni lolote la shule kuhusiana na mgao wa masomo, ikisema fedha zote za mwaka 2025 zimetolewa tayari licha ya walimu wakuu kusema kuwa ni kiwango kidogo tu cha fedha kilichotolewa. Katibu mkuu katika wizara ya fedha Chris Kiptoo, amesisitiza kuwa shughuli za masomo zinafaa kuendelea bila kutatizika kwani tayari wizara hiyo […]

HISIA ZA MSAMAHA WA RUTO

Rais William Ruto alistahili kuzuru hospitali ya Kenyatta wanakotibiwa waathiriwa wa maandamano ya kizazi cha Gen Z mwaka jana na kuwalipia bili za hospitali kama njia mwafaka ya kuwaomba msahama. Ndiyo kauli ya seneta wa Makueni Dan maanzo, akirejelea msahama alioomba rais hapo jana kupitia runinga. Hata hivyo, aliyekuwa kiongozi wa wengi katika bunge la […]

TUMEWAAJIRI WAKENYA ELFU 400, SERIKALI

Serikali ya Kenya Kwanza imewaajiri wakenya takribani elfu 400 wakiwemo walimu elfu 76,000, huku mikakati zaidi ikiendelea kuwekwa ili kuongeza nafasi za ajira. Haya ni kulingana na naibu Rais Kithure Kindiki, akiongeza mradi wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu umetoa nafasi elfu 200 huku wakenya zaidi wakiajiriwa kupitia mitandaoni. Ameyasema haya alipopokezwa ripoti za […]

BABU ATETEA KILIMO, UJENZI

Mbunge wa Embakasi East Babu Owino ameionya kamati ya fedha katika bunge la kitaifa dhidi ya kuongeza ushuru kwenye mswada wa kifedha wa mwaka 2025-26, akisema hatua hiyo italemaza sekta ya kilimo na uchumi kwa jumla. Akizungumza mbele ya kamati hiyo inayoongozwa na mbunge wa Molo Kimani Kuria, Owino ametaja sekta za kilimo, ujenzi na […]

DCI HAIJIFAHAMU, WANDANI WA GACHAGUA

Wandani wa aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua wamepuzilia mbali madai ya idara ya upelelezi DCI kwamba mbunge wa Juja George Koimburi alijiteka nyara, wakiwataja wanaoneza madai hayo kuwa wasiojifahamu. Wakizungumza katika hospitali ya Karen ambako mbunge huyo anadaiwa kuendelea kupokea matibabu, viongozi hao wamemshutumu Inspekta mkuu wa polisi Dougalas Kanja kwa madai ya kuwahangaisha kutokana […]