100 WAENDA “MTEJA” KWENYE MADARAKA

Zaidi ya wakenya 100 walipoteza simu zao kwenye uwanja wa Raila Odinga mjini Homa Bay wakati wa maadhimisho ya sherehe Madaraka za mwaka huu, nyingi ya simu zikiibwa usiku umati mkubwa ulipokuwa ukiingia uwanjani humo. Haya ni kwa mujibu wa kamanda wa polisi wa kaunti ya Homa Bay Lawrence Koilem, akisema idara ya upelelezi DCI […]

WAKAZI AMAGORO WALALAMIKIA UHALIFU

Wakazi wa eneo la Amagoro kaunti ya Busia wamelalamikia kudorora kwa biashara kutokana na ongezeko la visa vya uhalifu vinavyowalazimu kufunga biashara zao mapema. Wakazi hao wamehofia kuongezeka kwa uhalifu huo kutokana na madai kwamba kituo cha doria cha Amagoro kinalengwa kuhamishwa. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

SERIKALI YASHUTUMIWA KUHUSU “UDHALIMU WA TANZANIA”

Serikali imeendelea kushutumiwa kwa jinsi ilivyoshughulikia suala la utekaji nyara na madai ya unyanyasaji dhidi ya mwanaharakati Boniface Mwangi nchini Tanzania, na jinsi ilivyounga mkono kufurushwa kwa mawakili na wanaharakati kutoka nchini humo. Kwenye mahojiano na runinga moja nchini, viongozi mbali akiwemo mbunge wa Kitui Central Makali Mulu, mwenzake wa Uriri Mark Nyamita na mtaalam […]

AZMA YA GOR MAHIA KUTWA TAJI YAPATA PIGO

Azma ya Gor Mahia kuhifadhi taji la Ligi Kuu ya FKF ilipata pigo kubwa baada ya sare ya 1-1 na wapinzani wao AFC Leopards katika mchezo mkali wa Mashemeji Derby Uwanja wa Raila Odinga mjini Homa Bay, Jumatatu. Mabingwa hao wa rekodi ya ligi walikuwa wakitamani sana kupata pointi nyingi zaidi ili kusalia hai katika […]

RUTO ATETEA UKODISHWAJI WA VIWANDA

Rais William Ruto amehalalisha uamuzi wa serikali wa kukodisha viwanda vinne vya sukari vinavyomilikiwa na serikali, akitaja kuwa hatua muhimu ya kuboresha ufanisi, kurejesha faida, na kulinda maisha ya wakulima. Akizungumza kwenye sherehe za Madaraka Day katika Kaunti ya Homa Bay, Ruto amesema ukodishaji wa viwanda vya kutengeneza sukari vya Nzoia, Chemelil, Sony, na Muhoroni […]

MECHI KATI YA MUKUMU NA SHANDEEMA YASITISHWA

Mechi ya soka ya Shule ya Upili iliyokuwa ikitarajiwa kati ya Shanderema Boys na Mukumu Boys ilisitishwa Jumapili katika Shule ya Solyo iliyoko Shinyalu, Kaunti ya Kakamega, kufuatia wasiwasi wa usalama. Kusimamishwa huko kulijiri baada ya machafuko miongoni mwa mashabiki wa Mukumu, hali iliyosababisha kushindwa kwa mechi hiyo kuendelea. Mratibu wa Chama cha Michezo cha […]

POLISI AUAWA NAKURU, WENZAKE WAJERUHIWA

Afisa mmoja wa polisi ameuawa kwa risasi huku wenzake 2 wakijeruhiwa na watu wanaoaminika kuwa magenge ya wahalifu wakati polisi walipokuwa wakishika doria katika eneo la Free Area jijini Nakuru usiku wa kuamkia leo. Waliojeruhiwa ambao ni maafisa wa kituo cha polisi cha Bondeni, wanaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Nakuru level 5. Kamishna wa […]

MNATUMIWA VIBAYA, GACHAGUA AWAONYA WABUNGE

Aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua amewaonya wabunge kutoka eneo la Mlima Kenya wanaoegemea mrengo wa Rais William Ruto dhidi ya kile alichokitaja kuwa kutumiwa visivyo na Rais Ruto, akiwataka kuwa na msimamo na kupigania maslahi ya wakazi wa eneo hilo. Gachagua amewahusisha wabunge hao na rabsha ambazo zimekuwa zikishuhudiwa kwenye mikutano yake, akiwatuhumu kwa kutumiwa […]

ODINGA ASHINIKIZA FIDIA KWA WAATHIRIWA GEN Z

Kinara wa ODM Raila Odinga amejiunga na kauli za viongozi wa upinzani kumshinikiza Rais William Ruto kuwafidia waathiriwa wa maandamano ya yaliyoongozwa na vijana wa kizazi cha Gen Z mwaka jana, akisema hiyo ndiyo njia pekee ya kuliwezesha taifa kusahau madhila yaliyotokea na kusonga mbele. Akizungumza wakati sherehe za Madaraka kwenye kaunti ya Homa Bay, […]

SHA YA POLE POLE

Sekta mbali mbali ikiwemo ile ya nyumba za bei nafuu na bima ya afya SHA zinatarajiwa kufanyiwa marekebisho, iwapo bunge litaidhinisha mapendekezo ya Rais William Ruto kufanya mageuzi hayo ikiwemo kuwazesha wakenya kulipia huduma za SHA kwa malipo ya pole pole. Kulingana na Rais akizungumza alipoongoza taifa kwenye maadhimisho ya sherehe za Madaraka, wakenya pia […]