POLISI KUSHIRIKIANA ZAIDI NA WANANCHI

Idara ya usalama nchini itashirikiana zaidi na jamii katika kuimarisha usalama na kukomesha uhalifu. Ni usemi wake inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja kwenye mkutano na wakuu wa usalama nchini akisema kuwa ushirikiano huo utasaidia kuzuia visa vya uhalifu. Kanja amewataka polisi kuimarisha mawasiliano na wananchi. Imetayarishwa na Maureen Makhobe

WASHUKIWA 3 WA MAUAJI YA WERE WAACHILIWA

Washukiwa watatu waliohusishwa na mauaji ya mbunge wa Kaspul Charles Were wameachiliwa huru.Tatu hao Douglas Muchiri Wambugu,Juma Ali Haikal na David Mihigo wameachiliwa baada ya mahakama kupitia hakimu Irene Gishobi kuamua kuwa hakuna Ushahidi wa kutosha wa kuwahusisha na mauaji ya mbunge huyo. Hata hivyo washukiwa wengine wanaendelea kuzuiliwa kufuatia kifo cha mbunge huyo aliyepigwa […]

VILABU VYA EPL VIKO MBIONI KUNYAKUA WACHEZAJI

Vilabu vya Ligi Kuu ya Uingereza vimeanza kwa kasi kusajili wachezaji wapya katika dirisha hili la usajili huku mikataba ya pesa nyingi itaendelea kuja na uhamisho mkubwa unaoendelea kwa sasa. Liverpool imekuwa ikifanya kazi ya ziada kumpata mchezaji Florian Wirtz. Mazungumzo yanaendelea kuhusu mkataba utakaokuwa wa rekodi ya klabu utakaogharimu zaidi ya pauni milioni 120, […]

MENEJA WA DARAJANI GOGO ANA IMANI NA KIKOSI CHAKE

Meneja wa Timu ya Darajani Gogo Sudi Avoga ameelezea imani na timu yake kabla ya mechi muhimu huku msimu wa Ligi Kuu ya Taifa (NSL) ukikaribia mwisho. Gogo kwa sasa wako katika nafasi ya tano kwenye jedwali wakiwa na alama 50, mbili chini ya Naivas wanaowinda daraja la FKF-Premier League, walio nafasi ya tatu huku […]

VIHIGA QUEENS WAPIGIWA UPATO KUSHINDA KOMBE LA FKF

Kocha mkuu Boniface NyamuNyamu alisema ni lazima Vihiga Queens itimize katika Kombe la FKF msimu huu ambao umekua mgumu sana. Mabingwa mara nne wa Ligi Kuu ya Wanawake watamenyana na Bungoma Queens katika nusu-fainali siku ya Jumapili, na Nyamu anatazamia kuelekea fainali huku wakilenga kukwepa kampeni nyingine isiyo na taji. Mchezo huu utaandaliwa katika uwanja […]

MSHUKIWA ADAIWA KUWAUMA POLISI BUNGOMA

Polisi katika kaunti ya Bungoma wanatarajia kumfikisha mahakamani mshukiwa mmoja anayedaiwa kuwauma na kuwajeruhi maafisa 2 wa polisi kutoka kituo cha Namwela, waliokuwa wamekwenda kumkamata kwa tuhuma za uhalifu. Kulingana na wakazi, maafisa 2 kati ya 3 waliokuwa wamefika nyumbani kwa jamaa huyo katika kijiji cha Sitabicha, walishambuliwa na mshukiwa aliyewauma begani na mikononi, ila […]

RUTO AWAPA MAGAVANA JUKUMU

Rais William Ruto amewataka magavana kuhakikisha hospitali zote za umma na za kibinafsi kwenye kaunti zao zimejiandikisha chini ya bima ya afya SHA ili kuhakikisha mpango wa serikali wa utoaji huduma za afya kwa wote UHC unatekelezwa kikamilifu. Rais ameyasema haya kwenye mkutano na magavana katika Ikulu ya Nairobi hapo jana, akitaja hatua ya baadhi […]

NIMROD AJIKAANGA KITUI

Chama cha Wiper kimeshutumu kauli za mbunge wa Kitui East Nimrod Mbai kuhusiana na kauli zake kwamba mtu yeyote atakayemkosea heshima Rais William Ruto eneo hilo hatahakikishiwa uhuru wake, kauli ambazo zimehusishwa na kushambuliwa kwa mwakilishi wadi maalum Jacinter Mwoni. Kupitia taarifa ya katibu mkuu wa chama hicho Shakila Abdallah, Wiper imetaja tukio hilo kuwa […]

ATAHESHIMU MAHAKAMA? RUTO NJIA PANDA

Hatma ya IEBC mpya sasa iko mikononi mwa mahakama kuu, ambayo uamuzi wake utaamua iwapo Rais William Ruto atachapisha kwenye gazeti rasmi la serikali au la, majina ya watu 7 akiwemo mwenyekiti Erastus Ethekon na makamishna 6 na kisha kuapishwa kwao. Hii ni baada ya bunge hapo jana kwa kauli moja kuidhinisha uteuzi wa 7 […]

KOSKEI AWAONYA MAKATIBU WA WIZARA

Makatibu wakuu wanaohudumu katika wizara tofauti watalazimika kuwajibikia visa vya ufisadi unaoripotiwa katika wizara zao. Ni onyo iliyotolewa na mkuu wa utumishi wa umma Felix Koskei anayesema hataruhusu rais William Ruto kulaumiwa kwa visa vya ufisadi ilhali ni wakuu hao wanaosimamia shughuli za uagizaji. Ametaka pia kuripotiwa kwa maafisa wa serikali wanaotumia visivyo fedha za […]