WAHUDUMU WA UHC WAKANA KUWA ‘HEWA’

Utata unaokumba uajiri wa wahudumu wa afya ya wote UHC umechukua mkondo tofauti, wahudumu hao sasa wakipinga madai ya mwenyekiti wa kamati ya afya katika baraza la magavana na ambaye pia ni gavana wa Tharaka Nithi Muthomi Njuki kwamba kuna wafanyakazi hewa zaidi ya 3,000 miongoni mwao. Kulingana na wahudumu hao, madai ya gavana huyo […]

WABUNGE KENYA, UGANDA CHINI YA SHINIKIZO

Wabunge wa Kenya na Uganda wamejipata chini ya shinikizo, wakitakiwa kuziwajibisha serikali zao kuhusiana na taarifa za kuteswa kwa wanaharakati Boniface Mwangi na Agather Atuhaire wakiwa nchini Tanzania. Mbali na kuwajibishwa kwa wahusika, mashirika ya kutetea haki za kibinadamu yakiongozwa na chama cha wanasheria nchini LSK, yametaka serikali ya Tanzania kuwafidia wanaharakati hao. Katika taarifa […]

REKODI MPYA YA AKIBA YA DOLA NCHINI, RUTO

Kwa mara ya kwanza kabisa, Kenya imefanikiwa kuhifadhi akiba za dola bilioni 10.3 kwenye akiba zake, hatua hiyo ikiashiria kuendelea kwa ukuaji wa uchumu wa nchi. Haya ni kwa mujibu wa Rais William Ruto, akitaja kiwango hicho cha hifadhi kuwa chanzo cha juhudi za Pamoja katika kuzingatia ushauri wa wataalamu wa masuala yaa uchumi nchini. […]

MPANGO WA SHA KUBORESHWA

Wakenya wataanza kufaidi zaidi na mpango wa bima ya afya wa SHA baada ya wizara ya afya kuanzisha mpango wa kuuboresha. Afisa mkuu anayesimamia mpango huo Dkt Mercy Mwangangi ameelezea masikitiko yake kuwa wengi wa wakenya hawaelewi manufaa yanayotokana na mpango huo. Mwangangi ameanza rasmi kutekeleza majukumu yake kama msimamizi wa bima hiyo. Imetayarishwa na […]

ROSE NJERI AACHILIWA KWA DHAMANA.

Mwanaharakati Rose Njeri yuko huru baada ya kuachiliwa kwa dhamani ya shilingi laki moja baada ya kufikishwa kotini mapema leo. Njeri alikamatwa baada ya kuanzisha tovuti ya kuwawezesha wakenya kuwasilisha maoni yao kuhusu mswada wa fedha wa 2025 26 kwa karani wa bunge hatua iliyodaiwa kutatiza shughuli za bunge. Hakimu Geoffrey Onsarigo atatoa uamuzi wake […]

ROSE NJERI AFIKISHWA KOTINI

Mwanaharakati na mtaalam wa masuala ya mitandao Rose Njeri amefikishwa mahakamani hapa Nairobi akikabiliwa na kesi ya kuwachochea wakenya dhidi ya mswada wa fedha wa 2025 26. Miongoni mwa wanaomtetea Njeri ni Pamoja na aliyekuwa jaji mkuu David Maraga na kinara wa chama cha wiper Kalonzo Musyoka wakikosoa kukamatwa kwake. Njeri anatuhumiwa kwa kuanzisha mchakato […]

MAHAKAMA YATAKA USHAHIDI DHIDI YA NATEMBEYA

Wafanyikazi 3 wa serikali ya kaunti ya Trans nzoia wanadaiwa kukamatwa baada ya kuhudhuria mkao wa kesi ya ufisadi inayomkabili gavana wa kaunti hiyo George Natembeya. Haya yamejiri huku mahakama ikiagiza upande wa mashtaka kwenye kesi hiyo kuwasilisha Ushahidi wanaolenga kutumia dhidi ya Natembeya baada yao kukosa kufuata agizo la kuwataka kufichua stakabadhi wanazolenga kutumia […]

UAJIRI SHA WAPIGWA BREKI

Mahakama ya uajiri na leba imetoa pigo kwa mchakato wa uajiri wenye utata wa Mamlaka ya Afya ya Jamii (SHA) baada ya kutoa uamuzi kwamba matangazo yake ya ndani yaliyokuwa yanawahusu waliokuwa wafanyakazi wa Bima ya Afya ya taifa (NHIF) yalikuwa ya kibaguzi na kinyume na Katiba. Jaji Byram Ongaya, akitoa uamuzi katika ombi lililowasilishwa […]

KOCHA MUFUTU ATOA ONYO KALI KWA KIKOSI CHAKE

KOCHA Mkuu wa Ulinzi Warriors, Bernard Mufutu ametoa onyo kali kwa kikosi chake dhidi ya kuzembea katika Ligi ya Kitaifa ya Mpira wa Kikapu (KNBL), kufuatia wikendi ya uchezaji tofauti. Wanajeshi hao walipoteza kwa vikapu 70-68 kwa mabingwa watetezi Nairobi City Thunder siku ya Ijumaa, kabla ya kurejea na ushindi wa 81-65 dhidi ya Eldonets […]

BUNGOMA QUEENS WAINGIA FAINALI

KLABU ya Ligi Kuu ya Wanawake ya Shirikisho la Soka la Kenya (FKF-WPL) Bungoma Queens imepania kutinga fainali ya Kombe la Wanawake la FKF baada ya kung’oa Trinity Starlets katika robo-fainali wikendi. Ushindi wao uliifanya Bungoma Queens kuchuana na Vihiga Queens katika nusu fainali iliyotarajiwa kuchezwa Alhamisi. Bungoma Queens, ambao wameimarika kwa kasi katika kipindi […]