BUNGE LAIDHINISHA MAKAMISHNA WA IEBC

Makamishna 6 walioteuliwa kuhudumu katika tume ya IEBC Pamoja na mwenyekiti wake wameidhinishwa rasmi na bunge baada ya kuwasilishwa na kujadiliwa kwa ripoti ya kamati ya haki na sheria JLAC bungeni. Wabunge kwa Pamoja wameidhinisha saba hao kuhudumu katika tume ya IEBC na sasa kilichosalia ni kuchapishwa rasmi kwa majina yao kwenye gazeti rasmi la […]

MAHAKAMA YAIDHINISHA KUONDOLEWA KWA SPIKA NYAMIRA

Aliyekuwa spika wa bunge la Nyamira Enock Okero aliondolewa afisini kisheria kulingana na uamuzi wa mahakama ambayo imetupilia mbali notisi zote zilikuwa zimetolewa na Okero. Jaji wa mahakama kuu ya Bomet Julius Ng’aring’ari anasema vigezo vyote vya sheria vilizingatiwa wakati wa kubanduliwa kwake afisini. Nafasi yake ilichukuliwa na mwakilishi wa wadi ya Ekerenyo Thaddeus Nyabaro. […]

WASHUKIWA WA MAUAJI YA WERE KUCHUNGUZWA

Washukiwa 2 wa mauaji ya mbunge wa Kasipul Charles Were watafanyiwa uchunguzi wa akili kabla ya kufunguliwa mashtaka, kufuatia agizo la mahakama. Jaji Magret Muigai ameagiza Isaack Kuria na Allan Omondi Ogolla wafanyiwe uchunguzi huo na kuzuiliwa katika gereza la Kamiti. Were aliwawa kwa kupigwa risasi mwezi Aprili Nairobi na mshukiwa aliyetoweka kwa kutumia pikipiki. […]

NANE WAFARIKI KWENYE AJALI MWINGI

Idadi ya watu waliofariki kwenye ajali ya barabarani katika eneo la Mwingi huko Kitui imefikia nane. Ajali hiyo ilihusisha matatu ya abiria 14 iliyobingiria na kuanguka kwenye barabara ya Mwingi kuekelea Nairobi watu 5 wakifariki papo hapo.Watu wengine 3 wamefariki wakipokea matibabu,na wale walionusurika wanatibiwa katika hospitali ya Matuu. Imetayarishwa na Maureen Makhobe

CECAFA YA WANAWAKE KUANZA MWEZI HUU

Mashindano ya CECAFA kwa Wanawake 2025 yamepangwa rasmi kuanzia Juni 12 hadi 22 jijini Dar es Salaam, Tanzania. Kwa mujibu wa Yusuf Mossi, Mkurugenzi wa Mashindano katika Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), uamuzi wa kuandaa michuano hiyo kabla ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake la CAF (WAFCON) ulikuwa […]

JADON SACHO AREJEA MACHESTER UNITED

Chelsea imeamua kutomsajili winga Jadon Sancho kwa mkataba wa kudumu na badala yake italipa ada ya pauni milioni 5 ili kumrudisha mchezaji huyo Manchester United. Mshambuliaji huyo wa Uingereza alihamia Stamford Bridge kwa mkopo msimu uliopita wa joto baada ya uhusiano wake na meneja wa zamani wa United Erik ten Hag kuvunjika. United, ambao walimsajili […]

OTERE APANIA KUNYAKUA TAJI LA MPIRA WA WAVU

Kocha mkuu wa Klabu ya Mpira wa Wavu ya Mamlaka ya Bandari ya Kenya James Ontere analenga kusaidia klabu hiyo yenye makao yake makuu mjini Mombasa kunyanyua taji lao la kwanza watakapomenyana na mabingwa wa rekodi ya GSU katika fainali inayotarajiwa kufanyika Juni 6-8, 2025, uwanaj wa ndani wa Kasarani. Ontere anasalia na furaha kuhusu […]

HESHIMA IDUMU KWA WANYAMA

Kocha mkuu wa Harambee Stars Benni McCarthy ametaka heshima idumishwe kwa nahodha wa zamani Victor Wanyama. McCarthy anasema Wanyama ni nyota wa taifa ambaye ameiweka nchi kwenye ramani ya dunia kutokana na kuchezea baadhi ya vilabu maarufu duniani. Wanyama aliitwa tena kwenye timu ya taifa wiki jana, kabla ya mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi […]

UN YAONYA MZOZO WA SUDAN KUINGIA KWA MAJIRANI

Idadi ya watu waliotoroka nchini Sudan tangu kuzuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka wa 2023 imezidi milioni 4, shirika la umoja wa mataifa kuhusu wakimbizi likisema kuwa wengi wa wahanga wa vita hivyo walikabiliwa na uhabawa makazi. Kwenye kikao na wanahabari jijini Geneva, nchini Uswizi, msemaji wa shirika hilo Eujin Byun, amesema iwapo […]

MAAFISA 5 TRANS NZOIA KUFIKISHWA KORTINI

Maafisa 5 wa kaunti ya Trans Nzoia akiwemo mwakilishi wadi ya Sinyerere John Makhanu, wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mjini Kitale hii leo baada ya kukamatwa nje ya mahakama ya Milimani jijini Nairobi hapo jana walipokuwa wakihudhuria kesi ya gavana George Natembeya. Kwa mujibu wa idara ya polisi, maafisa hao wanashukiwa kuwafadhili wahuni walioharibu magari ya tume […]