MAAFA YA MAANDAMANO

Watu 8 wameripotiwa kuaga dunia huku wengine zaidi ya 400 wakijeruhiwa hapo jana kwenye makabiliano kati ya polisi na waandamanaji waliokuwa wakiadhimisha mwaka mmoja tangu kuuawa kwa zaidi ya wakenya 60 wakati wa maandamano ya mwaka jana. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa tume ya kitaifa kuhusu haki za kibinadamu Dakta Raymond Nyeris, maafa hayo yaliripotiwa […]

KANJA AWATAKA WAANDAMANAJI KUJITENGA NA MAENEO YALIYO CHINI YA ULINZI

Idara ya polisi imewatahadharisha wakenya watakaoshiriki maandamano hapo kesho kujitenga na maeneo yaliyo chini ya ulinzi. Katika mkao na wanahabari akiwa ameandamana na wakuu wengine wa usalama Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja anasema polisi watazingatia sheria watakapotekeleza majukumu yao na kuwataka raia kushirikiana nao. Imetayrishwa na Maureen Mukhobe

WASHUKIWA WA MAUAJI YA OJWANG WAKANA MASHTAKA

Washukiwa 6 wanaohusishwa na mauaji ya mwalimu Albert Ojwang wamefikishwa mahakamani leo na kukanusha mashtaka dhidi yao. Sita hao akiwemo ocs wa kituo cha polisi cha central Samson Talam wametaka mahakama kuwaachilia kwa dhamana ombi ambalo limepingwa na mawakili wa upande wa mashtaka. Imetayrishwa na Maureen Mukhobe

WATAKAOCHOKOZA POLISI WAONYWA

Wakenya watakaojitokeza kushiriki maandamano ya hapo kesho wameonywa dhidi ya kuwadhalilisha ama kuwachokoza polisi. Rais William Ruto anasema watakaofanya hivyo watakabiliwa na mkono wa sheria na kuwa jukumu la polisi ni kuimarisha doria na kuweka mazingira na ulinzi kwa waandamanaji. Naye waziri wa usalama Kipchumba Murkomen ametaka kuchukuliwa hatua watakaotishia kuvamia idara na taasisi za […]

KENYA YAPOKEA MKOPO MPYA

Kenya imetia saini mkopo wa masharti nafuu wa $126.8 milioni kutoka hazina ya Kimataifa ya Maendeleo ya Kilimo (IFAD) ili kufadhili mpango mpya unaolenga kuboresha maisha ya watu wa mashambani na kulinda maliasili. Kulingana na waziri wa fedha John Mbadi, Mpango Jumuishi wa Usimamizi wa Maliasili (INReMP) unalenga kushughulikia uharibifu wa mazingira, mabadiliko ya hali […]

ARSENAL WAVUTIWA NA MADUEKE

Arsenal wanavutiwa na winga wa Chelsea na wa kimataifa wa Uingereza Noni Madueke, linaripoti Independent. The Gunners wameripotiwa kujadili kuhusu kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 baada ya kuhangaika kufanya mazungumzo na Benjamin Sesko wa RB Leipzig, na inaaminika kuwa The Blues watakuwa tayari kuachana na Madueke iwapo watapata ofa yenye thamani ya […]

KIKOSI CHA TWINKLE KINAPANGA KUREJESHA USHINDI KATIKA LIGI YA WANAWAKE

Klabu ya Mpira wa Magongo ya Twinkle ya Kenya imeazimia kurejesha fomu yao ya ushindi katika Ligi Kuu ya Wanawake ya Mpira wa Magongo ya Kenya, huku ikilenga kujinasua kutoka kwenye eneo la kushushwa daraja na kujiimarisha miongoni mwa timu zinazoongoza. Wakiwa wamepandishwa daraja la juu msimu huu kutoka kwa Super League, Twinkle kwa sasa […]

TEREMI BOYS WALENGA KUBEBA TAJI LA MAGHARABI

MABINGWA wa kandanda kaunti ya Bungoma Shule ya Upili ya Teremi Boys wanalenga kunyakua taji la eneo la Magharibi baada ya kufuzu kwa mara ya kwanza, na kusimamisha kila mtu kutwaa taji la kaunti hiyo. kocha mkuu wa Teremi, Moses Wafula aliwahakikishia wafuasi wa timu hiyo na wakazi wa Bungoma kwamba ubingwa wa eneo hilo […]

KOCHA WA ZETECH ALAUMU KLABU CHAKE KW AMWANZO MBAYA

Licha ya ushindi mnono dhidi ya mabingwa watetezi Equity Hawks, kocha mkuu wa Zetech Sparks Maurice Obilo alikiri kwamba timu yake haikuanza na mwanzo mzuri katika pambano lao la wikendi. Zetech iliishinda Equity 69-61 katika mechi ya Ligi Kuu ya Kikapu ya Kitaifa ya Wanawake ya Kenya iliyoandaliwa katika uwanja wa Nyayo Gymnasium, Nairobi. Ushindi […]

KINDIKI AENDELEA KUMWITA MUSYOKA SERIKALINI

Naibu Rais Kithure Kindiki ameendeleza juhudi zake za kuitafutia serikali uungwaji mkono wa kisiasa kutoka eneo la Ukambani, akimtaka kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka ajiunge na serikali ya Kenya Kwanza. Akizungumza baada ya kufanya mkutano na zaidi ya wawakilishi wadi 100 kutoka kaunti za Makueni, Machakos na Kitui, Kindiki amemtaka Musyoka kujiepusha na mrengo ambao […]