SITA WAKABILIWA NA KESI MAUAJI YA OJWANG

Washukiwa 6 akiwemo OCS wa kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi Samson Taalam watarejeshwa mahakamani hii leo kufunguliwa rasmi kesi ya mauaji ya mwalimu na bloga Albert Ojwang aliyeuawa katika kituo hicho. Hii ni baada ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma DPP Renson Ingonga kuidhinisha mashtaka ya mauaji dhidi yao, mamlaka ya kuchunguza mienendo […]

WAZAZI KUENDELEA KULIPA KARO YA ZIADA, KESSHA YATANGAZA

Huenda wazazi wakaendelea kulipa karo ya ziada baada ya muungano wa walimu wakuu wa shule za upili KESSHA kutangaza kuwa hautazingatia agizo la mahakama lililoharamisha malipo hayo, kwa misingi kwamba shughuli zitalemazwa shuleni kutokana na mgao finyu. Akizungumza jijini Mombasa kwneye matayarisho ya kongamano la kila mwaka la muungano huo, mwenyekiti wake Willy Kuria amesema […]

ADA YA MATIBABU YA KARIUKI YAZIDI KUONGEZEKA

Familia ya mchuuzi aliyepigwa risasi ya mpira na kuwaachwa na majeraha mabayaitahitajika kulipia ada ya matibabu inayozidi shilingi milioni 2. Jamaa zake Bonface Kariuki wanasema mwanao ambaye angalia anatumia mitambo ya kumweka hai hawezi kuzungumza wala kuwaona na hali yake haijabadilika ada ya matibabu nayo ikifikia shilingi milioni 2.3. Haya yanajiri huku mkuu wa polisi […]

WASHUKIWA WA MAUAJI YA OJWANG WAKOSA KUSOMEWA MASHTAKA

Washukiwa 6 wanaohusishwa na kifo tata cha mwalimu Albert Ojwang wamekosa kusomewa mashtaka ya mauaji yanayowakabili baada ya kufikishwa katika mahakama ya Kibera alasiri hii. Hii ni baada ya baadhi yao kudai kukosa mawakili wa kuwaakilisha kwenye kesi hiyo baada ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma ODPP kuidhinisha washtakiwe. Sita hao akiwemo Samson Kiprotich Talam,James […]

ODPP AIDHINISHA TALAM NA WENZAKE KUSHTAKIWA KWA MAUAJI

Washukiwa 6 wanaohusishwa na kifo tata cha mwalimu Albert Ojwang sasa watashtakiwa kwa mauaji baada ya mamlaka ya ipoa kupata idhini ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma ODPP. Sita hao akiwemo Ocs wa kituo cha polisi cha central Samson Talam wanatarajiwa sasa kuwasilishwa katika mahakama ya Kibera kusomewa mashtaka dhidi yao. Afisi ya ODPP imeafikia […]

DAWA 77 ZA KUUA WADUDU ZAPIGWA MARUFUKU

Waziri wa kilimo Mutahi Kagwe ametangaza kupigwa marufuku kwa aina 77 ya dawa za kuua wadudu shambani kutokana na sababu za kiusalama. Katika ujumbe Mutahi anasema wamechukua hatua hiyo ili kuhakikisha kuwa dawa zinazotumika nchini ni salama kwa binadamu na kwa mazingira. Hii ni baada ya ukaguzi ulioendeshwa na bodi ya kudhibiti matumizi ya dawa […]

MSHUKIWA WA MAUAJI ANA MATATIZO YA KIAKILI, RIPOTI

Juhudi za kusaka haki kwa familia ya Sylvia Kemunto ambaye alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu cha Multimedia zimepata pigo baada ya kubainika kuwa mshukiwa mkuu wa mauaji ya mwanafunzi huyo Eric Mutinda hayuko sawa kiakili na hivyo kesi ya mauaji dhidi yake haiwezi kuendelea kwa sasa. Hii ni kufuatia ripoti ya uchunguzi wa kiakili uliofanywa […]

KINDIKI: HAKUNA ANAYEWEZA KUUA UGATUZI

Naibu Rais Kithure Kindiki amewahakikishia Wakenya kwamba serikali haina mpango wa kuhujumu hatua zilizopigwa kuhusiana na ugatuzi nchini katika kipindi zaidi ya miaka 10 iliyopita. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha 27 cha mkutano wa baraza la bajeti na uchumi linalojumuisha serikali za kaunti na ile ya kitaifa IBEC katika ofisi yake ya Karen, […]

POLISI WAONYA DHIDI YA ‘KUJILINDIA’ BIASHARA

Idara ya polisi imewaonya wafanyabiashara kuwakodisha vijana kuwalindia biashara wakati wa maandamano na badala yake wakatakiwa kuwaruhusu maafisa wa polisi kutekeleza jukumu hilo. Kupitia taarifa, msemaji wa polisi Muchiri Nyaga ameonya kuwa hatua hiyo ni kinyume na sheria, akisisitiza kuwa ni jukumu la polisi kuhakikisha usalama wa mali, na uharibifu wa aina yoyote utakabiliwa kisheria. […]

CITY WAINGIA AWAMU YA MWONDOANO

Kiungo wa Manchester City Ilkay Gundogan ameifungia klabu hiyo mabao mawaili katika ushindi wa mabao 6 kwa bila dhidi ya Al-Ain na kujikatia tiketi ya awamu ya mwondoano yaani last 16 mapema leo katika mashindano ya kombe la dunia la klabu yanayoendelea nchini Marekani. City waliowacharaza Wydad AC mabao 3:0 kwenye mechi ya ufunguzi, watahitaji […]