WABUNGE KUJADILI MAREKEBISHO YA SHERIA YA MAANDAMANO

Wabunge wameratibiwa kujadili na kupigia kura pendekezo la marekebisho ya sheria inayohusu maandamano linalolenga kuzuia uvamizi na taasisi nyingine za serikali wakati wa maandamano nchini. Mswada huo uliopendekezwa na mwakilishi wa kike wa kaunti ya Nairobi Esther Passaris mbele ya kamati ya usalama na utawala, tayari umeanza kupata uungwaji mkono wa wabunge. Miongoni mwa mapendekezo […]

HATMA YA HAZINA ZA NG-CDF, NGAF SENETI

Wakenya sasa wameelekeza macho yao kwa bunge la seneti kuhusu uidhinishwaji wa mswada unaolenga kuzijumuisha kwenye katiba hazina 3 katika katiba kwa lengo la kuzilinda hazina hizo na kukuza maendeleo katika maeneo ya mashinani, baada ya wabunge kuupitisha mswada huo hapo jana. Hazina hizo ni NG-CDF, hazina ya uangalizi wa maseneta na hazina ya kitaifa […]

UPINZANI WAMTAKA MURKOMEN NJE

Viongozi wa upinzani Kalonzo Musyoka na Eugene Wamalwa wanashinikiza kujiondoa afisini kwa waziri wa usalama Kipchumba Murkomen kufuatia kifo cha mchuuzi Boniface Kariuki aliyefariki kutokana na jeraha la risasi kichwani. Wakizungumza baada ya kuitembelea familia hiyo, viongozi hao wamekariri kuwa Murkomen anafaa kuwajibikia kifo hicho. Familia hiyo kwa sasa anaendeleza mipango ya mazishi ya jamaa […]

MATIANG’I AZUNGUMZIA MAUAJI YA MTO YALA

Waziri wa zamani wa usalama Dakta Fred Matiang’i, amevunja kimya chake kuhusu mauaji yaliyogonga vichwa vya habri alipokuwa waziri, ikiwemo miili kupatikana katika mto Yala na mauaji ya aliyekuwa afisa wa IEBC Chris Musando. Kwenye mahojiano yaliyopeperushwa na runinga moja hapo jana, Matiang’i amesema kuwa yuko tayari kufika mahakamani iwapo ataagizwa kufanya hivyo, akiilaumu serikali […]

19 WAACHILIWA NA MAHAKAMA YA OLKALOU

Washukiwa 19 waliohusishwa na vurugu wakati wa maandamano ya Juni 25 huko Nyandarua wameachiliwa kwa bondi na mahakama ya Olkalou. Hakimu Judicaster Nthuku aliagiza kuachiliwa kwao kwa bondi ya shilingi laki moja kila mmoja akisema upande wa mashtaka haujatoa sababu za kutosha kutaka waendelee kuzuiliwa. Imetayarishwa na maureen amwai

DCI YAAGIZWA KUMWASILISHA NDIANG’UI KOTINI

Mahakama imemuagiza Mkuu wa Dci Mohammed Amin kumwasilisha kotini mwana blogu Ndiang’ui Kinya,gia siku ya alhamisi awe hai ama maiti. Jaji Chacha Mwita amewataka mawakili wanaomwakilisha Amin kusitisha sarakasi na kutii agizo la mahakama. Anasema Kinyagia alichukuliwa nyumbani kwake na maafisa wa Dci na wanastahili kueleza aliko. Imetayarishwa na maureen amwai

AL HILAL YASAMBARATISHA MANCITY

Kocha wa Al Hilal Muitaliano Simone Inzaghi aliipongeza timu yake ya “ajabu” baada ya ushindi wa Jumatatu wa mabao 4-3 katika muda wa ziada dhidi ya wababe wa Ligi Kuu ya Uingereza Manchester City kwenye Kombe la Dunia la Vilabu. Inzaghi alikuwa ameiongoza timu hiyo kwa siku chache tu kabla ya mchezo wa ufunguzi ambapo […]

GOFU YA KENYA YAIMARIKA

Kenya imethibitisha kuimarika kwake katika soko la kimataifa la utalii wa gofu kufuatia kuandaliwa vyema kwa Mashindano ya 16 ya Dunia ya Gofu ya Baraza la Kimataifa la Michezo ya Kijeshi (CISM). Hafla hiyo ya wiki moja, iliyofanyika kuanzia tarehe 22 hadi 29 Juni katika ukumbi wa Diamonds Leisure Beach and Golf Resort katika Kaunti […]

ONYANGO AONDOKA STELLENBOSCH

Beki wa kimataifa wa Kenya Brian Onyango yuko mbioni tena kutafuta klabu mpya baada ya kumalizika kwa muda wake katika klabu hiyo ya Afrika Kusini. Onyango alijiunga na klabu hiyo mwanzoni mwa msimu wa 2024-25 na aliweza kucheza mechi nane pekee katika michuano yote, na kuisaidia klabu hiyo kufika fainali ya MTN8 na kufuzu kwa […]

DONDOO ZA UHAMISHO EPL

Manchester United wanaweza kumwania Ollie Watkins wa Aston Villa kuongoza safu yao, huku Bayern Munich watafikiria dili la Luis Diaz na Arsenal wamfukuzie Eberechi Eze wa Crystal Palace. Huku hayo yakijiri wanatatizika kumwondoa Tyrell Malacia, 25, baada ya PSV Eindhoven kukataa nafasi ya kumsajili beki huyo wa Uholanzi kabisa baada ya kukaa kwa mkopo. Naye […]