ASATI ANA IMNAI WATAWALAMBISHA KIVUMBI UGANDA

Nyota wa KCB RFC, Samuel Asati ana uhakika Simbas ya Kenya itawaangusha wapinzani wao Uganda katika mechi yao ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la Raga ya 2027 itakayoandaliwa wiki ijayo. Timu hiyo ilisifu kambi ya hivi majuzi ya mazoezi ya kikosi hicho yenye ufanisi wa hali ya juu nchini Afrika Kusini, ambapo walishiriki katika […]

GOR YATIMUA BENCHI LOTE LA UFUNDI

Vigogo wa soka nchini Kenya, Gor Mahia FC wametimua benchi yao yote ya ufundi, akiwemo kocha wa muda Zedekiah ‘Zico’ Otieno na maafisa wa usalama, katika kile klabu inachokitaja kuwa ni “kutengana kati yao. Uamuzi huo, uliotangazwa katika taarifa rasmi Jumatano, unakuja siku mbili tu baada ya Gor Mahia kushangazwa 2-1 na mabingwa wa Ligi […]

KENYA KUJIUNGA NA EBRD

Kenya inatazamiwa kuwa mwanachama wa Benki ya Ulaya ya Kujenga Upya na Maendeleo (EBRD) kufuatia kuidhinishwa kwa kauli moja na Bunge la Kitaifa, kuashiria hatua muhimu katika msukumo wa nchi wa kuimarishwa kwa maendeleo ya miundombinu na ukuaji wa uchumi. Uidhinishaji huo unaweka Kenya kama nchi ya sita ya Afrika-baada ya Benin, Côte d’Ivoire, Ghana, […]

MSWADA WA MAANDAMANO WAPOKEA PINGAMIZI

Mswada uliopendekezwa wa kuifanyia marekebisho sheria kuhusu maandamano umeendelea kupingwa, wa hivi punde kutoa ukosaji wake akiwa ni gavana wa Makueni Mutula Kilonzo Junior ambaye ameutaja kuwa wenye kulirejesha taifa nyuma na kutishia haki za kidemokrasia. Kupitia taarifa, Mutula amehoji kuwa taasisi kama vile bunge zinafaa kufikiwa na wananchi na wala si kuzuiwa kuzifikia. Kulingana […]

MIHEMKO YA UHAMISHO KATIKA LIGI KUU YA UINGEREZA

Bayern Munich wanafikiria kumnunua Marcus Rashford, Arsenal wanakaribia kumnunua Viktor Gyokeres, Crystal Palace wakubali bei ya pauni milioni 47 kwa Ousmane Diomande. Bayern Munich wanafikiria kumnunua fowadi wa Manchester United na Muingereza Marcus Rashford, 27, baada ya kufurahishwa na kiwango chake cha mkopo Aston Villa msimu uliopita. Arsenal wanakaribia kufikia makubaliano ya kumnunua mshambuliaji wa […]

OCHOLLA AJIVUNIA BAADA YA USHINDI MARA MBILI

Kocha mkuu msaidizi wa timu ya wanawake ya KPA Kenya Samuel Ocholla amepongeza hatua yake baada ya kusajili ushindi mara mbili wikendi. The Dockers walipeana kichapo cha 84-38 dhidi ya The Swish Jumamosi kabla ya kupepeta The Storms 87-44 siku ya Jumapili katika Ukumbi wa Makande Gymnasium, Mombasa. Licha ya mwendo mzuri, mtaalamu huyo anayezungumza […]

HAIKUA RAHISI KUPATA USHINDI ASEMA OBILO

kocha mkuu wa Zetech Sparks Maurice Obilo amekiri kwamba haikuwa kazi rahisi kupata ushindi ugenini mjini Eldoret katika mechi nyingine ya Ligi Kuu ya wanawake. Wanafunzi hao waliwashinda Eldonets 70-43 mjini Eldoret katika uwanja wa Uasin Gishu ili kuweka hai matarajio yao ya msimu Imetayarishwa na Nelson Andati

CITY WAONDOKA JAPO NA KITITA CHA ZAWADI

Kujiondoa kwa Manchester City kutoka Kombe la Dunia la Vilabu mikononi mwa Al-Hilal siku ya Jumatatu hatimaye kumepunguza pazia la msimu mbaya kwa kikosi cha Pep Guardiola huku kikithibitisha kwamba vigogo barani Ulaya hawana chochcote cha kujivunia katika mashindano mapya ya FIFA. City walikuwa wamesafiri hadi Marekani kutoka nyuma ya kampeni ya kukatisha tamaa nchini […]

POLICE FC WAPO TAYARI KWA MICHEZO YA CAF

Meneja wa timu ya Police FC George Maelo amethibitisha kuwa klabu yake itakuwa tayari kwa mechi ya Ligi ya Mabingwa ya CAF wakati mchuano wa kandanda wa klabu bingwa barani utakapoanza msimu ujao. Polisi walishinda taji lao la kwanza kabisa la ligi mwaka huu na kujiwekea nafasi ya kuwakilisha nchi katika mashindano ya bara katika […]

ALILA ATAKA GOR NA AFC KUBORESHA UONGOZI WAO

Aliyekuwa mgombea urais wa FKF Tom Alila ametoa changamoto kwa Gor Mahia, AFC Leopards na Shabana FC kuboresha mfumo wao wa uongozi kwa kupitisha bodi za kuziongoza. Kulingana na Alila, mtindo huu wa uongozi utaweka akili timamu, uwajibikaji, na usimamizi ufaao utakaokuza viwango vya soka miongoni mwa vilabu ili kuwezesha ushindani mkali katika ligi yetu […]