HAMNA SHINIKIZO KWA NAIBOIS, MUYOTI

Kocha mkuu wa Nairobi United Nicolas Muyoti ameelezea matumaini ya timu yake kumaliza miongoni mwa 5 bora msimu huu wa kwanza katika ligi kuu nchini, akisema hawana shinikizo za kupigania taji hilo msimu huu. Muyoti ambaye awali alikuwa kocha mkuu wa City Stars na Kakamega Homeboyz, amesema klabu hiyo itaanza kuangazia kutwaa taji hilo baada […]

KPA MACHO SASA WBLA

Klabu ya mpira wa vikapu ya Kenya Ports Authority KPA imeimarisha maandalizi yake inapojiandaa kushiriki Ligi ya wanawake ya mchezo hio barani Afrika WBLA baadaye mwishoni mwa wiki hii nchini Misri. KPA wanalenga kutumia uzoefu wao kujitangaza katika kiwango cha bara kwenye mashindano hayo. Kwa mujibu wa naibu mkufunzi Samuel Ocholla, kikosi hicho kinalenga kutumia […]

WABUNGE WATEULE KUAPISHWA

Wabunge waliochaguliwa kwenye chaguzi ndogo wiki jana wameratibiwa kuapishwa hii leo bungeni ili kuanza rasmi majukumu yao ya uwakilishi, utungaji sheria na uangalizi dhidi ya serikali ya kitaifa. Wabunge hao ni David Ndakwa wa Malava, Harrison Kombe wa Magarini, Leo wa Muthende wa Mbeere North, Boyd Were wa Kasipul, Ahmed Maalim Wa Banisa na Moses […]

NTSA YATANGAZA MSAKO BARABARANI

Wasafiri wamehakikishiwa usalama wao barabarani hasa msimu huu wa Krisimasi, mamlaka ya usalama barabarani NTSA ikitangaza msako mkali dhidi ya madereva wanaokiuka sheria za trafiki. Kwenye msako huo, NTSA itategemea mahakama tamba zitakazohakikisha kuwa madereva wanaokamatwa wanashtakiwa na kuhukumiwa papo hapo, mbali na utekelezaji wa vifaa vya kudhibiti mwendo. Aidha, wakenya wameruhusiwa kurekodi video za […]

RUTO AMWAGIZA IG KUMALIZA UHUNI

Macho yote sasa yameelekezwa kwa idara ya polisi kuanzisha msako na kuwakamata washukiwa wa uhuni ambao wamekuwa wakivuruga mikutano ya kisiasa kote nchini, mwathiriwa wa hivi punde akiwa aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua Jumapili iliyopita. Akitoa amri yake, Rais William Ruto amemwagiza Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja kuhakikisha washukiwa wote wanakamatwa ili kulihakikishia taifa […]

WIPER ‘YAMRUKA’ GACHAGUA

Tofauti za kisiasa zimeibuka kwenye muungano wa upinzani, kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka akipuzilia mbali madai ya mwenzake wa DCP Rigathi Gachagua kwamba Wiper itawaunga mkono wagombeaji wa DCP katika kaunti ya Nairobi kwenye uchaguzi mkuu ujao. Kwa mujibu wa Gachagua, wameafikiana na Musyoka kuwaondoa wagombeaji wa Wiper ili kuwapisha wa DCP kwenye uchaguzi huo. […]

ICC YAFUNGA RASMI UCHUNGUZI KENYA

Hatimaye miaka ya uchunguzi kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 imefikia kikomo baada ya mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu ICC kufunga rasmi uchunguzi wake kuhusu hali ya Kenya. Katika taarifa yake, afisi ya mwendesha mashtaka mahakamani humo Karim Khan, imesema ilikamilisha uchunguzi wake kuhusu ghasia hizo Novemba 27 mwaka 2023. […]

MAHAKAMA YABATILISHA USHURU WA MAPISHI

Wakenya wanatazamiwa kunufaika na bei ya chini ya mafuta ya kupikia baada ya Mahakama Kuu kubatilisha uamuzi wa serikali wa kutoza ushuru wa asilimia 10 kwa mafuta ghafi.Katika uamuzi wa Jaji Bahati Mwamuye, mahakama imetangaza ushuru huo kuwa kinyume na katiba, ikitaja ukosefu wa kibali cha bunge na ushirikishwaji wa maana wa umma. Ushuru huo, ulioanzishwa Julai […]

ARTETA ATETEA ARSENAL, FODEN AKIOKOA CITY

Kocha mkuu wa Arsenal Mikel Arteta amesema kuwa klabu hiyo inastahili heshima licha ya sare ya bao 1 dhidi ya Chelsea ugani Stamford Bridge. Arsenal walio na orodha ya majeruhi, walijizatiti na kuokoa pointi, baada ya Chelsea waliokuwa 10 kufuatia kadi nyekundu ya kiungo Moses Caicedo kuchukua uongozi kupitia kwa Trevor Chaloba. The Blues walilazimika […]

HOMEBOYZ WAPOTEZA FURSA TENA

Klabu ya Kakamega Homeboyz ilipoteza fursa ya kurejea kileleni kwa ligi ya KPL, kufuatia sare ya goli 1 dhidi ya KCB FC hapo jana. Homeboyz wana pointi 19 sawa na Gor Mahia, ila wanadunishwa na ubora wa mabao mbali na kucheza mechi 2 zaidi ya wenzao Gor. Katika matokeo mengine, Shabana FC walikosa adabu na […]