FKF KUIMARISHA SOKA KUFUATIA MASAIBU YA JUNIOR STARS

Shirikisho la soka nchini FKF limedokeza kuimarisha soka ya vijana baada ya timu ya taifa ya vijana wasiozidi umri wa miaka 17 Junior Starlets kunyimwa tiketi ya kufuzu mashindano ya mataifa bingwa barani Afrika kwa chipukizi AFCON U17. Matumaini ya chipukizi hao yalizimwa hapo jana baada ya kudhalilishwa kwa mabao 3 bila jibu na majirani […]

PAMBANO LA GOR- BANDARI LAHAMISHWA

Mchuano wa ligi kuu ya soka KPL kati ya viongozi wa ligi hiyo Gor Mahia na Bandari FC utachezewa  katika uwanja wa michezo wa Kwale tarehe 12 mwezi huu, na wala si uwanja wa nyumbani wa Bandari wa Mbaraki. Kulingana na afisa mkuu mtendaji wa Bandari FC Tony Kibwana, hatua hiyo inalenga kuimarisha usalama wakati […]

WASHUKIWA 7 WA VURUGU KARIOBANGI WAKAMATWA

Idara ya polisi imethibitisha kuwakamata watu 7 wanaohusishwa na vurugu zilizoshuhudiwa katika kanisa moja mtaani Kariobangi North jijini Nairobi wakati wa ibada iliyokuwa ikihudhuriwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua. Kupitia taarifa, idara hiyo imesema washukiwa Charles Opiyo, Wilson Okoth, Michael Mutunga, Reggy Opiyo, Brian Omondi, Gordon Onyango na Elisha Ochieng wamekamatwa mtaani Lucky Summer. […]

WAKENYA HAWATAKI MAHAKAMA, WADAU

Wakenya asilimia 10 pekee ndio wanaosaka haki mahakamani huku asilimia 19 ya wakenya wakisusia huduma za mahakama, idara hiyo sasa ikitakiwa kubadilisha mifumo ili kuwahimiza wakenya zaidi kurejesha uaminifu kwa idara hiyo. Wakizungumza kwenye ufunguzi wa kongamano la majaji na mahakimu wa Afrika Mashariki jijini Nairobi, Naibu Rais Kithure Kindiki na jaji Mkuu Martha Koome, […]

MURKOMEN AFICHUA CHANGAMOTO ZA USALAMA

Baadhi ya maafisa wa polisi, viongozi serikalini na wanasiasa wanachangia pakubwa kuenea kwa magenge ya uhalifu nchini na hivyo kuwa changamoto kuu katika vita dhidi ya magenge hayo. Ni kauli ya Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen, kwenye mazungumzo na kituo kimoja cha runinga nchini ambako amesema kuwa wizara yake inafanya kila iwezalo kuyakabili […]

MAKABILIANO YA KISHERIA SENETI

Ubabe wa kisheria unatarajiwa hii leo katika bunge la seneti kwenye vikao vya kusikiliza na kuamua hoja ya kumbadua kutoka mamlakani gavana wa Nyamira Amos Nyaribo, mawakili wake wakikabiliana kisheria na wale wa bunge la kaunti hiyo. Kwenye vikao hivyo, Nyaribo atapambana kuzuia kuwa gavana wa pili kubanduliwa tangu uchaguzi wa mwaka 2022, akileta Pamoja […]

RUTO NJIANI KUELEKEA MAREKANI

Rais William Ruto yuko safarini kuelekea nchini Marekani ambako amealikwa na mwenzake Donald Trump kushuhudia kutiwa Saini mkataba wa makubaliano ya amani kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda. Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, makubaliano hayo yanajiri baada ya michakato ya amani ya Nairobi na Luanda, mbali na juhudi za Pamoja za […]

UPINZANI WADAI KUIBIWA CHAGUZI NDOGO

Viongozi wa upinzani nchini wameendelea kutofautiana na matokeo ya chaguzi ndogo zilizoandaliwa mwishoni mwa wiki jana, wakisema wagombeaji wao ndio walioshinda ila IEBC ikawatangaza wanaoegemea mrengo wa serikali. Wakiongozwa na Kalonzo Musyoka wa Wiper na Martha Karua wa PLP, viongozi hao wameshikilia kuwa uchaguzi huo haukuwa huru na haki, na kuwataka wakenya kuwa macho ili […]

NAFASI NYINGI MPYA ZA AJIRA NI ZA KSH50,000–KSH100,000 – KNBS

Kampuni na taasisi za umma zilianzisha kazi rasmi za ziada 206,617 kwa Wakenya wanaopata kati ya Ksh50,000 na Ksh100,000 kwa mwezi katika kipindi cha miaka mitano hadi 2024, na kufanya hii kuwa bendi ya malipo inayokuwa kwa kasi zaidi, kufuatia data kutoka Ofisi ya Kitaifa ya Takwimu ya Kenya (KNBS). Wafanyikazi katika kitengo hicho cha mishahara […]

CITY KUPUNGUZA MWANYA NA ARSENAL

Manchester City wana fursa ya kupunguza mwanya wa pointi kati yao na viongozi wa ligi kuu ya Uingereza EPL Arsenal, watasafiri Craven Cottage kupambana na Fulham leo usiku. City ambao walilazimika kusubiri hadi dakika za majeruhi kupata point izote 3 dhidi ya Leeds United, wana pointi 25, 5 nyuma ya Arsenal ambao wataialika Brentford hapo […]