MCF FC YAIBWAGA MOMBASA UNITED 3-0 KATIKA MECHI YA NSL

MCF FC iliifunga Mombasa United mabao 3-0 katika mechi ya Ligi ya Kitaifa Daraja la Pili (NSL) kwenye Uwanja wa Serani, Mombasa. Mabao ya MCF yalifungwa na James Olweny, John Okoth, na John Ochieng. Olweny alifunga bao la kwanza dakika ya 30 baada ya pasi safi kutoka kwa Ezekiel Okare. Okoth aliongeza la pili dakika […]

KAGWE AAHIDI KILIMO ‘SAFI’ KWA VIJANA

Wengi wa vijana nchini hawajihusishi na kilimo kutokana na mbinu zisizo na mvuto zinazotumika, nami nitahakikisha sekta hiyo inarekebishwa. Ndiyo kauli ya waziri mteule wa kilimo Mutahi Kagwe, akizungumza alipofika mbele ya kamati ya uteuzi katika bunge la kitaifa kueleza ufaafu wake wa kuhudumu kwenye wadhifa huo. Amesema kuwa iwapo ataidhinishwa, atashirikiana na wizara nyingine […]

MATOKEO NI YA WALIMU, SI WANAFUNZI- WAKAZI BUSIA

Wakazi wa Bumala kaunti ya Busia wamefanya maandamano kulalamikia matokeo duni yaliyorekodiwa na watahiniwa wa mtihani wa KCSE katika shule ya Bumala B, wakiulaumu usimamizi wa shule hiyo kwa matokeo hayo. Wakizungumza baada ya maandamano, wakazi hao wameshinikiza mageuzi katika usimamizi wa shule hiyo. Kwenye mtihani huo, shule hiyo ilipata alama ya wastani ya 3.23, […]

NAIROBI YAZIDI KUDHIBITI USAFI WA JIJI KWA MATATU NA WAFANYABIASHARA WADOGO

Serikali ya Kaunti ya Nairobi imetoa miongozo kwa wamiliki wa matatu kufuatia wasiwasi kuhusu shughuli zinazodaiwa kuzuia shughuli za usafi katikati ya jiji. Geoffrey Mosiria, Afisa Mkuu wa Mazingira wa Kaunti, katika taarifa ameeleza kwamba maeneo mengi ya matatu yanabaki yakikaliwa na magari usiku, yakizuia shughuli za usafi. Kama matokeo, alielekeza kwamba magari yote yaondoke […]

AFUENI YA NG-CDF KHWISERO

Ni afueni kwa wakazi wa eneo bunge la Khwisero kaunti ya Kakamega baada ya hazina ya ustawishaji wa eneo bunge hilo NG-CDF kutenga kima cha shilingi milioni 35 kugharamia karo ya wanafunzi wa shule za kutwa. Mbunge wa eneo hilo Christopher Aseka amesema kuwa tayari shilingi milioni 8 zimetengwa kufanikisha mpango huo kwa awamu ya […]

TUMEMSAMEHE MUUAJI, FAMILIA YA IAN

Tumemsamehe yeyote aliyehusika katika mauaji ya mtoto wetu, na hatutashinikiza kujua aliyehusika. Ndiyo kauli ya familia ya Ian Sing’oei ambaye mwili wake ulipatikana katika eneo la Mwiki jijini Nairobi Jumamosi iliyopita, familia hiyo ikizungumza wakati wa mazishi ya kijana huyo. Babake Ian, John Korir ambaye ni kamishna wa kaunti ya Elgeyo Marakwet na mamake ambaye […]

MASHARTI MAPYA KWA WALIMU WATARAJIWA

Tume ya kuwaajiri walimu TSC imetoa mapendekezo mapya kwa wanaolenga kusomea kozi za ualimu katika vyuo vikuu na taasisi za mafunzo ya ualimu, ikipendekeza kwamba anayetaka kufundisha katika shule za sekondari ya juu na sekondari msingi ni sharti awe na alama ya B+ na zaidi katika masomo mawili anayotaka kufunza. Kupitia taarifa, TSC imesema kwamba […]

EACC YAPATA MKUU MPYA

Wakenya wanatarajia huduma zilizoimarika kutoka kwa tume ya maadili na kupambana na ufisadi EACC baada ya Abdi Ahmed Mohamoud kuapishwa rasmi kuwa afisa mkuu mtendaji wa tume hiyo kuhudumu kwa miaka 6 na kujaza nafasi ya Twalib Mbaraka aliyestaafu. Mohamoud ameapishwa na jaji mkuu Martha Koome, akiahidi kuimarisha utendakazi wa tume hiyo na kupambana na […]

KINDIKI: SERIKALI KUZINDUA MAENEO YA BIASHARA KILA KAUNTI

Huenda shughuli za kibiashara na kilimo zikaimarika kote nchini iwapo serikali kuu itatimiza ahadi yake ya kuzindua kati ya maeneo 6-10 ya biashara na uzalishaji katika kaunti zote 47 kufikia mwisho wa mwaka huu. Akizungumza katika kikao na magavana 19 kutoka kaunti 19 ambazo zimeorodheshwa kwa ujenzi wa maeneo maalum`ya biashara katika awamu ya kwanza […]

WAUGUZI BUNGOMA WAANZA MGOMO, WAWATAKA WAGONJWA WAONDOKE

Baadhi ya wakazi katika kaunti ya Bungoma wametatizika kupata huduma za kimatibabu katika vituo vya umma kwenye kaunti hiyo kufuatia mgomo wa wauguzi wanaolalamikia madai ya kutotekelezwa kwa mkataba wao. Wakizungumza mjini Bungoma, wauguzi hao wamelalamikia mazingira duni ya kazi, wakishikilia kwamba hawatarejea kazini hadi malalamishi yao yatakapoangaziwa. Miongoni mwa matakwa yao ni ajira ya […]