KVF YATAFUTA KOCHA WA MALKIA STRIKERS

Shirikisho la Mpira wa Voliboli la Kenya (KVF) linatafuta kocha mkuu mpya wa timu ya taifa ya wanawake ya voliboli, Malkia Strikers, kuelekea Mashindano ya Dunia ya Wanawake ya FIVB 2025 yatakayofanyika kuanzia Agosti 22 hadi Septemba 7, mwaka huu nchini Thailand. KVF ilitangaza kuwa inakaribisha maombi kutoka kwa wale wanaopenda kushika nafasi ya kocha […]

KENYA POLICE YASHINDA MARA SUGAR NA KUREJEA KILELENI MWA LIGI KUU YA FKF

Kenya Police waliwalaza Mara Sugar bao moja pekee na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Shirikisho la Soka Kenya (FKF) katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Awendo jana Jumapili. Clinton Kinanga, ambaye yuko kwenye fomu bora, alifunga bao muhimu katika dakika ya 56 na kuwafanya maafisa wa polisi kurejea kileleni mwa ligi wakiwa na pointi 36, […]

AFUENI: MATABIBU WASITISHA MGOMO

Ni afueni kwa wanaosaka huduma za kimatibabu katika hospitali za umma baada ya maafisa wakliniki kusitisha mgomo wao kwa siku 21 ili kupisha mazungumzo kuhusu malalamishi yao. Katika taarifa kwa wanahabari, katibu mkuu wa muungano wa maafisa hao George Gibore hata hivyo, amesema mgomo huo utaendelea katika kaunti za Kwale, Vihiga, Uasin Gishu na Lamu. […]

RUTO AWAKEMEA WANAOPINGA SHA

Rais William Ruto amewataka wakenya kupuzilia mbali wanaopinga mpango wa afya wa SHA na badala yake akawataka wajisajili kwa wingi ili kupokea ambacho serikali imetaja kuwa matibabu bora. Akizungumza kwenye kaunti ya Busia akiwa kwenye ziara, Rais amesisitiza kwamba chini ya mpango huo, wakenya watapata matibabu kwa gharama ya chini. Aidha, ametaja pingamizi dhidi ya […]

IKULU: HAKUTAKUWA NA KUPOTEZA AJIRA

Msemaji wa Ikulu, Hussein Mohamed, amesema hakuna mfanyakazi atakayepoteza kazi kufuatia uamuzi wa Baraza la Mawaziri wa kuunganisha mashirika 42 ya kiserikali yenye majukumu yanayofanana kuwa mashirika 20. Mageuzi hayo, yaliyotangazwa baada ya mkutano ulioongozwa na Rais William Ruto Kakamega, pia yanajumuisha kuvunjwa kwa mashirika tisa na marekebisho ya mengine ili kupunguza matumizi ya umma. […]

POLISI UINGEREZA WACHUNGUZA MAUAJI YA MWANAMKE MKENYA ALIYEPATIKANA AMEUAWA LONDON

Polisi nchini Uingereza wanachunguza tukio la mwanamke mwenye asili ya Kenya aliyepatikana amepigwa hadi kufa katika nyumba yake eneo la Woolwich, Kusini Mashariki mwa London. Taarifa ya Polisi wa Mijini imesema mwili wa Marianne Kilonzi, mwenye umri wa miaka 43, umepatikana katika nyumba yake baada ya wasiwasi kuhusu usalama wake kuripotiwa. Kulingana na wasifu wake […]

MWANAMKE AZUILIWA JUJA KWA KUMCHOMA KISU MPENZI WAKE

Polisi huko Juja wanamzuilia Cynthia Nakato, mwenye umri wa miaka 20, kwa madai ya kumchoma kisu mara saba mpenzi wake Peter Macharia, 23, na kusababisha kifo chake katika eneo la Mastore, Juja, Januari 20, 2024. Mwili wa marehemu umepelekwa katika chumba cha maiti kwa uchunguzi wa baada ya kifo, huku polisi wakisema uchunguzi unaendelea. Kamanda […]

HUDUMA KENYA YATAKIWA KUPIGA JEKI MIRADI YA SERIKALI

Idara ya huduma Kenya imetakiwa kupiga jeki juhudi za serikali kuhakikisha kuwa wakenya Zaidi wanajisajili kwenye bima ya Taifa Care. Akizungumza kwenye kongamano la mameneja vituo vya Huduma Center jijini Mombasa, katibu katika wizara ya utumishi wa umma Amos Gathecha ameitaka idara hiyo pia kuorodhesha idadi ya wakenya waliosajiliwa kupitia huduma Kenya. Aidha, ametoa hakikisho […]

SIWALIPI, GAVANA LUSAKA KWA WANAKANDARASI

Wanakandarasi wanaojenga madarasa ya chekechea kwenye kaunti ya Bungoma wameonywa dhidi ya kufanya kazi duni kwenye ujenzi huo, hatua ambayo inahatarisha maisha ya wanafunzi. Akizungumza katika eneo bunge la Bumula, gavana wa Bungoma Ken Lusaka ameonya kuwa serikali yake italazimika kukosa kuwalipa wankandarasi wanaokosa kuafikia viwango hitajika vya ujenzi. Amezungumza wakati wa uzinduzi wa usambazaji […]

MGOMO: WAGONJWA WAILILIA SERIKALI

Wagonjwa katika hospitali za umma wameendelea kukosa huduma za matibabu kwa siku ya pili kutokana na mgomo wa maafisa wa kliniki, baadhi yao sasa wakiitaka serikali kuangazia malalamishi ya maafisa hao ili kuondoa mahangaiko hospitalini. Wakizungumza na wanabahari, baadhi ya wanaosaka matibabu wamesema kuwa migomo ya mara kwa mara miongoni mwa wahudumu wa afya imeathiri […]