AFCON 2025: NDIDI AKOSA NUSU FAINALI DHIDI YA MOROCCO

Timu ya taifa ya Nigeria, Super Eagles, itamkosa nahodha wao Wilfred Ndidi katika nusu fainali dhidi ya Morocco baada ya kiungo huyo kusimamishwa kwa mechi moja. Ndidi alipata kadi yake ya pili ya njano katika mashindano hayo wakati wa ushindi wa mabao 2–0 dhidi ya Algeria, jambo lililosababisha adhabu ya kusimamishwa moja kwa moja kwa mechi moja. Awali […]

REGRAGUI APINGA VIKALI MADAI YA UPENDELEO WA WAAMUZI KWA MOROCCO

Kocha wa timu ya taifa ya Morocco, Walid Regragui, amepinga kwa hasira madai kwamba timu yake inanufaika na maamuzi ya upendeleo kutoka kwa waamuzi kama wenyeji wa Kombe la Mataifa bingwa barani Afrika (AFCON) 2025. Atlas Lions wanatarajiwa kukutana na vigogo wenzao Nigeriakatika nusu fainali kali itakayochezwa Jumatano, Regragui akishikilia kuwa faida ya pekee walio nayo ni kucheza mbele ya mashabiki 65,000 […]

SSENYOJO AWAHAKIKISHIA CHUI WINDO LA KPL

AFC Leopards waliharibika na kuvunja vibuyu vya Tusker FC ugani Nyayo, kwa kuwatandika kichapo cha mabao 4-0 kwenye mechi ya ligi kuu KPL na kuongeza mwanya wa uongozi. Mganda Samuel Ssenyonjo aliwapa Ingwe uongozi wa mabao 2-0 kabla ya kutamatika kwa kipindi cha kwanza, Robert Sichenje akafunga la 3 na kisha Ssenyonjo akarejea kukamilisha hattrick […]

OWALO AJIUZULU

Naibu mkuu wa wafanyakazi wa Ikulu anayesimamia kitengo cha ufanikishaji wa utendakazi wa serikali ya Kenya Kwanza Eliud Owalo, amejiuzulu baada ya kutangaza azma yake ya kuwania urais kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka ujao. Kupitia taarifa, Owalo amesema haiwezekani kwake kuendelea kuitumikia serikali ya Rais William Ruto baada yake kutangaza kuwania wadhifa huo. Kulingana na […]

MATIANG’I ASHINIKIZA MAGEUZI YA ELIMU

Aliyekuwa Waziri wa usalama Fred Matiang’i, amehimiza haja ya vikao vya dharura kuandaliwa ili kujadili na kupata suluhu kwa changamoto zinazoikabili sekta ya elimu nchini. Akizungumza kwenye kaunti ya Kiambu, Matiang’i ambaye ni naibu kinara wa chama cha Jubilee, amesisitiza haja ya sekta hiyo kufanyiwa mageuzi ili kuilainisha. Aidha, amekosoa madai kwamba serikali imeingiza siasa […]

SIKU YA KIHISTORIA GRADE 10

Pilkapilka za kujiunga na gredi ya 10 katika shule za sekondari ya juu zimeshika kasi huku kundi hilo la kwanza likianza safari yao hii leo chini ya mtaala wa umilisi CBE. Wengi wa wazazi wamelalamikia muda mfupi waliopewa na wizara ya elimu kujiandaa, hatua ambayo imesababisha misongamano kwenye maduka ya kuuza bidhaa za shule. Wakati […]

GACHAGUA ASISITIZA KAULI ZAKE

Aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua amesisitiza haja ya kila eneo nchini kuimarisha miundomsingi yake ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi ikiwemo shule na kupunguza hulka za Watoto kulazimika kusomea shule za mbali. Akizungumza katika eneo la Gatundu kaunti ya Kiambu, Gachagua amekariri msimamo wake kwamba wanafunzi wanapaswa kupewa nafasi katika shule zilizo karibu na wanakotoka. […]

RUTO: NITAWATIMIZIA KABLA YA KUWAOMBA TENA

Rais William Ruto amewahakikishia wakazi wa Mlima Kenya kwamba atakamilisha ahadi zote alizotoa kwao kwenye kampeni za kuelekea uchaguzi mkuu uliopita kabla ya kuwaomba kura za muhula wa pili. Rais alikuwa akizungumza katika eneo bunge la Othaya akiwa kwenye ziara yake ya siku 3 katika eneo la Mlima Kenya, ambako amewataka wakazi kuwatathmini viongozi kutokana […]

TSC YASEMA TAYARI KWA GRADE 10

Tume ya kuwaajiri walimu TSC imewahakikishia wazazi na washikadau wa elimu kwamba taifa limejiandaa kikamilifu kwa mpito wa masomo ya gredi ya 10, ikisema walimu wamepewa mafunzo kikamilifu kushughulikia masomo hayo. Akizungumza jijini Eldoret wakati wa kutangazw kwa matokeo ya KCSE yam waka 2025, afisa mkuu mtendaji wa TSC Eveleen Mitei, amesema walimu wote wameandaliwa […]

KNEC: THIBITISHA USAJILI WA MWANAO

Baraza la mitihani ya kitaifa KNEC limewataka wazazi kuthibitisha kwamba wanao wamesajiliwa kwenye mitihani ya kitaifa ya gredi ya 6, 8 na kidato cha 4 kwa kutumia mfumo wa ujumbe mfupi wa maandishi SMS utakaotumika kuanzia Aprili mwaka huu. Afisa mkuu mtendaji wa KNEC David Njeng’ere, amesema hilo litapunguza changamoto za watahiniwa kukosa kukalia mitihani […]