MKUFUNZI WA TUSKER AKIRI HANA UWEZO KUIPIKU GOR KPL

Kocha mkuu wa klabu ya Tusker Julien Mette, amekiri kwamba timu hiyo haitashinda taji la ligi kuu ya kandanda nchini, KPL, msimu huu, akisema hamna nafasi za kuipiku viongozi Gor Mahia. Tusker mara ya mwisho walishinda taji hilo mwaka wa 2016, na licha ya kutarajiwa kutamatisha kiu cha mwongo mmoja, Mette amesema lengo lao msimu […]

STARS WAILAZA GRENADA KUMALIZA WA TATU FIFA SERIES

Timu ya taifa ya kandanda ya wanaume Harambee Stars ilitamatisha kinyang’anyiro chao cha FIFA Series nchini Rwanda kwa ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Grenada kutoka bara Ulaya, kwenye mechi iliyosakatwa katika uwanja wa Amahoro jijini Kigali. Kutokana na ushindi, Kenya ilimaliza ya tatu, nyuma ya Estonia waliolazwa mabao 2-0 na mabingwa Rwanda kwenye […]

WAATHIRIWA WA MAANDAMANO WATAKA MUDA ZAIDI

Huku zikiwa zimesalia siku 2 kabla ya kukamilika kwa muda waliopewa waathiriwa wa maandamano kuwasilisha stakabadhi hitajika ili kuzingatiwa kwa fidia, familia za waathiriwa hao zimeitaka tume ya kitaifa kuhusu haki za kibinadamu kuziongeza muda zaidi. Miongoni mwa malalamishi ya familia hizo ni ukosefu wa mawasiliano ya kutosha pamoja na njia mwafaka za kuifikia tume […]

IEBC YAWAHIMIZA VIJANA KUSAJILIWA

Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imesema inalenga kuwasajili wapiga kura wapya milioni 6.5 kabla ya uchaguzi mkuu ujao, tume hiyo ikihimiza ushirikiano miongoni mwa washikadau ili kuafikia lengo hilo. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa tume hiyo Erastus Ethekon, awamu ya kwanza ya zoezi la kitaifa lililoanza katika wadi zote hapo jana, inatarajiwa kukamilika […]

MAIGIZO YA POLISI NJE YA AFISI YA SAKAJA

Maswali yameibuka kuhusu ni kwanini maafisa wa polisi wakaamua kumsaka gavana wa Nairobi Johnson Sakaja afisini kwake jana usiku baada ya saa za kazi, licha ya kamati ya seneti kuhusu uhasibu kutaka gavana huyo awasilishwe mbele yake jana saa nne asubuhi. Katika kinachoonekana kama maigizo, makumi ya polisi wakiongozwa na msemaji wa polisi Muchiri Nyaga […]

UPINZANI: RUTO ANATAKA KUWATUMIA WAFU KUSHINDA

Viongozi wa muungano wa upinzani wameratibiwa kuendelea na ziara yao katika eneo la Ukambani hii leo, baada ya kuanza ziara hiyo hapo jana katika kaunti ya Makueni. Kwenye ziara hiyo, viongozi hao wameibua madai kwamba Rais William Ruto ana nia ya kujilazimishia ushindi kwenye uchaguzi mkuu ujao kwa kutumia kura za wakenya waliofariki ila maelezo […]

GACHAGUA AMWEKA DUALE MBIO KUHUSU SHA

Aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua ameendeleza madai yake kuhusu ufisadi katika bima ya afya ya jamii SHA, akisema waziri wa afya Aden Duale ni miongoni mwa wamiliki wa kampuni moja inayoshukiwa kutumika kwenye ufujaji wa shilingi bilioni 104 kwenye bima hiyo. Akizungumza kwenye ziara ya muungano wa upinzani eneo la Ukambani, Gachagua amesema kuwa kampuni […]

KATIBU MKUU WA CAF AJIUZULU

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka barani Afrika, Veron Mosengo-Omba, amejiuzulu katika kipindi chenye misukosuko kwa mchezo huo barani. Katika taarifa yake, Mosengo-Omba ametangaza kustaafu, huku uamuzi huo ukijiri wakati shirikisho hilo linakosolewa vikali kufuatia maamuzi tata, yakiwemo kuinyang’anya Senegal ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika 2025 na kuahirishwa kwa mashindano ya wanawake katika […]

KOCHA WA MURANG’A SEAL ATAKA WAITHIRA KUITWA TIMU YA TAIFA

Kocha wa Murang’a Seal, Osborne Monday, amemshawishi kocha wa timu ya taifa, Benni McCarthy, kuzingatia kumuita mshambuliaji bora wa ligi, Joe Waithira, katika kikosi cha taifa. Waithira, kinara wa mabao katika Ligi Kuu ya SportPesa akiwa na mabao 15, hakuorodheshwa katika kikosi kilichosafiri Rwanda kwa FIFA Series 2026, jambo lililosababisha mjadala miongoni mwa mashabiki na […]

ULINZI STARLETS WAKAZIA UBINGWA WA LIGI

Kocha wa Ulinzi Starlets, Collins Ochieng, amesisitiza kuwa timu yake ipo kwenye nafasi nzuri ya kushinda Ligi Kuu ya Wanawake ya FKF msimu huu. Ulinzi Starlets waliibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Trinity Starlets kwenye uwanja wa Comboni, Gilgil Jumapili, hatua iliyowainua hadi nafasi ya pili wakiwa na pointi 41, moja nyuma ya vinara […]