OSAMA AHAMIA KLABU YA SWEDEN

Winga chipukizi wa Kenya, Paul Osama, amepiga hatua kubwa katika taaluma yake ya soka baada ya kujiunga na klabu ya Enköpings nchini Sweden akitokea Murang’a Seal. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 alijiunga na Murang’a Seal mwanzoni mwa msimu wa 2025/2026 akitokea Mombasa United na kujidhihirisha haraka kama mchezaji muhimu, akifunga mabao matatu muhimu. […]

SIFUNA ABADILISHA WIMBO ASEMA HAWEZI KUWA ‘SG’ WA ODM

Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna sasa ameonekana kubadilisha maneno yake na kusema kuwa hawezi kuwa katibu mkuu wa chama hicho kwa sasa. Kauli ya Sifuna inakuja siku moja baada ya mahakama kutupilia mbali kesi yake ya kutolewa kama Katibu mkuu wa Chama hicho na kutaka suluhu la ndani ya chama. Sifuna sasa ameonekana kuwachilia nafasi […]

FAMILIA YALALAMIKIA URITHI WA NDERITU GACHAGUA

Familia ya aliyekuwa Gavana wa Nyeri, James Nderitu Gachagua, imewasilisha ombi kwa Rais William Ruto ikitaka uchunguzi huru kufanyika kuhusu madai ya njama za kuwanyima urithi wao. Kupitia barua iliyowasilishwa kwa Rais kupitia Mwanasheria Mkuu, familia hiyo inadai kuwa ndugu wa karibu aliingilia mchakato wa urithi kwa vitisho, hila na udanganyifu, hali iliyosababisha uhamishaji usio […]

BABU OWINO APINGA UONGOZI WA OBURU ODM

Mbunge wa Embakasi Mashariki, Babu Owino, amepinga wazi uteuzi wa Daktari Oburu Oginga kama kiongozi wa chama cha ODM akisema wanamtambua kama mzee wa heshima zake na si kiongozi wa chama. Akizungumza katika mkutano wa wajumbe wa kundi la Linda Mwananchi uliofanyika Ufungamano House mbunge huyo amehoji kasi ya uteuzi wa Oburu kufuatia kifo cha Raila Odinga, akidai wanachama […]

WINNIE ODINGA AHUDHURIA KONGAMANO LA LINDA GROUND

Mbunge wa EALA ambaye pia ni Mwanawe Hayati Raila Odinga amejiunga na mkutano maalum wa Wajumbe wa chama cha ODM huko Jamhuri Grounds wiki chache baada ya kuidhinishwa kama mwakilishi wa Chama cha ODM. Hatua hiyo imejiri licha ya kuwepo kwa mkutano sambamba wa kundi la Linda Mwananchi katika Ukumbi wa Ufungamano, kundi ambalo amekuwa […]

KWS YAKANUSHA UHARIBIFU WA MSITU NAIROBI

Shirika la Huduma za Wanyamapori limekanusha madai yanayosambaa mitandaoni kwamba linaharibu msitu wa nyanda za juu katika Hifadhi ya Taifa ya Nairobi. Shirika hilo limesema madai hayo yanapotosha, likieleza kuwa kazi inayoendelea ni sehemu ya mpango halali wa kuhamisha kituo cha kulea wanyama yatima cha Nairobi. Aidha, limesema hatua hiyo inalenga kuboresha uhifadhi wa wanyamapori, […]

OBURU OGINGA AIDHINISHWA KIONGOZI WA ODM

Chama cha ODM kimemuidhinisha rasmi Seneta wa Siaya, Daktari Oburu Oginga, kuwa kiongozi wa chama hicho kufuatia kifo cha kaka yake na aliyekuwa kiongozi wa muda mrefu Raila Odinga. Daktari Oburu, aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo baada ya kupendekezwa na baraza la juu la chama, amepitishwa rasmi katika mkutano maalum wa wajumbe uliofanyika katika uwanja wa Jamhuri. Katika […]

MSWADA WA FEDHA 2026 HAUNA USHURU MPYA, WAKENYA WAHAKIKISHIWA

Hazina ya Kitaifa imewahakikishia Wakenya na Bunge kwamba Mswada ujao wa Fedha wa 2026 hautaleta ushuru mpya au kuongeza viwango vya ushuru vilivyopo. Ahadi hiyo inalenga kupunguza wasiwasi wa umma na kukuza uthabiti wa kiuchumi kufuatia mizozo kuhusu ushuru katika miaka iliyopita. Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Hazina ya Kitaifa John Mbadi amefika mbele […]

FIFA WORLD CUP: ITALIA WAKARIBIA KUKATA KIU

Timu ya taifa ya kandanda ya Italia itachuana na Bosnia and Herzegovina kwenye fainali za mwondoano wa bara Ulaya kusaka tiketi ya kusakata dimba la kombe la dunia mwaka huu, baada ya kuandikisha ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Northern Ireland kwenye semi fainali za mchujo huo. Wakati uo huo, Wales na Jamhuri ya Ireland […]

UKAMILISHO WA TALANTA STADIUM WASUKUMWA MEI

Makataa ya kukamilishwa kwa ujenzi wa uwanja wa michezo wa Talanta Sports City imesongeshwa kutoka Machi hadi Mei, uwezekano mkubwa ukiwa kwamba huenda ujenzi huo ukakamilika Julai mwaka huu. Kuahirishwa huko kumejiri kufuatia ukaguzi wa kamati ya seneti kuhusu barabara, uchukuzi na miundombinu, inayosema imeridhishwa na hatua zilizopigwa hadi sasa. Aidha, lengo lao la ukaguzi […]