LEONARDO VARESE ALENGA NAFASI YA JUU SAFARI RALLY

Bingwa mara sita wa kitaifa wa magari ya daraja la Two-Wheel Drive (2WD), Leonardo Varese, analenga kumaliza katika nafasi tano bora kwenye uainishaji wa kitaifa katika mashindano ya Safari Rally Kenya, yatakayofanyika Naivasha kuanzia Machi 12 hadi 15. Akiwa anaongozwa na msomaji ramani wake wa muda mrefu, Kigondu Kareithi, wawili hao watachuana kwa kutumia gari […]

ALAI: TUPILIA MBALI AJENDA KUMI ZA UDA NA ODM

Mwakilishi wadi wa wadi ya Kileleshwa Robert Alai amesema kwamba ajenda kumi ambazo zipo kwenye makubaliano kati ya ODM na UDA haziwezi kutekelezwa. Kupitia ukurasa wake wa X Alai ametaka ajenda hizo kufutwa na kutupiliwa mbali akisema kuwa vifungu muhimu ndani ya mfumo huo haviwezi kutekelezwa kivitendo chini ya muundo wa sasa wa kikatiba. Imetayarishwa […]

WATU WAWILI WAFARIKI KWENYE AJALI ATHI RIVER

Watu wawili wamefariki dunia kufuatia ajali mbaya ya barabarani iliyo husisha malori mawili yaliyogongana kwa nguvu kabla ya kushika moto, hali iliyozua taharuki miongoni mwa watumiaji wa barabara hiyo katika eneo la mto mawe Athi River Kwa mujibu wa mashuhuda, malori hayo yameteketea kwa moto mkali mara tu baada ya kugongana huku mtu mmoja akijeruhiwa vibaya katika ajali hiyo na […]

SIFUNA: HAKUTAKUWA NA KUONGEZWA KWA MKATABA WA UDA NA ODM

Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna amekanusha uwezekano wowote wa kuongezwa kwa Mkataba wa Maelewano kati ya chama cha UDA na ODM baada ya tarehe ya mwisho ya Machi 7. Akizungumza katika mahojiano na kituo kimoja cha runinga humu nchini, Sifuna amesema makubaliano hayo yaliyotiwa saini Machi 7, 2025, hayakuwa na kipengele chochote cha kuongezwa muda, na yalipangwa kudumu […]

NTSA KUTUMIA KAMERA MAALUM KUDUMISHA SHERIA BARABARANI

Rais William Ruto ameiagiza Mamlaka ya Kitaifa ya Uchukuzi na Usalama (NTSA), pamoja na Wizara ya Uchukuzi, kutekeleza mifumo ya kutumia kamera maalum za trafiki kuwanasa wanaovunja sheria katika barabara mbalimbali nchini. Akihutubia Baraza la Kitaifa la Utawala wa Haki kwenye Ikulu ya Nairobi Ruto amemkabili Waziri wa Uchukuzi Davis Chirchir na Mkurugenzi Mkuu mpya wa NTSA […]

IDADI YA WATALII WA CHINA YAFIKIA 100,000 KENYA

Sekta ya utalii nchini imepigwa jeki baada ya taifa hili kushuhudia ongezeko kubwa la idadi ya watalii kutoka China wanaozuru ili kufurahia vivutio vyake vya kuvutia, vikiwemo wanyamapori na fukwe za mchanga. June Chepkemei, afisa mkuu mtendaji wa Bodi ya Utalii, amesema kwamba mawasiliano yaliyolengwa kwa wasafiri wa China yamezaa matunda, na kuleta uhai katika sekta ya ukarimu ya nchi […]

WATU 153 WAFARIKI SHULENI IRAN- RIPOTI

Watu wasiopungua 153 wakiwemo Watoto wameripotiwa kufariki katika shambulizi dhidi ya shule kusini mwa Iran, huku Iran ikilaumu Marekani na Israel kutokana na shambulizi hilo. Kupitia taarifa, Iran imethibitisha vifo hivyo, huku idara kuu ya kutoa amri kwa jeshi la Marekani, Centcom, ikisema inachunguza ripoti kuhusu shambulizi hilo, nalo jeshi la Israel likisema halina taarifa […]

RUTO AHIMIZA MAZUNGUMZO KUOKOA HALI UARABUNI

Rais William Ruto ameshutumu mashambulizi ya makombora yanayolenga ngome za kijeshi katika mataifa yaliyo mashariki ya kati huku vita vikichacha katika eneo hilo. Haya yanajiri baada ya Iran, katika kulipiza kisasi dhidi ya uvamizi wa Amerika na Israel, kulenga ngome hizo katika mataifa ya United Arab Emirates, Qatar, Saudi Arabia, Oman, Iraq, Jordan, Kuwait na […]

ARSENAL WAJIOKOA NA IKABU, UNITED NAFASI YA 3

Viongozi wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza, EPL, Arsenal, walirejesha mwanya wa pointi 5 kati yao na Manchester City baada ya kushinda pambano la mipira mifu dhidi ya Chelsea hapo jana.Katika ushindi wa mabao 2-1, mabao yote yalifungwa kutokana na mipira ya kona.Beki William Saliba aliwaweka Gunners kifua mbele katika dakika ya 21 kutokana […]

INGWE YAWARARUA GLAMOUR BOYS

Klabu ya AFC Leopards ilitangaza hatari kwa viongozi wa ligi kuu ya soka nchini, KPL, kufuatia ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Shabana FC ugani Nyayo hapo jana. Kwenye mechi iliyotarajiwa kuwa na ushindani, Ingwe walitoa kucha na kuwaparura Glamour Boys kuanzia dakika za ufunguzi za mchezo. Samuel Semo aliwaweka Ingwe mbele katika dakika ya […]