PAULINE SHEGHU AJIANDAA KWA KUJIAMINI SAFARI RALLY 2026

Dereva wa magari ya mashindano kutoka Kenya, Pauline Sheghu, ameonyesha kujiamini huku akiongeza maandalizi yake kuelekea mashindano ya Safari Rally Kenya ya mwaka 2026 yatakayofanyika Naivasha. Sheghu, anayejulikana kwa lakabu ya “Queen of the Dust”, akishirikiana na msomaji ramani wake Linet Ayuko, amesema gari lake limekidhi kikamilifu viwango vikali vya kiufundi vilivyowekwa na Shirikisho la Kimataifa […]

GOR MAHIA YAPATA PIGO BAADA YA JERAHA LA OLUOCH

Klabu ya Gor Mahia imepata pigo kubwa baada ya mshambuliaji wake nyota Felix Oluoch kutolewa nje kwa muda mrefu kufuatia upasuaji wa goti Oluoch, anayeongoza orodha ya wafungaji wa klabu hiyo kwa mabao saba, anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa angalau miezi mitatu, hali itakayomweka mbali na kikosi hadi msimu ujao. Daktari wa timu, Brian Odongo, amethibitisha […]

WALIMU BUNGOMA NA BUSIA WALALAMIKIA HUDUMA ZA SHA

Walimu katika kaunti ya Bungoma na Busia wamesema hawajaridhishwa na huduma za matibabu kupitia mamlaka ya afya ya jamii (SHA) wakisema ni kinyume na matarajio yao. Wakizungumza katika Kaunti ya Bungoma, Katibu Mkuu wa KUPPET tawi la Bungoma Augustine Luketelo amesema Bima hiyo haijatekeleza makubaliano yaliyoafikiwa na Serikali. Aidha Walimu hao wamesisitiza kuwa Iwapo SHA […]

VUGUVUGU LA UPINZANI PWANI LAMPIGIA DEBE KALONZO 2027

Vuguvugu linalounga mkono upinzani katika eneo la Pwani limemtaja kinara wa Wiper, Kalonzo Musyoka, kuwa mgombea anayefaa kupeperusha bendera ya urais katika uchaguzi mkuu ujao. Wakizungumza katika eneo la Tononoka, Mombasa, viongozi hao wamedai kuwa Rais William Ruto hajatekeleza ahadi alizotoa kwa wakazi wa Pwani, ikiwemo ajira kwa vijana, utatuzi wa migogoro ya ardhi na […]

RUTH ODINGA ATAKA LINDA GROUND NA LINDA MWANANCHI KUVUNJWA

Mwakilishi wa Wanawake wa Kaunti ya Kisumu, Ruth Odinga, ametoa wito wa kuvunjwa au kuunganishwa kwa makundi ya Linda Ground na Linda Mwananchi ndani ya chama cha ODM, akisisitiza umuhimu wa umoja wa chama hicho. Katika taarifa aliyochapisha kwenye mitandao yake ya kijamii Jumatatu, Odinga ambaye pia ni katibu wa maandalizi wa chama hicho, amesema […]

SERIKALI YAAGIZWA KUMLIPA CRITICOS 30M

Mahakama kuu imeiagiza serikali kumlipa fidia ya shilingi milioni 30 mbunge wa zamani wa Taita Taveta Basil Criticos baada ya kubaini kuwa haki za kikatiba kuhusu umiliki wa mali za kiongozi huyo zilikiukwa. Kwenye uamuzi wake, mahakama imesema kuwa Criticos alinyimwa haki haki zake za kikatiba kinyume na kipengee cha 40 cha katiba, kinachompa kila […]

JOHO AWE NAIBU WA RUTO, VIONGOZI WA PWANI

Viongozi wanaoegemea chama cha ODM kutoka ukanda wa pwani wamependekeza rais William Ruto kumteua Waziri wa madini Ali Hassan Joho kuwa mgombea mwenza wake kwenye uchaguzi mkuu ujao. Wakiongozwa na naibu kinara wa chama hicho na gavana wa Mombasa Alduswamad Nassir, viongozi hao wamesema kwamba Joho ana tajriba ya kutosha kuwa naibu rais. Imetayarishwa na […]

“GUMBOOTS” ZA MAUTI TONGAREN

Polisi katika eneo bunge la Tongaren kaunti ya Bungoma wanaendelea kumzuilia mwanamme mwenye umri wa miaka 21, anayedaiwa kumdunga kisu na kumwua nduguye mwenye umri wa miaka 24 katika Kijiji cha Shivakala-Lusoko. Kulingana na walioshuhudia, Davis Wanyonyi alimdunga kisu mara kadhaa nduguye Joshua Wafula kutokana na mzozo kuhusu viatu aina ya gumboots. Naibu chifu eneo […]

HAZINA YAPENDEKEZA SHERIA KALI KWA WAKOPESHAJI WA KIDIJITALI

Hazina ya Kitaifa inapanga kuwasilisha sheria mpya za utoaji leseni kwa watoa mikopo wasiochukua amana (NDTCPs) chini ya Sheria inayopendekezwa ya Sheria ya Biashara (Marekebisho) ya 2024. Katibu wa Hazina John Mbadi ameambia Seneti kwamba mfumo huo mpya unalenga kuimarisha usimamizi wa wakopeshaji wa kidijitali huku ukilegeza masharti kwa waendeshaji wadogo na wasio na hatari […]

BIDCO YAKAANGA ULINZI, SOFAPAKA MASAIBU TELE

Bingwa wa ligi kuu ya soka nchini, KPL, mwaka wa 2009 Sofapaka, wanajeshi wa Ulinzi Stars pamoja na limbukeni, maafande wa APS Bomet sasa wamejipata katika eneo la kushushwa daraja, timu hizo zikishikilia nafasi tatu za mwisho kwenye msimamo wa ligi. Timu 3 zitashushwa daraja mwishoni mwa msimu, bila kupitia njia ya mwondoano ama playoff. […]