KIZAAZAA CHA EPL, LIVERPOOL WAUMWA NA WOLVES

Ushindani mkali unatarajiwa leo usiku katika mechi za ligi kuu ya soka nchini Uingereza, EPL, jumla ya mechi 5 zitakaposakatwa. Darubini itaelekezwa kwenye pambano kati ya Arsenal ugenini dhidi ya Brighton, na Manchester City nyumbani dhidi ya Nottingham Forest. Arsenal wanaoongoza ligi wakiwa pointi 5 mbele ya City, watakuwa na fursa ya kufungua pengo la […]

KCB KUSAKA USHINDI MFULULIZO WA KWANZA MWAKA HUU

Timu ya KCB ina fursa ya kupata ushindi wa pili mfululizo kwa mara ya kwanza mwaka huu itakapochuana na Nairobi United ugani Ulinzi Complex leo alasiri. Wenyeji Naibois wanaingia mechi ya leo baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 ugenini dhidi ya Bandari FC, wakisalia katika nafasi ya 10 na pointi 29. Wakati uo huo, […]

ROONEY ONYANGO APATA AFUENI

Jopokazi la kushughulikia mizozo ya michezo, SDT, limemwondolea marufuku ya muda beki wa Harambee Stars Rooney Onyango, aliyokuwa amewekewa na shirika la kukabili matumizi ya dawa za kutitimua misuli nchini, ADAK. Beki huyo mwenye umri wa miaka 24 anayesakata soka ya kulipwa katika klabu ya Sogndal Fotball nchini Norway, alikuwa ametemwa tarehe 28 mwezi jana, […]

ASANTE KWA MAAFANDE

Awamu ya mwisho ya nyongeza ya mishahara ya maafisa wa polisi, wale wa magereza na maafisa wa idara ya huduma ya kitaifa ya vijana, NYS, itatekelezwa Julai mwaka huu ikiwa ni sehemu ya mpango wa kutekeleza mageuzi katika sekta ya usalama nchini. Kupitia taarifa, katibu katika wizara ya usalama wa kitaifa Raymond Omollo, amesema uamuzi […]

SERIKALI YA SALIA KIMYA KUHUSU UTATA WA PASIPOTI

Serikali kwa mara nyingine imejipata kwenye darubani ya wakenya kuhusiana na kimya chake kuhusu ripoti kwamba idara ya uhamiaji ilitoa pasipoti za usafiri kwa wapiganaji wa kundi la Rapid Suppport Forces, RSF, la Sudan, kundi ambalo limehusishwa na uhalifu nchini humo. Kimya cha serikali kimeendelea kwa takribani wiki moja baada ya ufichuzi huo, ripoti zikiashiria […]

BRIAN ODHIAMBO: MAAFISA WA KWS KUJITETEA

Familia ya mvuvi Brian Odhiambo, aliyetoweka mapema mwaka jana katika mbuga ya kitaifa ya Wanyama ya Lake Nakuru imeelezea kupata afueni baada ya mahakama ya Nakuru kuamuru kwamba maafisa wa KWS wanaohusishwa na kutoweka kwa mvuvi huyo, wana kesi ya kujibu. Kwenye uamuzi wake, hakimu wa mahakama hiyo Kipkurui Kibellion, amesema kuwa ushahidi uliowasilishwa unatosha […]

REJESHA EDUAFYA, SERIKALI YATAKIWA

Washikadau katika sekta ya elimu wameitaka serikali kurejesha mara moja mpango wa bima ya afya ya wanafunzi ya EduAfya, ili kudhibiti kile ambacho wametaja kama ongezeko la ghafla la vifo vinavyoweza kuzuiwa vya wanafunzi shuleni. Kulingana na shirika la Elimu Bora, ongezeko la hivi punde la mikasa kwenye shule mbali mbali nchini limeweka wazi udhaifu […]

KENYA KUPOKEA UFADHILI WA MIUNDOMBINU

Miundombinu ya kidijitali nchini inatarajiwa kuimarika kutokana na ufadhili wa shilingi bilioni 50 kutoka kwa benki ya dunia, ambao Kenya imeratibiwa kupokea katika kipindi cha miaka 3 ijayo kuboresha miundombinu hiyo. Fedha hizo zitatumika kwenye upanuzi wa kasi ya huduma za intaneti, lengo likiwa ni kuwavutia wawekezaji wapya katika sekta ya teknolojia. Tim Kelly ni […]

BUNGE LAFUTILIA MBALI VIKAO VYA LEO

Bunge limefutilia mbali vikao vyake vya leo ili kuwawezesha wabunge kuhudhuria ibada ya wafu kutoa heshima zao za mwisho kwa aliyekuwa mwenzao wa Emurua Dikirr Johana Ng’eno, aliyefariki Jumamosi na watu wengine watano kwenye ajali ya ndege. Kiongozi wa walio wengi bungeni Kimani Ichung’wa, aliweka wazi tangazo hilo wakati wa vikao vya jana, akisema hatua […]

ROSENIOR AONYA CHELSEA KUHUSU NIDHAMU

Kocha wa Chelsea FC, Liam Rosenior, amedai maboresho ya nidhamu kutoka kwa wachezaji wake baada ya Pedro Neto kuwa mchezaji wa tisa wa klabu hiyo kutolewa nje kwa kadi nyekundu msimu huu. Chelsea walipoteza 2-1 dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya Uingereza, Arsenal FC, katika Uwanja wa Emirates Jumapili, matokeo yanayomaanisha kuwa wameshinda mechi […]