FAMILIA KIBRA YATAKA HAKI BAADA YA MWANAMKE KUCHOMWA MOTO KIBRA

Familia moja katika eneo la Gatwikira huko kibra inataka haki baada ya ndugu yao kudaiwa kushambuliwa kutokana na msimamo wake wa kisiasa. Maureen Matsili ambaye ni mama wa watoto wanne, anadaiwa kushambuliwa na kuchomwa moto Mei 18 na mtu anayemfahamu kutokana na kuunga mkono kauli mbiu ya “Two Term” katika eneo hilo. Polisi wa Kibra wanaendelea kuchunguza […]

DUALE: SHERIA ZA KENYA LAZIMA ZIHESHIMIWE KATIKA USHIRIKIANO WA EBOLA

Waziri wa Afya Aden Duale amesema makubaliano yoyote kati ya Kenya na mataifa ya kigeni kuhusu kushughulikia watu walioathiriwa na virusi vya Ebola lazima yaheshimu sheria za Kenya pamoja na kanuni za afya ya umma. Kauli hiyo inajiri kufuatia ripoti kuwa Marekani inaweza kuzingatia kuwaleta nchini Kenya baadhi ya raia wake waliokaribiana na wagonjwa wa […]

WANAFUNZI KADHAA WAFARIKI KATIKA MOTO WA BWENI LA WASICHANA LA UTUMISHI

Moto mkubwa umezuka alfajiri katika shule ya wasichana ya Utumishi Academy eneo la Gilgil na kusababisha hofu ya vifo pamoja na majeruhi kadhaa baada ya bweni moja kuteketea kwa moto. Ripoti za awali zinaonyesha kuwa baadhi ya wanafunzi wanahofiwa kufariki huku wengine wakijeruhiwa na wengine kuathiriwa na moshi, hali ambayo imezua taharuki kubwa miongoni mwa wanafunzi, walimu […]

MUKHISA KITUYI ASEMA HAGOMBEI WADHIFA WOWOTE

Aliyekuwa Waziri wa Biashara Mukhisa Kituyi amesema hana mpango wa kugombea wadhifa wowote wa kisiasa licha ya baadhi ya watu kumshawishi kufanya hivyo. Kituyi amesema si kila kiongozi anapaswa kuelekeza nguvu katika kuwania urais, akisisitiza kuwa taifa pia linahitaji watu wenye uzoefu na ushawishi wa kusaidia kutoa ushauri kwa viongozi wengine. Ameongeza kuwa kuna haja […]

RAIS RUTO AHUDHURIA KIKAO CHA KITAIFA CHA MAOMBI

Rais William Ruto amewasili katika hoteli ya  Safari Park kuhudhuria hafla ya kikao cha Kitaifa cha Maombi kinachowaleta pamoja viongozi wa kisiasa, kidini na serikali Viongozi mbalimbali wa kitaifa, wanasiasa pamoja na maafisa wa serikali pia wamewasili katika hafla hiyo inayolenga kuombea taifa na kuhimiza mshikamano wa kitaifa Hafla hiyo ya kila mwaka huwakutanisha viongozi kutoka sekta tofauti nchini kwa maombi, […]

MAANDALIZI YA UCHAGUZI MDOGO OLKALAU YAENDELEA

Hatimaye tume ya uchaguzi nchini IEBC imewaidhinisha wagombea 9 wa kuwania kiti cha ubunge wa Olkalau baada ya kukamilisha shughuli ya uhakiki wa nyaraka zao. Miongoni mwa wagombea 9 walioidhinishwa ni  Rechael Wangoi Njoroge wa chama cha PDP, Sammy Kamau Ngodho wa DCP,Samuel Muchina wa UDA, Wilson Kigwa wa Jubilee Abdee Fata Husein ambaye ni […]

UKOSEFU WA MAJI SAFI WAZUA HOFU YA MAGONJWA VIHIGA

Walimu wazazi  na maafisa  wa afya  katika kaunti ya vihiga wanaiomba serikali ya kaunti hiyo kuangazia swala la ukosefu wa maji safi na vifaa bora vya  usafi wa mazingira swla ambalo limekuwa tishio katika shule nyingi eneo hilo ikiwemo shule ya musingi ya kuitukha . Viongozi hao sasa wanaonya kuhusu hatari ya kuongezeka kwa magonjwa […]

RAIA WA MAREKANI WALIOAMBUKIZWA EBOLA WATARAJIWA KUPATA MATIBABU NCHINI

Huku kenya ikiendelea kulinda mipaka zake dhidi ya kusambaa  kwa virusi vya Ebola Rais wa marekani Donald Trump anasema kwamba raia wa marekani walioambukizwa virusi  vya Ebola nchini Demokrasia ya Congo DRC  sasa wataletwa hapa nchini Kenya kwa uangalizi wa matibabu badala ya kurudishwa badala ya kurejeshwa huko marekani. Kulingana na gazeti rasmi la marekani […]

DCI YAMKAMATA  MUSHUKIWA WA MATAMSHI YA UCHOCHEZI MITANDAONI

 Maafisa wa upelelezi wa kesi za jinai DCI wamemkamata mshukiwa anaehusishwa na matamshi ya uchochezi yaliyokuwa yakisambaa mitandaoni. Katika taarifa DCI imesema Evans Onyango Kawala maarufu kama Kidero Jasuba amekamatwa katika eneo la Shujaa Mall mtaani Kayole jijini Nairobi. Kulingana na DCI mshukiwa huyo mwenye umri wa miaka 33 anaendelea kuzuiliwa akisubiri kufikishwa mahakamani hapo […]

COTU IMEITAKA SERIKALI KUONDOA USHURU KWA WAFANYAKAZI WA KIPATO CHA CHINI

Chama cha  Wafanyakazi nchini COTU limeitaka serikali kutoa afueni ya ushuru kwa wafanyakazi wa kipato cha chini na cha kati baada ya kutoridhishwa na Mswada wa Fedha wa mwaka 2026 uliowasilishwa bungeni. COTU inapendekeza wafanyakazi wanaopokea mshahara wa hadi shilingi elfu sitini kwa mwezi wapunguziwe kiwango cha ushuru wa  ili kuongeza kipato wanachobaki nacho kila mwezi. […]