RUTO KUHUTUBIA BUNGE LA TANZANIA

Rais William Ruto ameratibiwa kulihutubia bunge la kitaifa la Tanzania Jumanne wiki ijayo, ikiwa n ani sehemu za kuimarisha uhusiano baina ya mataifa hayo mawili. Kulingana na taarifa kutoka afisi ya spika wa bunge hilo, wabunge wamehamishwa kuhusu kikao hicho kitakachoanza saa tano asubuhi, akiwataka wabunge hao kufika bila kukosa ili kusikiliza hotuba ya rais […]

WAFANYAKAZI TRANS NZOIA WATISHIA MGOMO

Huku wafanyakazi nchini wakijiunga na wenzao kote ulimwenguni kuadhimisha siku ya kimataifa ya wafanyakazi, Leba Dei, mmungano wa wafanyakazi wa umma katika kaunti ya Trans Nzoia umetishia kushiriki mgomo na kusambaratisha shughuli zote za utoaji huduma ikiwa wanachama wake hawatalipwa mshahara wa miezi miwili. Mwenyekiti wa wafanyakazi hao Lennox Opicho na mwenzake wa muungano wa […]

ASTON VILLA WAONJESHWA KICHAPO EUROPA

Bao la Chris Wood liliipa Nottingham Forest uongozi muhimu katika mechi ya mkondo wa kwanza wa semi fainali ya kombe la UROPA dhidi ya Aston Villa jana usiku. Wood alifunga bao hilo kupitia mkwaju wa penalti kunako dakika ya 71 baada ya Lucas Digne kuunawa mpira kwenye eneo la hatari, bao hilo likimaanisha vijana wa […]

UHASAMA WANUKIA DIAMOND LEAGUE

Bingwa wa dunia katika mbio za wanawake za mita 3,000 Faith Cherotich ameratibiwa kufufua uhasama wake dhidi ya mkenya mwenzake anayekimbilia taifa la Bahrain Winfred Mutile Yavi watakapokutana na mbio ya kuruka viunzi na maji kwenye mashindano ya pili ya Diamond League jijini Xiamen baadaye mwezi hu. Wawili hao watakutana kwa mara ya 12 katika […]

AFUENI YA SHA KWA WAFANYAKAZI

Ni afueni kwa maelfu ya walimu walio chini ya muungano wa KUPPET baada ya bima ya afya SHA kuwawekea kiwango cha malipo ya hospitali kutoka shilingi 1,200 hadi shilingi 10,000 kila mara wanapozuru hospitali kutibiwa. Kulingana na Waziri wa afya Aden Duale, hatua hiyo ni sehemu ya mpango wa kutatua changamoto walizokuwa wakikumbana nazo wanaposaka […]

 IEBC YAWEKA WAZI IDADI YA SAJILI WAPYA

Wakenya ambao hawakusajiliwa katika zoezi endelevu la usajili wa wapiga kura wapya lililokamilika mapema wiki hii wametakiwa kufanya hivyo katika afisi za tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC katika maeneo bunge. Hii nii baada ya zoezi hilo kukamilika huku tume hiyo ikisema jumla ya wapiga kura wapya 2, 612,725 tangu usajili wa kitaifa ulipozinduliwa. […]

 SERIKALI YAJICHANGANYA NA MAFUTA

Maswali yameibuka kuhusu uamuzi wa serikali kutangaza kwamba itaagiza mafuta ya viwango vya chini kwa muda wa miezi 6 ijayo hadi Oktoba mwaka huu, ikizingatiwa kuwa maafisa 3 katika sekta ya kawi walikamatwa na kulazimika kujiuzulu baada ya kuagiza mafuta yasiyokidhi viwango hapa nchini. Kupitia taarifa, waziri wa biashara na viwanda Lee Kinyanjui, amesema uamuzi […]

MAFURIKO YATATIZA UCHUKUZI NCHINI

Shughuli za usafiri katika maeneo mbali mbali ya nchi ikiwemo jijini Nairobi zimeendelea kutatizika kutokana na mvua kubwa ambayo imesababisha barabara kufurika maji, mbali na na nyumba kadhaa kufurika. Miongoni mwa barabara hizo ni ile ya Mombasa Road ambako sehemu kadhaa kama vile Belle Vue na GM zimefurika maji na kusababisha msongamano kwenye barabara hiyo […]

MATARAJIO YA WAFANYAKAZI LEBA DEI

Huku Kenya ikijiunga na ulimwengu kuadhimisha siku ya wafanyakazi, Leba dei, wafanyakazi nchini wanatarajia tangazo la nyongeza ya mishahara kwa asilimia 23 kutokana na ongezeko la gharama ya maisha. Katibu mkuu wa muungano wa vyama vya wafanyakazi, COTU, Francis Atwoli, amesema kuwa maafisa wakuu serikalini, wawakilishi wa mashirika na vyama mbali mbali wanatarajiwa kuhudhuria sherehe […]

  • 1
  • 2