WAKULIMA WA MAUA NCHINI WATAFUTA ONDOLEO LA USHURU HUKU KUKIWA NA HASARA YA SH200 MILIONI KILA SIKU

Sekta ya maua nchini Kenya imeshinikiza kupunguziwa kodi na hatua za haraka za usaidizi wa serikali, ikionya kwamba kupanda kwa ushuru chini ya Mswada wa Fedha wa 2026 unaopendekezwa kunaweza kuzidisha shinikizo kwa wakulima ambao tayari wanapambana na usumbufu wa usafirishaji unaohusishwa na mzozo wa Mashariki ya Kati. Kulingana na Baraza la Maua nchini, sekta hiyo inapoteza wastani […]

SWEDEN WATEGEMEA ISAK NA GYOKERES KATIKA KOMBE LA DUNIA

Timu ya taifa ya Sweden inatarajia safu yao ya ushambuliaji ikiongozwa na Alexander Isak na Viktor Gyokeres kuwasaidia kufanya vyema katika Kundi F la Kombe la Dunia mwaka huu. Timu hiyo chini ya kocha Graham Potter itachuana na Uholanzi, Japan pamoja na Tunisia nchini Marekani, Canada na Mexico. Sweden walifika fainali hizo kwa njia ngumu baada ya […]

ANN ALUOCH ASIFIA MAFANIKIO YA MATHARE UNITED WOMEN

Kocha wa Timu ya wanawake ya  Mathare United Ann Aluoch amesema mwanzo mzuri wa msimu, juhudi za wachezaji pamoja na usaidizi wa uongozi wa klabu vilichangia mafanikio ya timu hiyo katika Ligi ya Taifa ya Daraja la Kwanza kwa wanawake. Mathare United walitwaa ubingwa wa Kanda A na kufuzu kushiriki ligi kuu baada ya kucheza mechi 21 […]

KENYA YAIMARISHA AZMA YA KUANDAA MASHINDANO YA RIADHA DUNIANI

Kenya imeongeza juhudi za kuwania kuandaa Mashindano ya Dunia ya Riadha ya mwaka 2029 au 2031 baada ya Katibu Mkuu wa Michezo Elijah Mwangi kukutana na ujumbe wa shirrikisho la Riadha Duniani jijini Nairobi. Ujumbe huo ulioongozwa na Antti Pihlakoski ambaye ni mwenyekiti wa jopo la tathmini ya zabuni ulifanya mazungumzo na maafisa wa michezo nchini kuhusu […]

MWANAUME MACHKOS ATAKA HAKI BAADA YA KUCHOMWA NDEVU

Mwanaume mmoja mjini Machakos anayefahamika kama John Kyalo anataka haki baada ya kuvamiwa na kuchomwa ndevu alipokuwa amepumzika katika eneo moja mjini humo. Kyalo amesema mtu anayedai kumfahamu aliwasha moto kwenye ndevu zake ambazo amekuwa akizitunza kwa miaka mingi. Tukio hilo sasa limezua mjadala huku akiitaka sheria kuchukua mkondo wake dhidi ya mhusika. Imetayarishwa na Cyrus […]

UHABA WA MALAZI WAIBUKA WAJIR KABLA YA MADARAKA DEI

Mji wa Wajir unakabiliwa na uhaba mkubwa wa malazi kuelekea sherehe za kitaifa za Madaraka Day zitakazoongozwa na Rais William Ruto Jumatatu ijayo. Maelfu ya wageni kutoka maeneo mbalimbali nchini wanatarajiwa kuhudhuria hafla hiyo wakiwemo viongozi wa kitaifa, maafisa wa usalama pamoja na wanamuziki. Hoteli na nyumba nyingi za wageni mjini humo zimeripotiwa kujaa mapema […]

WANDAYI AHAKIKISHIA NCHI KUHUSU UPATIKANAJI WA MAFUTA

Waziri wa Nishati Opiyo Wandayi amesema Kenya ina akiba ya kutosha ya mafuta licha ya ripoti za uhaba katika baadhi ya maeneo ya ukanda huu kutokana na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati. Wandayi ambaye alikagua vituo vya mafuta katika kaunti za Nairobi na Machakos amesema serikali imejitolea kuhakikisha usambazaji wa mafuta haukatizwi. Aidha amewataka wananchi […]

BUNGE LAJADILI NJIA ZA KUPUNGUZA GHARAMA YA MAFUTA

Kizaazaa kimeshuhudiwa Bungeni wakati wabunge waliingia katika mjadala mkali kuhusu hatua za kupunguza gharama ya mafuta nchini. Hoja hiyo iliyowasilishwa na Mbunge wa Ndia George Kariuki ilifichua mgawanyiko mkubwa kuhusu mapendekezo ya kupunguza ushuru wa mafuta. Wakati huo huo, pendekezo la Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro la kupunguza matumizi katika taasisi za serikali lilipingwa vikali na […]

KNCCI NA COTU WAPINGA BAADHI YA MAPENDEKEZO YA MSWADA WA FEDHA

Chama cha Kitaifa cha Biashara na Viwanda Kenya kimeonya kuwa sera ya ushuru iliyopendekezwa katika Mswada wa Fedha 2026 inaweza kudhoofisha ushindani wa uchumi wa Kenya. Chama hicho kimesema ushuru mpya unaweza kuongeza gharama za biashara na kuathiri uwezo wa kampuni kushindana katika soko la ndani na la kimataifa. Kwa upande wake, Shirikisho la Vyama […]

NJERI MAINA ATAKA HATUA ZA DHARURA DHIDI YA MAUAJI YA WANAWAKE

Mwakilishi wa Wanawake wa Kaunti ya Kirinyaga Njeri Maina ametaka kuwepo kwa hatua za haraka na za pamoja kitaifa kukabiliana na ongezeko la mauaji ya wanawake na watoto wanaopotea nchini. Katika taarifa yake, Maina amesema visa vinavyoongezeka vya wanawake kuuawa na watoto kutoweka vinaonyesha kuwa taifa linakabiliwa na janga kubwa linalohitaji ushirikiano wa taasisi zote […]