UTAFITI WA KNUT WAFICHUA WALIMU WANAKABILIWA NA MADENI

Utafiti mpya wa Muungano wa KNUT umefichua kuwa walimu wengi nchini wanakabiliwa na matatizo makubwa ya kifedha, msongo wa mawazo na uchovu wa kazi. Ripoti ya ustawi na ushiriki wa walimu imeonyesha kuwa asilimia 97 ya walimu wanaishi kutegemea mshahara wa mwezi bila kuwa na akiba yoyote mwishoni mwa mwezi. Aidha, asilimia 92 ya walimu walioshiriki katika […]

KINDIKI ASEMA UCHAGUZI 2027 UTAAMULIWA NA MAENDELEO

Naibu Rais Kithure Kindiki ametetea rekodi ya maendeleo ya serikali akisema uchaguzi mkuu ujao utaamuliwa na utendakazi pamoja na utoaji huduma badala ya siasa za maneno. Akizungumza katika eneo Bunge la Msambweni, Kindiki amesema serikali ya Kenya Kwanza inalenga kubadilisha maisha ya wananchi kupitia miundombinu, umeme, masoko na uchumi wa baharini. Amesisitiza kuwa Rais William Ruto […]

MBAYA KIMWELE AJENGA MABWAWA YA MAJI KWA WAFUGAJI KITUI

Kitui imetajwa kuongoza nchini katika ufugaji wa mbuzi aina ya Gala kulingana na Waziri wa kilimo wa kaunti hiyo Mbaya Kimwele. Wizara hiyo inaendelea kuchimba mabwawa ya maji katika maeneo yanyojulikana kwenye  ufugaji ili kuimarisha shughuli hiyo katika maeneo kame. Akizungumza alipokuwa akizindua ujenzi wa bwawa la Kasiatu huko Treikuru Mwingi Kaskazini Mbaya amesema mabwawa […]

LUSAKA AONYA WAFANYAKAZI HEWA KAUNTI YA  BUNGOMA

Gavana wa Bungoma Ken Lusaka ameagiza bodi ya uwajiri katika kaunti hiyo kuangazia kwa kina swala la wafanyakazi hewa kuripotiwa katika utumishi wake akisema kuna wafanyakazi zaidi ya 1000 ambao hawakuidhinishwa kisheria. Lusaka ameagiza uchunguzi kufanywa kuhusu jinsi wafanyakazi hao walivyoajiriwa akisema bodi hiyo inafaa kukaguliwa upya. Imetayarishwa na Hilda Ajema

WAKENYA WAONYWA KUHUSU MVUA KUBWA INAYOTARAJIWA

Idara ya utabiri wa hali ya anga imetangaza kuwa baadhi ya maeneo yatapata mvua kubwa kuanzia leo Mei 26 hadi tarehe moja Juni mwaka huu. Katika taarifa idara hiyo imesema maeneo yatakayo pata mvu hiyo ni pamoja na Nairobi, Nyeri, Murang’a, Kiambu,  kaunti ya Kakamega, Bungoma, Nandi, Uasin Gishu na Trans Nzoia, kaunti nyingine ni […]

MUSALIA AONYA WAKENYA KUHUSU EBOLA

Waziri mkuu Musalia Mudavadi amewataka wakenya kufuata maagizo yanayotolewa na wizara ya Afya kufuatia mulipuko wa ugonjwa wa Ebola ulioripotiwa katika mataifa jirani ya Uganda na Demokrasia ya Congo DRC. Akizungumza katika kaunti ya Morang’a Mudavadi amesema japo kenya haijaripoti kisa chochote cha Ebola uzembe unaweza kuhatarisha taifa hivyo wananch wanapaswa  kujitahadhari katika muingiliano wa […]

KEPSA YAONYA KUHUSU VIPENGELE KATIKA MSWADA WA FEDHA WA 2026

Muungano wa Sekta ya Kibinafsi ya Kenya (KEPSA) umepinga baadhi ya vipengele vya Mswada wa Fedha wa 2026, ukionya kwamba baadhi ya hatua zinazopendekezwa za ushuru zinaweza kukandamiza biashara, kudhoofisha ushindani wa Kenya na kupunguza kasi ya kuunda kazi. Ukiwakilishwa mbele ya Kamati ya Kitaifa ya Idara ya Fedha na Mipango ya Kitaifa, viongozi wa KEPSA wameambia Bunge […]

CHELSEA WALAUMIWA KWA UTOVU WA NIDHAMU

Kocha wa muda wa Chelsea Calum McFarlane amesema utovu wa nidhamu ulikuwa sababu kubwa iliyosababisha timu hiyo kukosa nafasi ya kushiriki mashindano ya Ulaya msimu ujao. Chelsea walimaliza katika nafasi ya 10 kwenye Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kufungwa mabao 2-1 na Sunderland Katika mechi ambayo, beki wa Ufaransa Wesley Fofana alitolewa nje kwa kadi nyekundu, ikiwa ni […]

MANCHESTER UNITED WANAPANGA KUMBAKISHA BRUNO FERNANDES

Manchester United wameanza mazungumzo ya kumbakisha nahodha wao Bruno Fernandes licha ya kuwepo kwa kipengele cha kuvunja mkataba wake chenye thamani ya pauni milioni 57. Ripoti zinaeleza kuwa mazungumzo ya awali tayari yamefanyika huku klabu hiyo ikiwa tayari kumzawadi kiungo huyo kwa mkataba bora zaidi. Bruno pia anaripotiwa kuvutiwa na vilabu vya Ulaya pamoja na […]

VIPIMA UBORA WA HEWA VYAWEKWA KABLA YA MBIO ZA NAIROBI CITY MARATHON

Vipima ubora vya hewa vinne vimewekwa katika maeneo muhimu kando ya Barabara ya Nairobi Expressway kuelekea mashindano ya Nairobi City Marathon yatakayofanyika Juni 7. Mashindano hayo yataanza City Hall Way na kumalizikia Uhuru Park huku sehemu kubwa ya mbio ikifanyika kwenye barabara hiyo. Mtafiti wa masuala ya ubora wa hewa kutoka Taasisi ya Mazingira ya Stockholm Ngongang Wandji amesema vifaa hivyo […]