USIKU MUHIMU KWA KLABU ZA UEFA

Mechi ya 7 kati ya 8 ya awamu ya kwanza ya ligi ya klabu bingwa barani Ulaya, UEFA, zitachezwa usiku wa leo ambapo timu kadhaa ikiwemo Liverpool, Real Madrid na Inter Milan zitalenga kupata ushindi ili kujihakikishia kufuzu moja kwa moja katika awamu ya 16 bora kutokana na kudidimia kwa matumaini ya kupata mataji ya […]

CITY WANAYE GUEHI

Hatimaye Manchester City imemsajili beki wa kati Marc Guehi kwa kima cha pauni milioni 20 kutoka Crystal Palace kwa mktaba wa miaka 5 unusu katika juhudi za kuimarisha safu yao ya ulinzi. City waliimarisha juhudi za kumsaka beki huyo Mwingereza kutokana na masaibu ya majeraha kwa mabeki wao wa kati tegemeo Ruben Diaz, John Stones […]

AFCON 2025: MOROCCO YAWASILISHA MALALAMISHI KWA CAF, FIFA

Shirikisho la soka nchini Morocco limetangaza kuwasilisha rasmi kwa shirikisho la soka barani Afrika, CAF, na shirikisho la soka Ulimwenguni, FIFA, malalamishi yake kuhusu matukio yaliyowahusisha mashabiki na wachezaji wa timu ya taifa ya Senegal kuondoka uwanjani kupinga penalti dhidi yao kwenye fainali za AFCON 2025. Matukio hayo yalisababisha mechi hiyo kusimamishwa kwa takribani dakika […]

BINGWA POLICE FC AZIDI KUJIKWAA

Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka, KPL, Police FC, waliendeleza msururu wa mechi 3 bila ushindi na kichapo cha mechi 7 msimu huu kutokana na sare ya bao 1-1 dhidi ya Nairobi United ugani Police Sacco hapo jana. Mabao yote yalifungwa na Police FC, Jacques Ndecke akijifunga kunako dakika za 69 kabla ya Yves […]

MGAWANYIKO ODM: KINARA ALAUMIWA

Baadhi ya viongozi wanaoegemea chama cha ODM wamemkosoa kinara wao Oburu Oginga kuhusiana na misukosuko inayokumba chama hicho, wakidai Oginga ameonyesha miegemeo. Miongoni mwao ni naibu kinara hicho na seneta wa Vihiga Godfrey Otsotsi, akisema Oginga na kiongozi wa walio wachache bungeni Junet Mohammed wamepuuza wosia wa mjane wa kinara mwanzilishi wa ODM Raila Odinga- […]

AMISI ADAI RUTO ALINUNUA ODM

Mbunge wa Saboti kaunti ya Trans Nzoia, Caleb Amisi, amehusisha masaibu ya chama cha ODM na mwingilio kutoka nje ya chama, akiibua madai kwamba Rais William Ruto amekinunua chama hicho huku wanachama chipukizi wakikabiliwa na vitisho vya kufurushwa. Akizungumza wakati wa zoezi la kuwapokeza wanafunzi hundi za basari katika eneo la Matisi, Amisi amesema waliolengwa ni pamoja na mwanawe kinara […]

RUTO: MSIWAPOTOSHE VIJANA

Rais William Ruto amewataka viongozi wa upinzani kukomesha alichokitaja kama kuwapotosha vijana wanaosaka njia za kujiwezesha kimaisha, kutokana na ukosoaji wa viongozi hao dhidi ya mpango unoafadhiliwa na serikali wa NYOTA. Ruto alikuwa akizungumza kwenye hafla ya kutoa mtaji huo kwa vijana wa kaunti za Kiambu, Nairobi na Kajiado, akipinga dhana kwamba mradi huo unatumiwa […]

POLISI WAHIMIZA MADEREVA KUMAKINIKA BARABARANI

Madereva wamehimizwa kuchukua tahadhari wanapokaribia maeneo ya Gilgil na Kikopey kwenye barabara kuu ya Nairobi- Nakuru kufuatia visa vya ajali ambapo watu 7 wameaga dunia huku wengine 11 wakijeruhiwa kwenye ajali iliyohusisha magari kadhaa. Kamanda wa polisi eneo la Gilgil Winson Mwakio, amethibitisha ajali hiyo na kuwataka madereva kuwa makini ili kudhibiti visa vya ajali. […]

WANAHARAKATI BUSIA WASHINIKIZA HAKI KWA MWANAMME

Mwanamme mwenye umri wa miaka 25 mjini Busia anaendelea kuuguza majeraha hospitalini baada ya kudaiwa kumwagiwa maji ya moto na mkewe, huku familia ikiikosoa mahakama kwa madai ya kuharakisha kumwachia kwa dhamana mshukiwa. Kulingana na Ishmael Oundo, tukio hilo lilisababishwa na ugomvi kati yake na mkewe, wakazi na wanaharakati wakishinikiza mshukiwa akamatwe upya. Imetayarishwa na […]

REGRAGUI AKOSOA VIKALI FUJO KATIKA FAINALI YA AFCON

Kocha wa Morocco, Walid Regragui, amekosoa vikali tukio alilolitaja kuwa la “aibu” lililotokea katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, baada ya wachezaji wa Senegal kuondoka uwanjani kwa kupinga uamuzi wa waamuzi kabla ya kurejea na kushinda mchezo huo katika muda wa nyongeza. Akizungumza baada ya Morocco kupoteza fainali hiyo 1-0 jijini Rabat, Regragui […]