GUEYE ASEMA SENEGAL ILITUMIA HASIRA KUSHINDA AFCON

Mfungaji wa bao la ushindi katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, Pape Gueye, amesema Senegal ilichochewa na hali ya kutotendewa haki baada ya Morocco kupewa penalti ya utata iliyokaribia kuwagharimu taji hilo. Mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa Prince Moulay Abdellah mjini Rabat ulikuwa bado bila bao hadi dakika za mwisho za muda […]

AKONNOR AIPONGEZA GOR MAHIA BAADA YA KUICHAPA MARA SUGAR

Kocha mkuu wa Gor Mahia Charles Akonnor amewapongeza wachezaji wake kufuatia ushindi wa mabao 3–0 dhidi ya Mara Sugar katika mechi ya Ligi Kuu ya FKF iliyochezwa Jumapili Januari 18, 2026, katika uwanja wa Nyayo National Stadium. Akizungumza baada ya mechi hiyo, Akonnor alisema alifurahishwa na utulivu na maamuzi sahihi ya wachezaji wake uwanjani, akibainisha […]

HATUA YA MAKUNDI YA KVF KENYA CUP YAFIKIA TAMATI

Hatua ya makundi ya mashindano ya KVF Kenya Cup msimu wa 2025/2026, toleo la pili, ilifikia tamati Jumapili Januari 18, 2026, katika uwanja wa mpira wa kikapu wa Nyayo Stadium. Mashindano hayo yalishuhudia ushindani mkali huku timu za National Police Service zikijitokeza kwa kiwango cha juu. Timu ya KAPU, iliyokuwa pekee kuiwakilisha NPS siku ya […]

RAIS FAYE ATANGAZA HOLIDEI SENEGAL KUSHEREHEKEA AFCON

Rais wa Senegal Bassirou Diomaye Faye, ametangaza siku ya mapumziko nchini humo hii leo ili kuwapisha wananchi kusherehekea ubingwa wa dimba la taifa bingwa barani Afrika, AFCON, walilotwaa hapo jana nchini Morocco. Katika tangazo, rais Faye amesema holidei hiyo inalenga kuwawezesha raia kushiriki sherehe za alichokitaja kama fahari kuu ya taifa. Kupitia runinga ya kitaifa […]

KESI YA SALASYA- NCIC YAAHIRISHWA

Mahakama kuu jijini Nairobi imeahirisha kupitishwa kwa makubaliano ya suluhu katika kesi inayomhusisha mbunge wa Mumias East Peter Salasya na tume ya kitaifa ya uwiano na utangamano NCIC ambako Salasya anatuhumiwa kutoa matamshi ya chuki. Hii ni baada ya mahakama kufahamishwa kwamba baadhi ya vigezo vya makubaliano hayo havijaafikiwa, ambako mbunge huyo anafaa kupewa wajibu […]

UKAME WAATHIRI WANYAMAPORI LAMU

Shirika la Huduma kwa Wanyamapori nchini (KWS) limezidisha hamasa kwa jamii zinazoishi vijijini Lamu kuepusha migogoro na wanyamapori huku ukame ukiendelea kukithiri eneo hilo na sehemu zingine nchini. Mkurugenzi wa KWS Kaunti ya Lamu Ibrahim Ahmed, amesema shirika hilo pia limeweka mikakati ili kuhakikisha wanyamapori wanasambaziwa maji porini endapo kiangazi kitaendelea, ili kuwazuia kuingia vijijini. Vile vile amewashauri […]

CARRICK AHIMIZA UDHABITI UNITED

Meneja mshikilizi wa klabu ya Manchester United Michael Carrick, amewataka wachezaji wake kuonyesha viwango sawa walivyoonyesha kwenye ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya majirani zao Manchester City Jumamosi, mechi ambayo iliashiria mwanzo mpya Old Trafford. United walichochewa na mabadiliko katika uongozi, mabao ya Brian Mbeumo na Patrick Dorgu yakitia breki kwa juhudi za City kunyakua […]

MMUST RUGBY WAPATA USHINDI ADIMU

Kikosi cha Masinde Muliro University Rugby kiliandikisha ushindi wake wa kwanza wa msimu wa Kenya Cup baada ya kuwatandika Impala Saracens 20-15 katika pambano la kusisimua lililoandaliwa chuoni humo. Kabla ya Pambano hilo, Impala walikuwa wamewanyuga Daystar Falcons 50-17, ila wakapata mshtuko mikononi mwa MMUST Rugby. Akizungumza baada ya mechi hiyo, kocha mkuu wa MMUST […]

GOR MAHIA WAONYESHA WANGALI MAWINDONI

Mabingwa wa kihistoria wa ligi kuu ya soka nchini, KPL, Gor Mahia, waliweka wazi kwamba wangali katika uwindaji wa taji hilo msimu huu, kufuatia ushindi wao wa mabao 3-0 dhidi ya Mara Sugar na kuwabandua mahasimu wao wa karibu AFC Leopards kutoka uongozi wa ligi hiyo. K’Ogalo walitamalaki mchezo mwanzoni na kutangaza hatari katika dakika […]

SENEGAL BINGWA AFRIKA

Bao la kiungo wa Villareal Pape Gueye katika muda wa ziada liliwahakikishia Simba wa Taranga Senegal ubingwa mara 2 katika kipute cha AFCON, kutokana na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Atlas Lions wa Morocco kwenye fainali za dimba hilo. Kwenye mechi iliyojaa shinikizo, mihemko na vitimbi, wachezaji wote wa Senegal waliondoka uwanjani katika dakika […]