MOROCCO NA SENEGAL KATIKA FAINALI YA AFCON

Wenyeji Morocco na Senegal wamefuzu fainali ya kombe la mataifa ya afrika baada ya ushindi wa jasho katika mechi za nusu fainali zilizochezwa jumatano. Morocco walitinga fainali baada ya kuibuka na ushindi wa mikwaju ya penalti dhidi ya Nigeria kufuatia sare ya bila kufungana katika nusu fainali iliyochezwa Rabat. Fainali hiyo inawakutanisha mataifa mawili yanayoongoza […]

WAITHIRA NA AMBANI WATWAA TUZO ZA FKF DECEMBER

Nahodha wa Murang’a seal Joe Waithira ametangazwa mchezaji bora wa ligi kuu ya FKF kwa mwezi wa desemba 2025 baada ya kiwango bora wakati wa sikukuu. Waithira aliwashinda Ovella Ochieng’, Tyson Otieno, Paul Okoth, Jimmy Owili na Bixente Lizarazu, baada ya kufunga mabao manne katika mechi tatu, akiisaidia Murang’a seal kukusanya pointi saba kati ya […]

HARAMBEE STARLETS KWA KUNDI GUMU WAFCON 2026

Harambee Starlets wamepangwa katika kundi a lenye ushindani mkali kwenye kombe la mataifa ya afrika kwa wanawake 2026 litakalofanyika Morocco kuanzia machi 17 hadi aprili 2. Kwa mujibu wa droo iliyofanyika alhamisi katika kituo cha soka cha Mohammed vi mjini Rabat, Kenya itakutana na wenyeji Morocco, Senegal na algeria. Mashindano ya mwaka 2026 yataandika historia […]

KeNHA YATANGAZA KUFUNGWA KWA BARABARA KUU YA UHURU

Mamlaka ya barabara kuu ya kitaifa nchini KENHA imetangaza kufungwa kwa muda kwa sehemu muhimu za barabara kando ya barabara kuu ya uhuru katika mzunguko wa haile selassie avenue ili kurahisisha kazi muhimu za barabara. Katika taarifa ya umma, KENHA imetangaza awamu ya i ya kufungwa kwa huduma wakati wa saa za usiku zisizo  nne usiku hadi saa kumi na […]

UMEME KUKATIKA KAUNTI YA NYERI

Kampuni ya kusambaza umeme nchini  imetangaza kukatika kwa umeme hii leo katika sehemu tofauti za kaunti ya Nyeri kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni. Baadhi ya maeneo yatakayo athirika ni  gachatha, wamagana, na kariguini. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WANAFUNZI WA GREDI YA 10 KUONGEZEWA MUDA

Wizara ya elimu inataka kuongeza muda kwa wanafunzi wanaojiunga na gredi ya 10 ikisisitiza kuwa itafikia asilimia 100 ya mpito. Hili linajiri baada ya takriban wanafunzi 400,000 pekee kati ya wanafunzi milioni 1.1 waliowekwa kuripoti shuleni. Ingawa shule za kitaifa zimerekodi zaidi ya asilimia 90 ya wanafunzi waliojitokeza, mamia ya maelfu ya wanafunzi bado wamesalia  nyumbani huku wazazi wakikabiliana na gharama huku wasiwasi kuhusu uhaba wa vifaa ukiongezeka. […]

Temi esclusivi di slot nei migliori casino non AAMS: guida estiva con cashback live

Temi esclusivi di slot nei migliori casino non AAMS: guida estiva con cashback live L’estate è il momento ideale per provare slot dal design unico e dalle promozioni più calde. Se vuoi risparmiare tempo nella ricerca, casino non aams sicuri ti offre un confronto pronto all’uso, così da scegliere subito il sito più adatto alle […]

ARBELOA AANZA KWA MASAIBU REAL

Miamba wa soka nchini Uhispania Real Madrid walibanduliwa nje ya kipute cha Copa del Rey na klabu ya Albacete inayoshiriki divisheni ya pili katika mechi ya kwanza ya kocha mkuu Alvaro Arbeloa aliyechukua nafasi ya Xabi Alonso. Beki huyo wa zamani wa Liverpool na Real Madrid aliwapumzisha Kyllian Mbappe, Thibaut Courtois, Jude Bellingaham na Rodrygo […]

CHELSEA WAADHIBIWA KWA MAKOSA YAO- ROSENIOR

Meneja wa Chelsea Liam Rosenior amekiri kwamba kikosi chake kiliadhibiwa kutokana na makosa yao yaliwapa Arsenal uongozi wa mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya dimba la Carabao Cup jana usiku baada ya kupokezwa kichapo cha mabao 3-2 nyumbani. The Blues wana mlima wa kukwea katika mkondo wa pili watakazuru Fly Emirates tarehe 3 mwezi […]

AFCON: SADIO AWEKEA SENEGAL MIADI YA MOROCCO

Bao la pekee la mashambulizi wa zamani wa Liverpool Sadio Mane katika dakika ya 78 liliwahakikishia Senegal fainali yao ya pili ya taifa bingwa barani Afrika AFCON tangu mwaka 2021, lililowapa ushindi mwembamba ila muhimu wa bao 1-0 dhidi ya bingwa wa kihistoria Misri yake Mohammed Salah. Mabingwa hao wa mwaka 2021 walitamalaki mchezo dhidi […]