HUZUNI GILGIL BAADA YA MOTO WA SHULE, DNA KUFANYWA

Maumivu na simanzi vilitawala katika shule ya Utumishi Girls Academy eneo la Gilgil huku wazazi na walezi wakihangaika kutafuta taarifa za watoto wao kufuatia moto uliosababisha vifo vya wanafunzi 16 na kujeruhi wengine 79. Msemaji wa Serikali Isaac Mwaura amesema mwanapatholojia wa serikali Johansen Oduor tayari amewasili eneo hilo kuanza uchunguzi wa vinasaba vya DNA […]

RUTO AZINDUA MPANGO WA KUPUNGUZA VIFO VYA KINA MAMA NA WATOTO WACHANGA

Rais William Ruto amezindua rasmi mpango wa kitaifa wa EWENE wa miaka 2026 hadi 2028 unaolenga kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto wachanga nchini. Mpango huo unalenga kuboresha huduma za afya, kuimarisha uwajibikaji pamoja na kutekeleza afua maalum katika kaunti zinazorekodi visa vingi vya vifo vya kina mama na watoto wachanga. Serikali pia imeanzisha mpango […]

RUTO: WALIO NA MISHAHARA YA CHINI YA SH30,000 WASILIPISHWE KODI

Rais William Ruto ametangaza kuwa serikali itapeleka bungeni pendekezo la kuwaondoa wafanyakazi wanaopata mshahara wa hadi shilingi elfu 30 katika ulipaji wa kodi ya mapato. Akizungumza katika kikao cha Kitaifa cha Maombi jijini Nairobi, Ruto amesema hatua hiyo inalenga kupunguza ugumu wa maisha kwa wananchi wa kipato cha chini licha ya serikali kukabiliwa na upungufu wa mapato […]

BUNGE LAHOJI BAJETI YA 2026/27

Wanachama wa Kamati ya Bajeti na Matumizi ya Fedha wameibua wasiwasi kuhusu upungufu wa mapato, uwajibikaji katika sekta ya afya pamoja na shinikizo la kifedha wakati wa kupitia bajeti ya mwaka wa fedha 2026/27. Waziri wa Hazina ya Kitaifa John Mbadi ametetea bajeti ya shilingi trilioni 4.785 yenye nakisi ya shilingi trilioni 1.111 itakayofadhiliwa hasa […]

MASWALI YAIBUKA KUHUSU MOTO WA SHULE YA UTUMISHI

Maswali yanaendelea kuibuka kuhusu chanzo cha moto ulioteketeza bweni katika shule ya Utumishi Girls Academy iliyoko Kaunti ya Nakuru huku Wakenya wengi wakieleza hofu kuhusu usalama wa wanafunzi katika mabweni ya shule. Taarifa mpya zinaashiria kuwa huenda moto huo uliosababisha vifo vya wanafunzi 16 na kujeruhi wengine 79 uliwashwa kimakusudi, jambo ambalo limeongeza wasiwasi miongoni […]

WATAALAMU WA EBOLA WA AMERIKA WAWASILI KENYA

Wataalamu wa magonjwa ya kuambukiza kutoka Amerika wamewasili nchini Kenya na kuanza maandalizi ya kituo maalum cha Ebola ambacho Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani Marco Rubio amesema kitaanza kufanya kazi ndani ya siku saba zijazo. Ikulu ya White House imethibitisha kuwa Amerika inaandaa kituo maalum nchini Kenya kwa ajili ya kuwatenga raia wa […]

DCP YAMTAKA WAZIRI WA ELIMU KUJIUZULU

Chama cha DCP kinataka uchunguzi wa kina kufanyika kutokana kuhusiana na chanzo cha moto katika shule ya Upili ya wasichana ya  Utumishi. Akizungumza katika makao makuu ya chama hicho Katibu mkuu John Metho ametaka wizara ya usalama kutoa taarifa ya kina kuhusiana na waraka wa serikali kukabiliana na majanga. Imetayarishwa na Hilda Ajema

GAVANA KIHIKA AAHIDI KUSAIDIA FAMILIA ZA WAATHIRIWA WA MOTO GILGIL

Huko Nakuru gavana Susan Kihika amesema serikali yake itashirikiana kikamilifu na serikali ya kitaifa katika kuzisaidia familia zilizoathirika na mkasa wa moto. Kauli yake imesisitizwa na Waziri   Murkomen akisema serikali inalenga kuwasaidia wazazi na wanafunzi na huduma za ushauri nasaha wakati huu ambapo zinaendelea kukumbwa na wakati mugumu. Imetayarishwa na Hilda Ajema

WAZIRI OGAMBA AZUNGUMZA KATIKA ENEO LA MKASA  WA MOTO HUKO GILGIL

Waziri wa elimu Julius Ogamba amesema kati ya wanafunzi 808 ambao walikua  katika shule ya  wasichana ya Utumishi huko Nakuru  wakati wa mkasa wa moto wanafunzi 79 wamejeruhiwa, huku 71 wakihudumiwa na kuruhusiwa kuondoka hospitalini, saba wakiendelea kupokea matibabu. Akizungumza katika shule ya wasichana ya Utumishi Ogamba ametuma rambi rambi zake kwa familia na marafiki […]

NTSA KUZINDUA MFUMO WA KIDIJITALI WA KUTATUA MAKOSA BARABARANI

NTSA imesema itaanzisha mfumo wa kisasa wa utekelezaji wa makosa madogo ya barabarani kuanzia Juni 2026, katika hatua ambayo itawaruhusu madereva kupewa Arifa ya Polisi ya Uhalifu wa Trafiki ili  kuepuka kufika mahakamani.  Katika taarifa, Mamlaka ya Kitaifa ya Uchukuzi na Usalama pamoja na Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma ODPP, Mahakama na mashirika mengine ya […]