GACHAGUA APIGA ABAUTANI KWENYE KESI YA KUTIMULIWA

Aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua sasa amefutilia mbali ombi lake la kutaka arejeshwe afisini jinsi alivyokuwa amewasilisha kesi inayoendelea kwa sasa katika mahakama ya Milimani, na badala yake anataka kupewa fidia. Wakati wa vikao vinavyosikilizwa na majaji Anthony Mrima, Freda Mugambi na Erick Ogolla, mawakili wa Gachagua wameiarifu mahakama kwamba kesi hiyo iliyofanyiwa marekebisho sasa […]

BEI YA TANI YA MIWA YASHUKA

Bodi ya Sukari ya nchini imetangaza marekebisho ya kushuka kwa bei ya miwa, na kupunguza kiwango hicho kutoka Ksh5,750 hadi Ksh5,500 kwa tani. Katika notisiambayo imetolewa , kufuatia mikutano ya Kamati ya Muda ya Kupanga Bei ya Miwa iliyofanyika Aprili 17 na Aprili 24, mwaka huu bodi imethibitisha kwamba bei mpya ya chini ya Ksh5,500 kwa tani itaanza kutumika mara moja. […]

MAN CITY, CHELSEA FAINALI ZA FA

Manchester City ilijikatia tiketi ya kushiriki fainali za dimba la FA, ikiwa ni mara ya kwanza katika historia kwa klabu yoyote kucheza kwenye fainali za FA mara 4 mfululizo. Mabao ya Jeremy Doku na Nico Gonzalez yaliiwezesha City kutoka nyuma na kupata ushindi wa mabao 2-1 kwenye semi fainali dhidi ya Southampton ugani Wembley. City […]

K’OGALO WAKAMATA USUKANI WA KPL

Bingwa wa kihistoria wa ligi kuu ya soka nchini, KPL, Gor Mahia, waliongeza pengo la pointi kileleni mwa jedwali la ligi hiyo na kushika usukani, kufuatia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wapinzani wao AFC Leopards katika debi la mashemeji. Baada ya ukame wa mabao kwa pande zote licha ya K’Ogalo kutamalaki mchezo, bao Alpha […]

SAWE AVUNJA REKODI YA MARATHON

Mkenya Sebastian Sawe amekuwa binadamu wa kwanza kuwahi kukamilisha mbio za marathon chini ya muda wa saa mbili, baada ya kuibuka bingwa wa mbio za London Marathon katika muda wa 1:59:30. Kwa upande wa wanawake, Tigst Assefa wa Ethiopia alitetea taji lake la mbio za London Marathon, na kuvunja rekodi yake ya awali. Hata hivyo, […]

RUTO AMTETEA KINDIKI DHIDI YA UKOSOAJI

Rais William Ruto amemtetea naibu wake Kithure Kindiki dhidi ya wakosoaji, akimtaja kama kiongozi mnyeneyekevu huku akiwapuzilia mbali viongozi anaosema wanamdhalilisha Kindiki. Rais alikuwa akizungumza katika kaunti ya Tharaka Nithi baada ya kuwakabidhi wafanyabiashara soko jipya mjini Chuka, akiipigia upato sekta za kilimo, afya na elimu. Amewataka wakenya kuwapiga msasa viongozi kwa misingi ya utendakazi. […]

ORENGO AJITANGAZA KINARA WA ODM

Utata wa uongozi umeendelea kujitokeza ndani ya chama cha ODM, gavana wa Siaya James Orengo akijitangaza kuwa kaimu kinara wa chama hicho, wadhifa unaoshikiliwa na seneta wa kaunti hiyo Oburu Oginga. Wakizungumza jijini Kisumu wakati wa mkutano wa Linda Mwananchi ulioongozwa na katibu mkuu Edwin Sifuna, viongozi wa mrengo huo wameikosoa serikali kwa kukosa kutekeleza […]

HOFU YATANDA TSEIKURU BAADA YA UVAMIZI

Maafisa wa usalama wameanzisha msako dhidi ya washukiwa wa uvamizi uliotekelezwa katika kijiji cha Kwa Kamari kaunti ya Kitui Jumamosi, na kusababisha vifo vya watu 7, serikali ikisema uvamizi huo ni sehemu ya mashambulizi ya kulipiza kisasi kati ya jamii za wafugaji na wakulima eneo la Tseikuru. Wakazi ambao wameingiwa na hofu, wamesema wavamizi wanaoshukiwa […]

UDA MATATANI KWA ‘KUKWEPA’ KULIPA KODI

Tume ya kutetea haki za kibinadamu, KHCR imetishia kukishtaki mahakamani chama tawala cha UDA kutokana na madai ya kukwepa kulipa kodi na madai ya kuhusika katika matumizi mengine mabaya ya fedha za umma. Ikinukuu ripoti ya mkaguzi wa hesabu za serikali, KHCR imesema kupitia taarifa kwa vyombo vya habari kwamba ripoti hiyo inafichua uvunjaji wa […]

MAHAKAMA KUANZA VIKAO VYA KESI YA GACHAGUA

Vikao vya siku 3 vya kusikiliza kesi ambapo aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua anapinga kutimuliwa kwake kutoka afisini vinaanza hii leo mbele ya jopo la majaji 3, Gachagua akisema ana imani kwamba atapata haki. Wakati uo huo, viongozi wa muungano wa upinzani wamelitaka jopo hilo la mahakama kuu kuangazia kwa makini sababu za kutimuliwa kwake, […]