UHABA WA MALAZI WAIBUKA WAJIR KABLA YA MADARAKA DEI

Mji wa Wajir unakabiliwa na uhaba mkubwa wa malazi kuelekea sherehe za kitaifa za Madaraka Day zitakazoongozwa na Rais William Ruto Jumatatu ijayo. Maelfu ya wageni kutoka maeneo mbalimbali nchini wanatarajiwa kuhudhuria hafla hiyo wakiwemo viongozi wa kitaifa, maafisa wa usalama pamoja na wanamuziki. Hoteli na nyumba nyingi za wageni mjini humo zimeripotiwa kujaa mapema […]

WANDAYI AHAKIKISHIA NCHI KUHUSU UPATIKANAJI WA MAFUTA

Waziri wa Nishati Opiyo Wandayi amesema Kenya ina akiba ya kutosha ya mafuta licha ya ripoti za uhaba katika baadhi ya maeneo ya ukanda huu kutokana na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati. Wandayi ambaye alikagua vituo vya mafuta katika kaunti za Nairobi na Machakos amesema serikali imejitolea kuhakikisha usambazaji wa mafuta haukatizwi. Aidha amewataka wananchi […]

BUNGE LAJADILI NJIA ZA KUPUNGUZA GHARAMA YA MAFUTA

Kizaazaa kimeshuhudiwa Bungeni wakati wabunge waliingia katika mjadala mkali kuhusu hatua za kupunguza gharama ya mafuta nchini. Hoja hiyo iliyowasilishwa na Mbunge wa Ndia George Kariuki ilifichua mgawanyiko mkubwa kuhusu mapendekezo ya kupunguza ushuru wa mafuta. Wakati huo huo, pendekezo la Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro la kupunguza matumizi katika taasisi za serikali lilipingwa vikali na […]

KNCCI NA COTU WAPINGA BAADHI YA MAPENDEKEZO YA MSWADA WA FEDHA

Chama cha Kitaifa cha Biashara na Viwanda Kenya kimeonya kuwa sera ya ushuru iliyopendekezwa katika Mswada wa Fedha 2026 inaweza kudhoofisha ushindani wa uchumi wa Kenya. Chama hicho kimesema ushuru mpya unaweza kuongeza gharama za biashara na kuathiri uwezo wa kampuni kushindana katika soko la ndani na la kimataifa. Kwa upande wake, Shirikisho la Vyama […]

NJERI MAINA ATAKA HATUA ZA DHARURA DHIDI YA MAUAJI YA WANAWAKE

Mwakilishi wa Wanawake wa Kaunti ya Kirinyaga Njeri Maina ametaka kuwepo kwa hatua za haraka na za pamoja kitaifa kukabiliana na ongezeko la mauaji ya wanawake na watoto wanaopotea nchini. Katika taarifa yake, Maina amesema visa vinavyoongezeka vya wanawake kuuawa na watoto kutoweka vinaonyesha kuwa taifa linakabiliwa na janga kubwa linalohitaji ushirikiano wa taasisi zote […]

UTAFITI WA KNUT WAFICHUA WALIMU WANAKABILIWA NA MADENI

Utafiti mpya wa Muungano wa KNUT umefichua kuwa walimu wengi nchini wanakabiliwa na matatizo makubwa ya kifedha, msongo wa mawazo na uchovu wa kazi. Ripoti ya ustawi na ushiriki wa walimu imeonyesha kuwa asilimia 97 ya walimu wanaishi kutegemea mshahara wa mwezi bila kuwa na akiba yoyote mwishoni mwa mwezi. Aidha, asilimia 92 ya walimu walioshiriki katika […]

KINDIKI ASEMA UCHAGUZI 2027 UTAAMULIWA NA MAENDELEO

Naibu Rais Kithure Kindiki ametetea rekodi ya maendeleo ya serikali akisema uchaguzi mkuu ujao utaamuliwa na utendakazi pamoja na utoaji huduma badala ya siasa za maneno. Akizungumza katika eneo Bunge la Msambweni, Kindiki amesema serikali ya Kenya Kwanza inalenga kubadilisha maisha ya wananchi kupitia miundombinu, umeme, masoko na uchumi wa baharini. Amesisitiza kuwa Rais William Ruto […]

MBAYA KIMWELE AJENGA MABWAWA YA MAJI KWA WAFUGAJI KITUI

Kitui imetajwa kuongoza nchini katika ufugaji wa mbuzi aina ya Gala kulingana na Waziri wa kilimo wa kaunti hiyo Mbaya Kimwele. Wizara hiyo inaendelea kuchimba mabwawa ya maji katika maeneo yanyojulikana kwenye  ufugaji ili kuimarisha shughuli hiyo katika maeneo kame. Akizungumza alipokuwa akizindua ujenzi wa bwawa la Kasiatu huko Treikuru Mwingi Kaskazini Mbaya amesema mabwawa […]

LUSAKA AONYA WAFANYAKAZI HEWA KAUNTI YA  BUNGOMA

Gavana wa Bungoma Ken Lusaka ameagiza bodi ya uwajiri katika kaunti hiyo kuangazia kwa kina swala la wafanyakazi hewa kuripotiwa katika utumishi wake akisema kuna wafanyakazi zaidi ya 1000 ambao hawakuidhinishwa kisheria. Lusaka ameagiza uchunguzi kufanywa kuhusu jinsi wafanyakazi hao walivyoajiriwa akisema bodi hiyo inafaa kukaguliwa upya. Imetayarishwa na Hilda Ajema

WAKENYA WAONYWA KUHUSU MVUA KUBWA INAYOTARAJIWA

Idara ya utabiri wa hali ya anga imetangaza kuwa baadhi ya maeneo yatapata mvua kubwa kuanzia leo Mei 26 hadi tarehe moja Juni mwaka huu. Katika taarifa idara hiyo imesema maeneo yatakayo pata mvu hiyo ni pamoja na Nairobi, Nyeri, Murang’a, Kiambu,  kaunti ya Kakamega, Bungoma, Nandi, Uasin Gishu na Trans Nzoia, kaunti nyingine ni […]