HAKIMI NJE DHIDI YA BAYERN

Bingwa mtetezi wa dimba la klabu bingwa barani Ulaya, PSG, itakosa huduma za beki wake Achraf Hakimi katika mechi ya marudiano ya semi fainali ya dimba hilo dhidi ya Bayern kutokana na jeraha la paja. Kupitia taarifa, PSG imesema raia huyo wa Morocco atakuwa nje kwa kile ilichotaja kama wiki chache kutokana na jeraha hilo. […]

MIKWAJU YA PENLATI YAOKOLEA ARSENAL, ATLETICO

Julian Alvarez aliirejesha Atletico Madrid mchezoni kupitia mkwaju wa penalti katika mechi ya mkondo wa kwanza ya awamu ya semi fainali za dimba la klabu bingwa bara Ulaya jana usiku dhidi ya Arsenal na kuishia sare ya bao 1. Viktor Gyokeres aliwaweka viongozi wa EPL kifua mbele kunako dakika ya 44 vile vile kupitia mkwaju […]

KCB YAJIIMARISHA KABLA YA FAINALI KENYA CUP

Klabu ya raga ya KCB RFC imeimarisha maandalizi yake kwa fainali ya dimba la Kenya Cup dhidi ya Kabras RFC litakalochezwa tarehe 9 mwezi ujao mjini Kakamega. Kocha mkuu wa klabu hiyo Andrew Amonde amesema kuwa wanabenki hao wanalenga kurekebisha makosa yaliyosababisha kupoteza kwao katika fainali zilizopita dhidi ya Kabras mwaka wa 2023 na 2024. […]

MZOZO MWINGI: WASAFIRI WAKWAMA 

Shughuli za uchukuzi zimeendelea kutatizika kwenye barabara kuu ya Mwingi kuelekea Garissa kutokana na hali tete ya usalama iliyochochewa na kuuawa kwa watu wanane mwishoni mwa wiki jana kwenye uvamizi. Mzozo huo unaohusisha jamii mbili kutoka kaunti jirani, umesababisha kufungwa kwa barabara hiyo huku wasafiri wakikwama katika vituo vya mabasi ya usafiri. Tayari muungano wa […]

WIZARA YAONYA DHIDI YA DHULUMA ZA NGONO

Wizara ya elimu imeibua hofu kuhusu visa vya unyanyasaji wa kingono katika vyuo vya kiufundi, TVET, ikionya kuwachukulia hatua walimu wa taasisi hizo wanaojihusisha na visa hivyo. Akizungumza katika kaunti ya Mombasa, Waziri wa elimu Julius Ogamba, amekiri kuwa wizara yake imepokea ripoti kuhusu unyanyasaji huo anaokariri kuwa unakiuka sheria za mafunzo nchini. Kauli yake […]

JAJI WARSAME NDIYE CHAGUO

Rais William Ruto anatarajiwa muda wowote kumteua rasmi jaji wa mahakama ya rufaa Mohammed Warsame kuwa jaji wa mahakama ya upeo, kufuatia kuteuliwa kwake hapo jana na tume ya huduma za mahakama, JSC. Warsame ni miongoni mwa watu 5 waliohojiwa kwa muda wa siku mbili na JSC, mahojiano yake yakiendeshwa hapo jana kabla ya kuteuliwa […]

KINDIKI ATOA HAKIKISHO KWA WAWEKEZAJI

Naibu Rais Kithure Kindiki amewahakikishia wawekezaji na wafanyabiashara katika sekta ya kibinafsi kwamba serikali imeweka mikakati ya kutosha kuhakikisha usalama baada ya uchaguzi mkuu ujao, na hivyo hapana haja ya kuhofia biashara zao. Alikuwa akizungumza kwenye kongamano mja akiwahimiza wawekezaji kuwekeza katika nguzo kuu za serikali ambazo ni kilimo, kawi na miundomsingi. Imetayarishwa na Antony […]

BINGWA SAWE AREJEA KWA MBWEMBWE

Shughuli za kawaida zilitatizika kwa muda katika uwanja wa ndege JKIA jana usiku wakati bingwa wa dunia katika mbio za marathon Sebastian Sawe kuwasili uwanjani humo kutoka London. Sawe mwenye umri wa miaka 31 na mzaliwa wa Kijiji cha Ndonyongaria kaunti ya Nandi, alishangaza ulimwengu baada ya kuwa binadamu wa kwanza kukamilisha mbio hizo chini […]

GACHAGUA ADAI MILIONI 80 KAMA FIDIA

Vikao vya kusikiliza kesi kuhusiana na mchakato wa kubanduliwa kutoka afisini kwa aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua vinaingia siku ya pili hii leo huku kiongozi huyo wa DCP akitaka mahakama iamuru serikali imlipe fidia ya shilingi milioni 80 na marupurupu ya kustaafu. Wakati wa vikao vya siku ya kwanza, Gachagua ameiarifu mahakama kwamba hana haja […]

MASOMO JSS NJIA PANDA MUHULA HUU

Muhula wa pili katika shule za msingi na upili umeingia siku ya pili huku wazazi na wanafunzi wa sekondari msingi, JSS wakiachwa kwenye njia panda kutokana na mgomo wa walimu wa shule hizo, ambao wametishia kuendelea na mgomo hadi malalamishi yao yatakapotatuliwa. Miongoni mwa matakwa ya walimu hao waliofanya maandamano hapo jana, ni walimu 44,000 […]