UTABIRI WAONYA MVUA KUBWA KUENDELEA

Wakenya wametakiwa kuchukua tahadhari kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha katika mengi ya maeneo ya nchi, mafuriko ya ghafla na matatizo ya kuona vizuri barabarani yakihofiwa. Kwenye ripoti yake, idara ya utabiri wa hali ya anga imebashiri kuwa mvua itaendelea kunyesha hadi tarehe 4 mwezi ujao, katika maeneo kadhaa ikiwemo nyanda za juu za maeneo […]

IEBC YATOA TARAIFA KUHUSU USAJILI WA WAPIGA KURA

Zoezi la usajili wa wapiga kura wapya limeratibiwa kukamilika hii leo huku tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC ikisema inajitahidi kuwafikia wakenya wote waliohitimu ili kuwasajili kabla ya zoezi hilo kufungwa. Katika taarifa ya hivi punde, IEBC imesema imeafikia asilimia 75 ya wapiga kura wapya milioni 2.5 waliokuwa wamelengwa, Nairobi ikiongoza kwa takribani wapiga […]

CARRICK HANA WASIWASI NA SAFU YA ULINZI

Kocha wa Manchester United Michael Carrick amesema hana wasiwasi wowote kuhusu eneo la beki wa kati kuelekea dirisha la usajili wa majira ya kiangazi, akisisitiza kuwa kwa sasa si kipaumbele kikubwa kwa timu. Carrick pia amefichua kuwa alikutana na mmiliki mwenza wa klabu Sir Jim Ratcliffe katika uwanja wa mazoezi wa Carrington ambapo walifanya mazungumzo ya kirafiki, […]

SYPHAS OTIENO ANG’ARA AKIWA AMERUDI KUTOKA MAJERAHA

Mshambuliaji wa Migori Youth Syphas Otieno ameonyesha furaha yake baada ya kurejea uwanjani kufuatia majeraha na kuchangia pakubwa ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Nzoia Sugar FC katika mechi ya National Super League mwishoni mwa wiki. Otieno ambaye alikuwa nje kwa wiki tatu alicheza dakika 10 za mwisho lakini alifanya athari ya haraka kwa kufunga […]

JOHN NJOGU AAGA KCB BAADA YA MKATABA KUISHA

Kocha mwenye uzoefu John Njogu ametangaza rasmi kuondoka katika klabu ya KCB FC baada ya mkataba wake kumalizika Aprili 26. Kupitia mitandao ya kijamii, Njogu alitoa ujumbe wa hisia akitafakari safari yake ndani ya klabu hiyo, akishukuru kwa nafasi aliyopata na ushirikiano alioupata kutoka kwa wachezaji na benchi la ufundi. Njogu alijiunga na KCB mnamo […]

ADUDA AONYA MVUTANO FKF WATISHIA AFCON 2027

Aliyekuwa Afisa Mkuu Mtendaji wa Shirikisho la Soka Kenya (FKF) Lodvick Aduda ameonya kuwa Kenya inaweza kuhatarisha nafasi yake ya kuandaa michuano ya Mataifa ya Afrika 2027 kutokana na mvutano unaoendelea ndani ya shirikisho hilo. Mvutano huo unamkabili Rais wa FKF Hussein Mohammed na naibu wake McDonald Mariga kufuatia madai ya kashfa ya bima ya […]

WALIMU VIHIGA WATOA NOTISI YA MGOMO KUHUSU SHA

Walimu katika Kaunti ya Vihiga wametoa notisi ya siku 14 kwa Wizara ya Afya pamoja na Tume ya Kuwaajiri Walimu (TSC) kutatua changamoto zinazohusiana na bima ya afya ya SHA au waanze mgomo. Kupitia chama cha walimu KUPPET walimu hao wamesema wamekuwa wakihangaika mara kwa mara wanapotafuta huduma za matibabu. Wamesisitiza kuwa iwapo matatizo hayo […]

SERIKALI YATAKA USHIRIKIANO NA WAENDESHA BODABODA KUIMARISHA USALAMA

Katibu Mkuu wa Usalama wa Ndani Raymond Omollo amewahimiza waendesha bodaboda kote nchini kushirikiana na vyombo vya usalama katika juhudi za kukabiliana na ongezeko la ukosefu wa usalama. Akizungumza Kaunti ya Homabay, Omollo amesema serikali inapanga kutumia waendesha bodaboda kama watoa taarifa muhimu ili kusaidia kubaini na kuripoti shughuli za uhalifu kwa wakati akionya kuwa wachache […]

WAKILI ONGOYA AHOJI MISINGI YA KUMNG’ATUA GACHAGUA

Wakili Elisha Ongoya amesema tafsiri ya Mahakama ya Juu kuhusu “utovu mkubwa wa nidhamu” inahusisha makosa makubwa yanayoweza kuhalalisha kuondolewa madarakani. Ongoya amesisitiza kuwa mashtaka ya aina hiyo yanapaswa kuwa mahususi na yenye uzito sawa na mashitaka ya jinai ili kukidhi viwango vya kikatiba vinavyohitajika katika mchakato wa kuondoa kiongozi madarakani. Amehoji kuwa madai yaliyotolewa […]

RUTO ATOA WITO WA MAGEUZI YA SEKTA YA AFYA AFRIKA

Rais William Ruto ametoa wito kwa mataifa ya Afrika kufanya mageuzi makubwa katika mifumo ya afya kwa kukumbatia ubunifu, ushirikiano na kujitegemea ili kuboresha huduma za afya Akizungumza katika Mkutano wa Kikanda wa Afya Duniani jijini Nairobi Ruto amesema kuna pengo kubwa ambapo Afrika inabeba zaidi ya asilimia 25 ya mzigo wa magonjwa duniani lakini inapokea chini […]