WATU TISA WAUAWA KATIKA MILIPUKO KATIKA GHALA LA RISASI CHAD

Watu tisa wameuawa na wengine 46 kujeruhiwa katika milipuko iliyosababishwa na moto katika ghala la silaha za kijeshi katika mji mkuu wa Chad jana usiku. Kwa mujibu wa waziri wa afya Abdelmadjid Abderahim Idadi ya waliofariki inaweza kuongezeka huku watu wengi wakipata majeraha mabaya. Milipuko hiyo ilitanda angani usiku juu ya kambi ya kijeshi karibu […]

WAPE HAKI WAJANE

Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu wameibua wasiwasi kutokana na kuongezeka kwa kesi za ardhi katika kaunti ya Migori zinazohusu wajane. Huku idadi kubwa ya wajane wakikabiliwa na migogoro ya ardhi kwa miaka mingi katika mahakama wakitafuta haki, kikundi cha watetezi kimehimiza mashirika yote ya serikali yanayoshughulikia masuala ya ardhi kutoa haki kwa waathiriwa. Imetayarishwa na Janice […]

IPITISHWE AMA IANGUSHWE?

Wabunge wanatarajiwa kuanza tena kujadili Mswada wa Fedha wa 2024 ambao umeibua hisia tofauti miongoni mwa Wakenya kutokana na msukumo wake wa kutaka kutozwa ushuru zaidi. Jana jumatano wabunge waliendeleza mjadala kuhusu ripoti iliyotolewa na kamati ya fedha ya bunge la kitaifa Pamoja na mswada wa fedha huku baadhi yao akiwemo mbunge maalum John Mbadi […]

KRA YANYIMWA MPESA, AKAUNTI ZA BENKI ZA WALIPA KODI

Mamlaka ya ukusanyaji Ushuru nchini KRA imepata pigo baada ya ombi lao kutaka kupeleleza akaunti za walipa kodi za Mpesa na benki kukataliwa. Katika mkakati mpya wa kufichua udanganyifu wa kodi, mtoza ushuru, kupitia Hazina ya Kitaifa, KRA ilitaka kupewa kibali cha kuwa na data za walipa kodi za benki na mpesa. Mswada wa Fedha, […]

WAFURUSHE WANAKANDARASI WAZEMBE; WAKAZI WAAMBIA SERIKALI YA KISUMU

Wakaazi wa kaunti ya Kisumu wameitaka serikali ya kaunti hiyo kuharakisha kukamilisha miradi iliyokwama katika kaunti nzima. Wakizungumza katika ukumbi wa Kosawo katika kaunti ndogo ya Kisumu Mashariki wakati wa Huduma Mashinani inayolenga kuboresha utoaji wa huduma, wakazi hao wameitaka serikali ya kaunti kuchukua hatua dhidi ya wanakandarasi wanaochelewesha miradi hiyo, ambayo kulingana nao imewanyima […]

HUDUMA ZA AFYA HAZIPO KASKAZINI MWA BONDE LA UFA

Utoaji wa huduma katika Hosipitali za umma eneo la kaskazini mwa bonde la ufa utaendelea kutatizika zaidi baada ya maafisa wa kliniki kuhapa kuendeleza mgomo wao hadi malalamishi yao yatekelezwe. Kwa mujibu wa muungano wa maafisa hao KUCO serikali imekosa kutekeleza makubaliano baina yao hali ambayo kulingana nao ni kutelekezwa. Imetayarishwa na Janice Marete

KAUNTI YA MURANG’A KUWAPA WAFANYIKAZI BIMA YA AFYA

Serikali ya kaunti ya Murang’a imetangaza mipango ya kuwapa wafanyikazi wake bima ya matibabu kwa sekta ya kibinafsi mara tu Hazina ya Bima ya Afya ya Jamii (SHIF) itakapoanza kutekelezwa. Utawala wa kaunti pia unapanga kusambaza baadhi ya vipengele vya mpango wake wa bima ya matibabu bila malipo unaojulikana kama Kang’ata Care kwa sekta ya […]

IDARA YA MAJANGA YAONYA KUHUSU HALI MBAYA

Mamlaka ya Usimamizi wa majanga nchini NDMA imesema, watu wapatao milioni 1.9 wanahitaji msaada wa chakula, wakati hali ya Uchumi ikizidi kuwa mbaya kati ya mwezi wa Juni na Agosti. Mamlaka hiyo imetoa ripoti mpya kwa mwezi wa Mei ikisema kuwa idadi kubwa ya waathiriwa wako katika kaunti 23 kame na nusu kame nchini. Mamlaka […]

SINOMA YAONDOA ‘NOMA’ YA MAZINGIRA

Kampuni ya China kwa jina SINOMA ya kuunda vifaa vya kuweka paa za nyumba imefungua kiwanda kipya nchini ili kulipatia soko la taifa hili vifaa hivyo vya bei nafuu, ambavyo ni vya kudumu na ni salama kwa mazingira. Akizungumza mjini Machakos kwenye ufunguzi wa kiwanda hicho, meneja mkuu wa Kampuni ya SINOMA Wu Shuang, amesema Kenya na […]

OBADO BADO KIKAANGONI

Mahakama kuu imeipa ruhusa tume ya maadili na kukabili ufisadi EACC kuipiga mnada mali ya thamani ya shilingi milioni 235 ya aliyekuwa gavana wa Migori Okoth Obado, anayokisiwa kuipata kupitia njia za udanganyifu. Miongoni mwa mali hiyo ni nyumba za makazi katika mtaa wa Loresho jijini Naiorbi na magari mawili ya kifahari, ambayo EACC inasema […]