BADILISHENI VITAMBULISHO; BITOK ASEMA

Julius Bitok katibu katika wizara ya uamiaji amesema kuwa kila mkenya atahitajika kuwa na kitambulisho cha kitaifa cha kisasa kinachojulikana nkama maisha Crad. Kwa mujibu wa balozi Bitok serikali imeweka mikakati ya kiutosha kuhakikisha kwamba wananchi wanapata vitambulisho hivyo vya kisasa ili kudumisha usalama na kwamba kitambulisho hicho kitakuwa kinabadilishwa baada ya muda fulani. Imetayarishwa na Janice Marete

MAAFISA WAKUU WAKAMATWA KWA MADAI YA ULAGHAI KATIKA AFISI YA MUDAVADI

Ofisi ya Waziri mwenye mamlaka makuu na Wizara ya Mambo ya Nje Musalia Mudavadi imethibitisha kukamatwa kwa baadhi ya viongozi waandamizi katika wizara hiyo. Katika taarifa, uchunguzi uliofanywa siku ya Jumamosi ulisababisha kukamatwa kwa watu hao kwa madai ya kusaidia walaghai ambao wanasemekana kuwalaghai wageni katika afisi ya Mudavadi. Kwa mujibu wa taarifa hiyo ililenga […]

WATOTO WATATU WAANGUSHWA NA GARI LA POLISI KITUI

Watoto watatu wenye umri wa kati ya miaka saba na minane wanapokea matibabu katika hospitali moja huko Kyuso, Kaunti ya Kitui baada ya kuangushwa na gari la polisi jana jumapili. Ajali hiyo ilitokea katika eneo la Kamuwongo huku polisi wakiendesha gari kutoka Kakunike kuelekea Kyuso. Kwa mujibu wa Chifu msaidizi wa eneo hilo David Mwendwa […]

WACHA WATOTO NAIROBI WALE, MAHAKAMA

Jaji wa mahakama kuu Chacha Mwita ametupilia mbali kesi ya kupinga mpango wa lishe shuleni maarufu kama Dishi na Kaunti chini ya serikali ya kaunti ya Nairobi, akisema kusitisha mpango huo ni ishara ya kutojali maslahi ya wanafunzi. Kesi hiyo ilikuwa imewasilishwa na kikundi cha Tunza Mtoto Coalition Kenya kupinga mpango huo kikisema ni haramu […]

ERIC OMONDI AKAMATWA

Maafisa wa polisi jijini Nairobi wamemkamata msanii Eric Omondi alipokuwa akiandamana nje ya majengo ya bunge kupinga mswada wa fedha wa mwaka 2024. Kulingana na kanda ya video ambayo imesambaa mitandaoni, Omondi amekuwa kwenye maandamano na wenzake wakiwa wamevaa mavazi mekundu Omondi amekuwa akiandamana kutumia farasi. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

HONGERA WABUNGE; DUALE ANAWAAMBIA WABUNGE

Waziri wa Ulinzi Aden Duale amewapongeza Wabunge waliopiga kura kupitisha Mswada tata wa Fedha wa 2024. Katika taarifa Duale amesema wabunge hao wameonyesha ujasiri kwa kupiga kura ya kupitisha mswada huo kwa manufaa ya wananchi. Duale ameongeza kuwa kwa sasa anatazamia hatua inayofuata ya Bill huku akibainisha kuwa pamoja na kwamba kuna maoni yaliyogawanyika kuhusu […]

KAZI YA POLISI SIO KUUA NI KULINDA;IPOA

Mamlaka ya kutathmini utendakazi wa maafisa wa polisi IPOA imeanzisha uchunguzi kufuatia kifo cha mmoja wa waandamanaji Rex Masai anayesemekana kuawa kwa kupigwa risasi na afisa wa polisi wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha. Ann Makori mwenyekiti wa IPOA amewashtumu maafisa wa polisi kwa kutumia nguvu kupita kiasi kuwatawanya waqandamanaji. Viongozi mbali mbali […]

SIMAMA NA FAMILIA YA REX MASAI

Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino amewataka Wakenya kusimama na familia ya Rex Kanyike Maasai, ambaye inasemekana aliuawa wakati wa maandamano ya jana Alham jioni. Inasemekana kwamba Rex alipigwa risasi na kuuawa mwendo wa saa saba mchana katika barabara ya Moi avenue jijini Nairobi wakati wa maandamano ya kupinga Mswada wa Fedha wa 2024. Akizungumza […]

SAKAJA AZINDUA UJENZI WA UWANJA WA KIHUMBUINI WA KSH.277 MILIONI

Gavana wa kaunti ya Nairobi Johnson Sakaja amezindua ujenzi wa uwanja wa michezo wa Kihumbuini, mradi utakao gharimu shilingi milioni 277. Akizungumza katika hafla ya kuzindua mradi huo Gavana Sakaja amesisitiza kuwa uwanja huo utajengwa kwa viwango vya kimataifa, ikilenga kuimarisha soka jijini Nairobi. Sakaja aidha ameangazia kuwa uwanja huo pindi tu utakapokamilika utachangia katika […]

TUWATUNZE WANYAMA ;DKT ALFRED MUTUA

Utalii humu nchini huchangia asilimia 12 ya pato la taifa, hay ani kwa mujibu wa Waziri wa Utalii na wanyamapori Dkt Alfred Mutua akizungumza wakati wa zoezi la kitaifa la kutathmini hesabu ya wanyama pori humu nchini kaunti ya narok ambapo ameongeza kuwa zoezi hilo litaimarisha mikakati ya uhifadhi na usimamizi bora wa wanyamapori kote […]