“POMBE YA MAUTI NA JELA”

Mahakama Kuu mjini Eldoret imewahukumu wafanyakazi wawili kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kuhusika na mauaji ya kikatili ya mfanyakazi mwenzao wakati wa unywaji wa pombe. Walipofikishwa mbele ya Jaji Reuben Nyakundi, wawili hao, Daniel Kiprotich na Meshack Kipchirchir, wamepatikana na hatia ya kumuua Nicholas Tenai mnamo Septemba 28, 2019, katika kituo cha biashara cha […]

MUDAVADI APENDEKEZA NYONGEZA YA FEDHA KWA WIZARA YAKE

Msimamizi wa maswala ya kigeni ambaye pia ni Waziri mwenye mamlaka makuu Musalia Mudavadi ameitaka serikali kuongeza mgao wa fedha katika wizara yake. Kwa mujibu wa Mudavadi wizara yake inahitaji fedha Zaidi ili kufanikisha shughuli zake kikamilifu. Ameongeza kuwa serikali imefanikiwa kutia Saini mikataba mbali mbali na serikali za mataifa menginee Pamoja na sekta binafsi […]

OGAMBA: SERIKALI INAJIKAZA KUMALIZA MGOMO WA WAHADHIRI

Serikali inajisatiti kuhakikisha wahadhiri wanaogoma wanarejea kazini, haya ni kwa mujibu wa waziri wa elimu Julius Ogamba akiongeza kuwa mazungungumzo yangali yanaendelea baina ya wahadhiri na serikali katika juhudi za kumaliza mgomo unaoendelea. Kuhusu swala la matatizo yanayokikumba chuo kikuu cha moi mjini Eldoret Ogamba amesema kuwa ni jambo la kusikitisha kuona baathi ya wanafunzi […]

WHO: WATU 3000 HUFARIKI KILA SIKU KATIKA AJALI ZA BARABARANI

Utafiti uliofanya na shirika la afya duniani WHO unaonyesha kuwa zaidi ya watu 3000 hupoteza Maisha kutokana na ajali za barabarani kila siku. WHO imetoa wito kwa watu wote duniani kuwaunga mkono waliofiwa na wale wanaopatwa na kiwewe cha kisaikolojia cha mda mrefu kutokana na ajali hizo. Imetayarishwa na Janice Marete

NTSA YATOA WITO KWA WAKENYA KUDUMISHA USALAMA BARABARABANI

Washikadau mbali nbali katika sekta ya uchukuzi wametakiwa kuchukua tahathari za mapema ili kuhakikisha visa vya ajali ambavyo vinaweza kuzuiliwa vinazuiwa haswa msimu huu wa krismasi. Mshirikishi wa mamlaka ya kitaidfa ya uchukuzi na usalama barabarani NTSA tawi la Nyanza Isaac Silali ametoa wito kwa wananchi kushirikiana na idara husika ili kudumisha usalama barabarani. Imetayarishwa na […]

SIMBAS WAANGAZIA KOMBE LA AFRIKA 2025 BAADA YA KOMBE LA ELGON

Simbas waelekeza umakini wao kwa Kombe la Afrika la 2025 baada ya kushinda Kombe la Elgon. Msaidizi wa kocha wa Kenya Simbas, Carlos Katywa, anaamini ushindi wao dhidi ya Uganda Cranes katika Kombe la Elgon la 2024 umeweka msingi wa maandalizi yao kwa Kombe la Afrika la Raga la 2025 linalotarajiwa kufanyika Uganda. Simbas walishinda […]

NAIROBI UNITED YASHINDA APS 1-0

Nairobi United ilishinda 1-0 dhidi ya Administration Police Service (APS) Bomet na kusimamisha mbio zao nzuri katika Ligi Kuu ya Taifa. Nairobi United ilifunga kupitia kijana Dancun Omalla, ambaye aliongeza idadi yake ya mabao kuwa matano, baada ya michezo tisa. Kocha wa Nairobi United, Edwin Mwaura, amesema bado hawajafika wanapotaka kuwa licha ya ushindi mdogo. […]

MWAURA ATETEA SERIKALI DHIDI YA KUFELI, MSWADA WA CHERARGEI

Kauli za viongozi wa kidini za kuikosoa serikali ya Kenya Kwanza zimeendelea kuibua shutuma kutoka kwa serikali hiyo, wa hivi punde akiwa msemaji wa serikali Isaac Mwaura ambaye amesema kuwa serikali imewajibika kwa kuwaajiri walimu na kupambana na ufisadi. Akizungumza na wanahabari jijini Nairobi, Mwaura amesema kuwa serikali imefanikiwa kurejesha shilingi bilioni 28 kutoka kwa […]

RUTO AJITETEA DHIDI YA VIONGOZI WA KIDINI

Wakati uo huo, Rais William Ruto mwenyewe amechukua jukumu la kuitetea serikali yake dhidi ya kauli za viongozi wa kidini za hapo jana kwamba serikali yake imejaa ubinafsi badala ya kuyashughulikia maslhai ya wakenya. Akizungumza katika hafla ya kufuzu katika chuo kimoja jijini Nairobi, Rais amewataka viongozi wa kidini na wakenya kwa jumla kuzingatia ukweli […]

HAKUNA WIZI WA MTIHANI, WIZARA YAKANA

Huku uadilifu wa mtihani wa kitaifa wa kidato cha 4 KCSE ukitiliwa shaka kutokana na visa vya udanganyifu, serikali imesema kwamba mtihani huo uko salama kwamba hakujakuwa na udanganyifu wowote. Akizungumza kwenye kaunti ya Meru mapema leo, katibu katika wizara ya elimu Dakta Belio Kipsang amesema majaribio ya wizi yamezimwa huku akiongeza kuwa karatasi za […]