POLISI WAATHIRWA WAKUBWA, KANJA AFICHUA

Katika juhudi za kuboresha utendakazi wa polisi na kuimarisha huduma yao kwa wananchi, Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja ameongoza mkutano wa kujadili matatizo ya akili na msongo wa mawazo miongoni mwa maafisa hao ili kupata suluhu. Kongamano hilo ambalo limeandaliwa jijini Nairobi limewaleta Pamoja maafisa wakuu wa idara ya polisi na wale wa upelelezi […]

ELIJAH WACIRA: WIZARA YA AFYA YAKOSOLEWA

Hatua ya wizara ya afya kumtimua afisa mkuu mtendaji wa bodi ya bima ya afya Elijah Wacira imeibua hisia mseto, maafisa wa kiliniki wakiwa wa hivi punde kuikosoa wizara hiyo wakisema uamuzi huo si suluhu kwa matatizo yaliyo kwenye bima hiyo. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kitaifa Peterson Wacira, ufisadi umekithiri katika wizara ya afya […]

WAKENYA WAENDELEA KUSHINIKIZWA KUJIANDIKISHA KWA SHA

Wito umetolewa kwa wakenya kuendelea kujitokeza na kujisajili katika bima ya afya ya jamii SHA. Akitoa wito huo mwakilishi wa kike katika kaunti ya Nyandarua Faith Gitao anasema kuwa mpango wa kujisajili na bima hiyo ukitekelezwa ipasavyo utatoa ulinzi wa afya na usalama wa kifedha kwa wakenya haswa walio na mapato ya chini. Gitau aidha […]

MWANAMKE AFARIKI KATIKA AJALI YA BARABARA KWENYE BARABARA YA LANG’ATA

Mwanamke mmoja amefariki kutokana na majeraha aliyopata kufuatia ajali ya barabarani katika barabara ya Lang’ata karibu na bustani ya Uhuru. Mwanamke huyo ambaye hajatambuliwa anasemekana kuwa alikuwa akivuka barabara wakati gari lililokuwa likielekea Lang’ata kutoka kutoka jijini nairobi lilipomgonga. Kulingana na polisi marehemu amepata majeraha mabaya na kufariki papo hapo. Mwili huo umepelekwa katika chumba […]

WANASIASA CHIPUKIZI WATETEA BEI YA SHILINGI 3500 INAYONUIWA KUNUNUA MAHIDI YA GUNIA YA KILO TISISNI NA SERIKALI

Wanasiasa chipukizi katika kaunti ya Transnzoia wametamaushwa na hatua ya serikali kupunguza bei ya mahidi gunia moja ya kilo 90 kutoka 4000 hadi 3500. Kulingana na wanasiasa hao wakulima waliuziwa mbolea ya bei nafuu isiyoafikia ubora wa viwango vinavyohitajika na wizara ya kukadiria ubora wa bidhaa KEBS huku wakitoa wito kwa rais William Ruto kuingilia […]

ROBO FAINALI YA UEFA YAINGIA DIMBANI

Ufaransa, Italia na Ureno zinachuana kuwania kufuzu kwa robo fainali ya UEFA Nations League, huku matumaini ya England yakikabiliwa na ati ati kutokana na kuenguliwa kwa wachezaji kadhaa. Huku Uhispania na Ujerumani zikiwa tayari zimefuzu kwenda mbele, nafasi sita zimesalia wakati duru mbili za mwisho za mechi za kundi zikikaribia. Italia na Ureno zinahitaji sare […]

KOCHA WA LIONESS APONGEZA KIKOSI CHAKE

Kocha mkuu wa timu ya Kenya Lionesses Dennis Mwanja ameipongeza timu yake baada ya kumaliza katika nafasi ya pili katika mashindano ya Rugby Africa Women’s 7s yaliyomalizika hivi punde nchini Ghana. Simba waliangukia kwenye kizingiti cha mwisho dhidi ya mabingwa watetezi Afrika Kusini lakini Mwanja ana matumaini na kile kitakachowangoja wasichana hao.Kocha msaidizi wa KCB […]

MATHARE UNITED WAJIANDAA KUBAKIA NAFASI NZURI KWENYE LIGI

Huku wakiwa na imani mpya na timu hiyo, Mathare United wanalenga kuwa na mbio za kuvutia ili kulinda nafasi yao katika Ligi Kuu ya Kenya. Timu hiyo iliyorejeshwa daraja la kwanza mwanzoni mwa msimu huu, hadi sasa imeshinda mechi tatu, sare mbili na kupoteza tatu na kukaa nafasi ya sita kwenye jedwali kwa pointi 11. […]

PPB YAENDESHA ‘MSAKO WA AFYA BORA’

Wakenya wanatarajia kuimarika kwa ubora wa dawa na usalama wa afya yao kufuatia msako unaofanywa na bodi ya sumu na dawa nchini dhidi ya usambazaji wa dawa haramu kwenye maduka ya dawa na wahudumu wengine wa afya. Msako huo unaendeshwa kwa ushirikiano na idara ya polisi ukiwalenga wawasilishaji wa vifurushi ama parcels na wasafirishaji mizigo […]

SERIKALI NAROK YARAHISISHA USAFIRI WA MAAFISA

Katika juhudi za kuimarisha utendakazi wa wasimamizi wa wadi na kuboresha Maisha ya wakazi katika kaunti ya Narok, serikali ya kaunti hiyo imewanunulia wasimamizi hao pikipiki ili watumie wanapokuwa katika utekelezaji wa majukumu yao. Akizungumza wakati wa zeozi la kuwapokeza pikipiki hizo, gavana wa Narok Patrick Ole Ntutu amesema kuwa usafiri umekuwa kikwazo kikubwa kwa […]