MAGEUZI MAPYA SEKTA YA CHAI YAJADILIWA

Wakulima wa chai nchini huenda wakapata afueni kufuatia mikakati mipya ya mageuzi iliyoandaliwa na Wizara ya Kilimo huku Katibu wa wizara hiyo Kiprono Ronoh akikutana na wadau wa sekta ya chai kujadili namna ya kuongeza uzalishaji, kupanua masoko na kuboresha kipato cha mkulima. Wadau wamesisitiza umuhimu wa utafiti wa kina ili kuinua ubora wa chai […]

MWANAMKE NA BINTI YAKE WAFA KATIKA AJALI YA BARABARANI

Polisi wameanzisha uchunguzi kuhusu ajali iliyotokea katika Kituo cha Biashara cha Sikri kilichopo barabara ya Oyugis-Sondu, eneo la Rachuonyo Kusini, Kaunti ya Homa-Bay, ambapo mwanamke mwenye umri wa kati na binti yake wamefariki baada ya pikipiki yao kugongwa na trela. Kwa mujibu wa taarifa, Pamela Ondiek na binti yake wamefariki papo hapo, huku dereva wa […]

MICHEZO YA SEKONDARI KUANZA RASMI LEO MOMBASA

Hatua Kitaifa ya Muhula wa Kwanza Michezo ya Shule za Sekondari ya Kenya (KSSSA) 2025, zimepangwa kuanza hii leo huku mabingwa wa kanda wakikutana Mombasa kwa wiki moja ya mashindano makali. Kuanzia leo hadi Aprili 12, Mombasa itakuwa kitovu cha michezo ya shule za upili, huku Shule ya Upili ya Wavulana ya Shimo la Tewa, […]

MIKEL ARTETA ASEMA ARSENALI INA UWEZO WA KUINDOA REAL MADRID

Mikel Arteta hana shaka kwamba Arsenal wanaweza kuisumbua Real Madrid katika leo katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa. The Gunners hawajawahi kutawazwa mabingwa wa Uropa na watakutana na washindi mara 15 katika robo fainali huko Emirates leo na huku marudiano huko Madrid wiki ijayo. Timu hizo mbili zimekutana mara mbili pekee katika michuano ya […]

KISPED WAIMARISHA MCHEZO WAO KWA USHINDI MKUBWA

Katika onyesho la hali ya juu ambalo linaweza kubainisha msimu wao, timu ya FKF ya Ligi Kuu ya Wanawake Kisped Queens ilichukua hatua muhimu kuelekea kunusurika kwenye ligi kwa ushindi mnono wa 2-1 dhidi ya Bunyore Starlets mnamo Jumamosi. Ushindi huo mahususi uliwainua wachezaji hao wa kwanza wa WPL kutoka kwenye eneo la kushushwa daraja […]

JUNIOR STARLETS WAMALIZA KWA KISHINDO

Timu ya wasichana ya U17 ya Kenya, Junior Starlets, ilikamilisha ziara yao nchini Morocco kwa kishindo, na kuandikisha ushindi wa 2-0 dhidi ya Morocco U17 katika mechi yao ya pili ya kirafiki iliyochezwa Jumatatu katika Uwanja wa Mohammed VI Sports Complex. Mitshel Waithera na Elizabeth Ochaka waliibuka kidedea kwa kufunga bao kila mmoja kukamilisha ushindi […]

ZIARA YA KUREJESHA USALAMA PWANI

Katika juhudi za kurejesha utulivu katika eneo la Pwani kufuatia misururu ya visa vya uvamizi wa vijana wanaojiita Panga Boys, waziri wa usalama Kipchumba Murkomen na wakuu wa usalama wanazuru kaunti 6 za powani ili kutathmimini mbinu za kuondoa magenge hayo. Waziri huyo amefanya kikao na maafisa wa usalama jijini Mombasa, akisema ziara hiyo inalenga […]

SAKATA YA MALARIA YAMWANDAMA TUM

Mhandisi Peter Tum aliyeteuliwa na Rais William Ruto kuwa balozi wa Kenya nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amelazimika kujitetea dhidi ya sakata ya shilingi bilioni 3.7 za ununuzi wa vyandarua vya kuzuia Malaria alipokuwa katibu mkuu katika wizara ya afya. Akiwa mbele ya kamati ya masuala ya kigeni katika bunge la kitaifa, Tum amesema […]

PARENO, KARUGU WAHOJIWA

Kamati ya ulinzi na masuala ya kigeni katika bunge la kitaifa imewahoji Daktari Caroline Karugu na Judith Pareno walioteuliwa na Rais William Ruto kuhudumu kama katibu mkuu kwenye wizara ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na idara ya haki na masuala ya kikatiba mtawalia. Daktari Karungu ametakiwa kuzungumzia uchaguzi wa mwenyekiti wa tume ya umoja wa […]

WAKENYA 6 WASAKWA

Zoezi la kuwasaka wakenya 6 kujaza nafasi za makamishna wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC linaendelea, wakenya 5 wakijitetea hii leo mbele ya kamati ya uteuzi kuhusiana na uwezo wao wa kuhudumu kwenye tume hiyo. Wanaohojiwa hii leo ni Grace Surpin, Hali Mutisya, Humphrey Kimani, Issak Shaban na Ibrahim Rashid. Imetayarishwa na Antony […]