SERIKALI YAKODISHA VIWANDA VYA SUKARI ILI KUFUFUA SEKTA YA SUKARI

Serikali imeanzisha hatua mpya ya kufufua sekta ya sukari nchini kwa kukodisha viwanda vinne vya sukari kwa kipindi cha miaka 30 vilivyokuwa vikikumbwa na changamoto kubwa za kifedha. Kampuni ya Kibos Sugar and Allied Industries Limited imechukua usimamizi wa Chemelil Sugar, Muhoroni Sugar Factory sasa iko chini ya West Valley Sugar Company, West Kenya Sugar […]

KENYA YAONDOA IMF KWENYE BAJETI

Kenya imejitoa katika kupata fedha kutoka kwa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kwenye bajeti yake inayokuja, itakayoanza Julai mwaka huu. Hatua hii inaashiria jitihada za kuepuka masharti magumu ya IMF kama vile ongezeko la ushuru, kufungiwa ajira, na kupunguzwa kwa matumizi ya serikali. Hati za bajeti zilizowasilishwa bungeni zinaonyesha kuwa hakuna fedha kutoka IMF […]

WAKAZI TURKANA KUKOSA HUDUMA ZA MAABARA

Huduma za maabara katika hospitali za umma kwenye kaunti ya Turkana zimesambaratika kufuatia mgomo wa maafisa wa maabara wanaohudumu katika wizara ya afya kwenye kaunti hiyo wanaolalamikia mazingira magumu ya kazi. Wakiongozwa na mwenyekiti wa muungano wao tawi la Turkana Moses Emoit, maafisa hao wamesema hawatarejea kazini hadi hali itakaporekebishwa, ikiwemo kuongeza idadi ya maafisa […]

SERIKALI YATANGAZA AFUENI MAU

Mzozo wa ardhi katika msitu wa Mau hatimaye umepata suluhu baada ya zoezi la upimaji wa msitu na kuweka mipaka baina ya msitu huo na ardhi ya wakazi kukamilika, wakazi sasa wakiratibiwa kupokezwa hatimiliki ndani ya muda wa wiki moja. Tangazo hilo limewekwa wazi na katibu mkuu katika wizara ya ardhi Nixon Korir, akisisitiza kuwa […]

USHIRIKIANO WA KENYA-FINLAND

Uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano wa kibiashara baina ya Kenya na Finland unatarajiwa kuimarika kufuatia mikataba mbali mbali itakayotiwa Saini kati ya Rais William Ruto na mwenzake wa taifa hilo Alexander Stubb ambaye yuko nchini. Alexander na mkewe Suzanne Ines-Stubb wamepokelewa katika Ikulu ya Nairobi kwa ziara ya siku 3 humu nchini. Imetayarishwa na Antony […]

ONG’ONDO: MSHUKIWA MKUU KUWASILISHWA JKIA

Mshukiwa mkuu wa mauaji ya aliyekuwa mbunge wa Kasipul Ong’ondo Were, Isaac Kuria aliyekamatwa hapo jana katika eneo la Isebania, ameratibiwa kuwasilishwa katika mahakama ya JKIA majira ya 2pm ambapo polisi wanatarajiwa kuomba muda zaidi wa kuendelea kumzuilia wanapoendesha uchunguzi. Kuria anayeaminika kufyetua risasi iliyomuua Ong’ondo, alikamatwa akiwa mafichoni, polisi wakikisia kwamba alikuwa na njama […]

WAKULIMA WA MIWA WAPINGA ‘KUVURUGIWA UTAMU’

Kundi la wakulima wanaouza miwa yao katika kiwanda cha Nzoia kaunti ya Bungoma wamepinga vikali maandamano yaliyopangwa na viongozi wanaopinga kukodishwa kwa kiwanda hicho kwa mwekezaji wa kibinafsi, wakiwataja viongozi hao kama wabinafsi. Wakizungumza na wanahabari mjini Webuye, wakulima hao wakiongozwa na David Opala, uwepo wa kiwanda hicho chini ya serikali hakujawafaidi kwa muda mrefu, […]

PHILLIP AROKO KUSALIA KIZUIZINI KWA SIKU SABA ZAIDI

Phillip Aroko, mshukiwa wa mauaji ya Mbunge wa Kasipul Charles Were, ataendelea kuzuiliwa na polisi kwa siku saba kama ilivyoamriwa na mahakama ya chini, kwa mujibu wa agizo la Mahakama Kuu. Mshukiwa huyo alifikishwa katika mahakama ya JKIA chini ya ombi maalum, ambapo Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) iliomba muda zaidi wa kumzuilia ili […]

KENYA YAANZISHA MASHAURIANO YA KISIASA NA DOMINIKA

Sekta ya usalama, afya, biashara na uwekezaji zasimama kidedea katika mashauriano ya kwanza ya kisiasa kati ya Kenya na Jamhuri ya Dominika. Waziri Mkuu Musalia Mudavadi, yuko Santo Domingo, mji mkuu wa Dominika, kwa mazungumzo na uongozi wa taifa hilo la Karibi kuhusu ushirikiano katika nyanja hizo muhimu. Mudavadi ambaye ameandamana na Mshauri wa Usalama […]

KARUA AIKOSOA SERIKALI KWA KUTOA KIPAUMBELE USALAMA WA VIONGOZI

Kinara wa chama cha Peoples Liberation Party, Martha Karua, ameikemea vikali idara ya usalama kwa kuharakisha uchunguzi wa kifo cha Mbunge wa Kasipul, Charles Were, huku visa vingine vingi vya mauaji dhidi ya Wakenya wa kawaida vikiendelea kupuuzwa. Karua anasema hatua hiyo inaonesha kuwa serikali haijajitolea kikamilifu kuhakikisha haki kwa waathiriwa wote, bali inaelekeza juhudi […]