DCI KUCHUNGUZA MADAI YA SIMU YA TALAM KUTUMIKA

Idara ya Dci imeagizwa kuchunguza madai ya kutumika kwa simu ya Ocs wa kituo cha central kutuma jumbe za kuitisha fedha kutoka kwa watu tofauti. Hakimu mkuu katika mahakama ya milimani Benmark Ekhubi ameutaka upande wa mawakili wake Samson Talam kutotumia suala hilo kutia doa kwenye uchunguzi unaoendeshwa na mamlaka ya Ipoa. Simu yake Talam […]

ALIYEKUWA MKUU WA TSC NANCY MACHARIA APATA AJIRA MPYA

Aliyekuwa afisa mkuu mtendaji wa tume ya kuwaajiri walimu TSC Nancy Macharia, ameteuliwa na gavana wa Murang’a Irungu Kang’ata kuwa mwenyekiti wa bodi ya huduma za umma kwenye kaunti hiyo, siku chache kabla ya kuondoka kutoka TSC tarehe 30 mwezi huu. Kupitia kwa waraka kwa bunge la kaunti ya hiyo, Macharia ni miongoni mwa watu […]

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA MWANAHARAKATI NJERI

Ni afueni kwa mwanaharakati Rose Njeri aliyekamatwa baada ya kutengeza tovuti ya kuwawezesha wakenya kutoa maoni yao kuhusu mswada wa fedha, baada ya mahakama kutupilia mbali kesi dhidi yake. Kwenye uamuzi wake, hakimu mwandamizi wa mahakama ya Milimani Geoffrey Onsaringo, amesema stakabadhi zilizowasilishwa mahakamani zilikosa kuafikia viwango hitajika kwa kesi kuendelea. Njeri aliyetuhumiwa kwa makosa […]

AFISA WA POLISI MUKHWANA RUMANDE SIKU 21 ZAIDI

Mahakama imeagiza kuzuiliwa kwa siku 21 zaidi afisa wa polisi James Mukhwana, aliyekiri kumtesa mwalimu na bloga Albert Ojwang kwa maagizo ya OCS wa kituo cha polisi cha Central Samson Taalam na naibu inspekta mkuu wa polisi aliyejiondoa kwa muda Eliud Lagat. Kwenye uamuzi wake, hakimu Robinson Ondieki amekubaliana na sababu za upande wa mashtaka […]

MADEREVA, BODA BODA KUKAZA KAMBA CHINI YA SHERIA MPYA

Waendesha boda boda na madereva wa magari ya umma wanaojihusisha ukiukaji wa kanuni za barabarani watalazimika kukaza mkanda baada ya wabunge kuidhinisha mswada wa fedha 2025 ambao una sheria na kanuni zilizochapishwa na Waziri wa uchukuzi nchini Davis Chirchir zinazowalenga ili kuleta mabadiliko na ubora katika sekta ya uchukuzi. Baadhi ya sheria alizopendekeza Waziri ni […]

MAHAKAMA YAWAPA WANAUME AFUENI

Ni afueni kwa wanaume kufuatia uamuzi wa mahakama kuu ambao umetangaza kuwa kinyume na katiba kipengee cha 29 cha sheria za urithi, ikisema kipengee hicho kinawabagua wanaume waliofiwa na wake zao. Kwenye uamuzi wake, jaji Lawrence Mugambi ameauru kuwa kipengee hicho kinachowataka wanaume kuthibitisha kuwa walikuwa wakiwategemea wake zao kimaisha kabla ya kupewa sehemu ya […]

AFUENI KWA KYLIAN MBAPPE

Nyota wa Real Madrid, Kylian Mbappe amelazwa katika hospitali nchini Marekani baada ya kuugua mdudu wa tumbo, miamba hao wa Uhispania walisema Alhamisi. Mshambulizi Mfaransa Mbappe alikosa mechi ya ufunguzi ya Kombe la Dunia la Klabu ya Real Madrid dhidi ya Al-Hilal siku ya Jumatano, sare ya 1-1 katika mchezo wa kwanza wa Xabi Alonso […]

DIVAS WAWALAZA WENYEJI UAE

Timu ya taifa ya netiboli, Divas, iliwashangaza wenyeji Falme za Kiarabu kwa ushindi mnono wa 58-50 kwenye Kombe la Netiboli la UAE huko Dubai, ikitoa taarifa ya utendaji dhidi ya timu yenye uzoefu zaidi na yenye viwango vya juu zaidi. Ushindi huu unakuwa ushindi wa pili mfululizo kwa Kenya katika dimba hilo na kuwahakikishia nafasi […]

MANCHESTER CITY WAPIGWA FAINI YA PAUNI MILLIONI MOJA

Manchester City wamepigwa faini ya zaidi ya pauni milioni 1 na Premier League kutokana na kuchelewa kuanza kwa mechi tisa msimu uliopita. Maafisa wa Ligi ya Premia walitangaza Alhamisi kuwa kikosi hicho cha Pep Guardiola kilikiuka kanuni za kuchezwa kwa mechi na saa za kuanza tena kati ya Oktoba na Februari. Muda mrefu zaidi uliocheleweshwa […]

STARLETS MBIONI KUTWA TAJI LA CECAFA

Harambee Starlets wamesalia na mchezo mmoja tu kutwaa ubingwa wa CECAFA kwa Wanawake kufuatia ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Sudan Kusini Uwanja wa Azam Sports Complex jijini Dar es Salaam, Tanzania mnamo Alhamisi. Ushindi huo uliifanya timu hiyo inayonolewa na kocha Beldine Odemba kuibuka na ushindi wa tatu mfululizo na kuwa kileleni mwa […]