KENYA KUANDAA FAINALI ZA CHAN

SHIRIKISHO la Soka barani Afrika (CAF) limetangaza nchi zitakazoandaa sherehe za ufunguzi na fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) mwaka huu. Kenya imepewa haki ya kuandaa fainali, huku mechi ya ufunguzi ikifanyika nchini Tanzania. Uganda itakuwa mwenyeji wa mechi ya mshindi wa tatu/nne kama ilivyotangazwa na CAF kupitia tovuti […]

MSWADA WA FEDHA: KIPENGEE TATA CHATEMWA

Wakenya wanaolipa ushuru wamepata afueni baada ya kipengee chenye utata kilicholenga kuipa nguvu mamlaka ya kukusanya ushuru KRA kufikia deta zao bila idhini yao au ya mahakama kuondolewa kwenye mswada wa fedha wa mwaka wa 2025-26. Kipengee hicho kilichozua shutuma dhidi ya KRA, kililenga kuiruhusu mamlaka hiyo kufikia maelezo ya kibinafsi ya walipa ushuru ikiwemo […]

MACHO YOTE IPOA BAADA YA KUMHOJI DIG LAGAT

Wakenya wanasubiri kuona ni hatua gani ambayo mamlaka ya kuchunguza mienendo ya maafisa wa polisi IPOA itamchukulia naibu inspekta mkuu wa polisi aliyejiondoa kwa muda Eliud Lagat baada yake kuandikisha taarifa na mamlaka hiyo kuhusu kifo cha mwalimu na bloga Albert Ojwang. Licha ya maelezo yake kutowekwa wazi, taarifa zimearifu kuwa Lagat alihojiwa kwa saa […]

POLISI ‘WALIOMDHULUMU’ MWANGI KUZUILIWA ZAIDI

Maafisa wawili wa polisi ambao ni Klinzy Masinde na Duncan Kiprono wanaotuhumiwa kumpiga risasi mchuuzi Boniface Mwangi jijini Nairobi wataendelea kuzuiliwa kwa siku 15 zaidi ili kuruhusu uchunguzi dhidi yao kuendelea. Mawakili wa maafisa hao hata hivyo umeiomba mahakama kuhakikisha kuwa simu za wateja wao zinalindwa wakati wa uchunguzi, upande wa mashtaka ukishikilia kuwa hakuna […]

FAMILIA YA MWANGI ALIYEPIGWA RISASI YASHIKILIA TUMAINI

Familia ya mchuuzi Boniface Mwangi aliyepigwa risasi kwenye maandamano jijini Nairobi imeitaka serikali kuhakikisha mwanao anapata haki kwa kuwawajibisha maafisa wa polisi wanaodaiwa kumjeruhi mwanao aliyekuwa akiuza maski wakati wa maandamano hayo. Mwangi aliyepata jeraha baya kichwani, amefanyiwa upasuaji wa pili katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta ili kuondoa mabaki ya risasi yaliyokwama kichwani, baada […]

LAGAT AANDIKISHA TAARIFA NA IPOA

Naibu inspekta mkuu wa polisi Eliud Lagat leo ameandikisha taarifa yake mbele ya mamlaka ya IPOA kuhusiana na kifo tata cha mwalimu Albert Ojwang. Lagat aliyewasili katika afisi za IPOA Pamoja na wakili wake alihojiwa kwa muda was aa tatu japo yaliyozungumziwa hayajawekwa wazi. Lagat aliwasilisha lalama zake katika idara ya DCI kuhusu madai yaliyokuwa […]

WASHUKIWA WA SHAMBULIZI LA DUSIT WAFUNGWA MIAKA 30

Mahakama ya kukabili na ugaidi imewapa hukumu ya miaka 30 gerezani washukiwa 2 wanaodaiwa kuhusika na shambulizi la kigaidi katika hoteli ya Dusit D2 hapa Nairobi mwaka wa 2019. Jaji Diana Kavedza amewahukumu Mohammed Abdi Ali na Hussein Mohamed Abdille Ali kufuatia shambulizi hilo lililosababisha vifo vya watu 21 na kuwaacha wengine na majeraha. Kavedza […]

SINA HAJA NA USHINDI WA 2027,ASEMA RAIS

Rais William Ruto anasema lengo lake kwa sasa sio kutwaa uongozi kwenye uchaguzi wa mwaka wa 2027 bali kubadilisha taifa. Akiongea huko Kajiado rais amekanusha madai kuwa serikali yake imekosa kutimiza ahadi nyingi ilizotoa kwa wakenya wakati wa kampeni. Rais amekiri kuwa safari ya kuafikia mabadiliko anayolenga haijakuwa rahisi japo akaelezea kujitolewa kwake kuhakikisha ametimiza. […]

POLISI WALIOMJERUHI MCHUUZI KUSALIA NDANI KWA SIKU 15

Polisi 2 waliokamatwa baada ya kuonekana wakimpiga na kumjeruhi mchuuzi mmoja hapa Nairobi wakati wa maandamano watasalia ndani hadi tarehe 3 mwezi Julai. Mahakama imeagiza wawili hao Barasa Masinde na Dancun Kiprono kuendelea kuzuiliwa kwa muda wa siku 15 ili kutoa nafasi ya kukamilishwa kwa uchunguzi dhidi yao. Wawili hao walimjeruhi mchuuzi Bonface Mwangi Kariuki […]

OGAM ASEMA AKO TAYARI KUMENYANA NA KAKAMEGA HOMEBOYZ

Mchezaji wa Tusker FC Ryan-Wesley Ogam ametangaza kuwa tayari kumenyana na Kakamega Homeboyz katika mechi ya mwisho ya msimu huu wikendi hii, baada ya kupona jeraha la goti lililomweka nje kwa miezi mitatu. Kabla ya kuumia, Ogam alikuwa katika hali nzuri, akifunga mabao 15 na kutoa asisti tatu katika mechi 13 pekee wakati wa mkondo […]