KARUA ASEMA ATAONGOZA KWA MUHULA MMOJA PEKEE

Kiongozi wa Chama cha People’s Liberation Party (PLP), Martha Karua, ametangaza rasmi azma yake ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 akiahidi kwamba endapo atachaguliwa, atahudumu kwa muhula mmoja pekee. Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Kitaifa wa chama hicho, Karua amesema uamuzi wake haujatokana na tamaa binafsi, bali ni kutokana na dhamira ya […]

UHURU: UONGOZI HAUHITAJI UCHUNGU, HASIRA AU CHUKI

Rais wa zamani Uhuru Kenyatta amesema kwamba katika siasa, kiongozi hawezi kuongozwa na uchungu, hasira au chuki.  Akizungumza katika Mkutano wa Kitaifa wa Chama cha Jubilee, Kenyatta amesema siasa inapaswa kuwa chombo cha kuleta umoja na maendeleo kwa wananchi, badala ya kugawanya watu kwa misingi ya tofauti za kisiasa. Kenyatta amesisitiza kuwa viongozi wanapaswa kuweka mbele […]

KEPSA YASHINIKIZA USHIRIKIANO MPYA AGOA

Muungano wa Sekta ya Kibinafsi nchini Kenya (KEPSA) umeitaka Marekani kutayarisha upya Sheria ya Ukuaji na Fursa Afrika (AGOA) kwa kipindi cha miaka 16, ikionya kuwa kushindwa kufanya hivyo kunaweza kuyumbisha kazi na mtiririko wa uwekezaji katika nchi zote mbili. Akizungumza katika Jukwaa la Uwekezaji mjini New York, Mkurugenzi Mtendaji wa KEPSA Carole Kariuki amesema kwamba iwapo ushirikiano wa […]

MSURURU WA GOFU KUENDELEA WEEKEND HII

Msururu wa Mashindano ya Gofu ya Wanariadha wa Kenya (KAGC) utaendelea wikendi hii huku Nanyuki Sports Club ikiandaa Mashindano ya kwanza kabisa ya NCBA Nanyuki Open kuanzia Ijumaa, Septemba 26, hadi Sunda, tarehe 28. Mashindano hayo yamekusanya wachezaji 74 ambao watapigania zawadi ya Ksh 500,000, na kikomo cha ulemavu cha kuingia 13.5, hakikisho la uwanja […]

KENYA YASHINDA MEDALI KATIKA MBIO ZA DUNIA ZA MLIMA

Kenya ilifungua akaunti yake ya medali katika Mashindano ya Dunia ya Mbio za Milima na Njia za Milima ya 2025 huko Canfranc-Pirineos, Uhispania, huku Richard Omaya Atuya akiibuka kidedea katika mbio za kupanda mlima za wima Alhamisi. Bingwa mara mbili wa dunia Patrick Kipng’eno alijipatia shaba, huku bingwa mtawala wa Kombe la Dunia la Mountain […]

KIKOSI CHA BASEBALL CHAINGIA HATUA YA ROBO FAINALI

Kikosi chaka kenya kwenye Kombe la Dunia la Baseball5,kilishangaza wengi baada ya  kukiuka matarajio ya wengi na  kupata nafasi ya kutinga robo fainali mjini Mexico. Katika mchuano huo unaotawaliwa na wacheza uzani mzito duniani, chipukizi wa Kenya wameibuka kuwa timu iliyoibuka kidedea ya mashindano hayo. Safari yao kutoka chini hadi kwa washindani wakubwa imeteka hisia […]

MSHTUKO KERICHO, JAMAA AWAUA WATU 3

Wakazi wa Kijiji cha Samutet kaunti ya Kericho wameachwa na mshtuko baada ya mwanamme mwenye umri wa miaka 19 kuripotiwa kuwaua kwa kuwakatakata watu 3 ambao ni shangazi yake, shemeji yake na mpwa wake kutokana na sababu ambazo hazijajulikana. Kamanda wa polisi kaunti hiyo James Ng’etich amesema mshukiwa kwa jina Evans Kiprop alianza kwa kumshambulia […]

WALIODHALILISHA BENDERA KUFIKISHWA MAHAKAMANI

Wavulana wawili waliokamatwa na maafisa wa DCI kwa madai ya kuidhalilisha bendera kwa kuikanyaga na kuirusha kiholela wanatarajiwa kufikishwa mahakamani hii leo. Muhidin Ahmed mwenye umri wa miaka 14 alikamatwa jana jioni, saa chache baada ya mwenzake Ibrahim Haidar mwenye umri wa miaka 17 kukamatwa. Waziri wa usalama Kipchumba Murkomen amesema washukiwa watafunguliwa mashtaka ya […]

AFISA ALIYEFARIKI HAITI KUWASILISHWA NCHINI

Familia ya afisa wa polisi Kennedy Mutuku aliyefariki kwenye ajali nchini Haiti inatarajiwa kupokezwa mwili wa afisa huyo utapowasilishwa nchini hii leo kutoka Haiti. Kulingana na idara ya polisi, Mutuku mwenye umri wa miaka 41, alikuwa akihudumu katika kitengo cha RDU, na alifariki baada ya gari lao lilolokuwa likikokotwa kupata matatizo ya kiufundi kabla ya […]

IEBC TAYARI KWA USAJILI, MWENYEKITI

Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imeweka mikakati jumuishi itakayohakikisha usajili wa juu zaidi wa vijana kama wapiga kura kwenye usajili utakaofunguliwa Jumatatu ijayo. Ni hakikisho la mwenyekiti wa tume hiyo Erastus Ethekon, akizungumza alipofika mbele ya kamati ya utekelezaji wa katiba bungeni, akisema tume hiyo inalenga kuwasajili wapiga kura wapya hasa vijana milioni […]