SERIKALI YAWAONYA WAHADHIRI WANAOGOMA

Serikali imewataka wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma wanaogoma kwa wiki moja sasa kurejea kazini la sivyo wachukuliwe hatua za kinidhamu. Waziri wa elimu Julius Ogamba, amesema mgomo huo ni ukiukaji wa amri ya mahakama iliyofutilia mbali, akiongeza kuwa tayari serikali imetoa shilingi bilioni 2.5 ili kutatua malalamishi yao. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

RUPHA YASHIKILIA HAKUNA SHA

Wagonjwa wanaotegemea bima ya SHA kulipia huduma za matibabu katika hospitali za kibinafsi wataendelea kuhangaika hadi serikali itakapolipa deni inalodaiwa la zaidi ya shilingi bilioni 70 kama malimbikizi ya malipo chini ya bima ya zamani NHIF. Ndio msimamo wa hospitali za kibinafsi chini ya muungano wa RUPHA, ambao umeendelea kuilaumu serikali kutokana na mahangaiko wanayopitia […]

DEMBELE ASHINDA TUZO LA BALLON D’OR

Fowadi wa Ufaransa Ousmane Dembele alishinda tuzo ya Ballon d’Or kwa wanaume katika hafla iliyofanyika Paris hapo jana Hili ni  tuzo la mtu binafsi lenye hadhi zaidi katika kandanda likituzwa kwa nafasi yake katika kikosi cha Paris Saint-Germain kilichoshinda Ligi ya Mabingwa msimu uliopita. Dembele, 28, alimshinda mchezaji wa Barcelona na Uhispania Lamine Yamal kwenye […]

MAANDALIZI MAZURI YALIVUNIA KENYA USHINDI TOKYO

Makocha wa riadha wamehusisha uchezaji bora wa wanariadha wa kike wa Kenya katika Mashindano ya Dunia ya Riadha yaliyokamilika huko Tokyo Japan na maandalizi mazuri ya kiakili na kimwili. Wasichana wa Kenya – Faith Kipgeon, Beatrice Chebet, Peris Jepchirchir, Faith Cherotich na Lilian Odora- wote waliambulia dhahabu katika nyanja zao huku Timu ya Kenya ikitoa […]

PAMZO APONGEZA KIKOSI CHAKE

Kocha mkuu wa Posta Rangers, Sammy “Pamzo” Omollo amepongeza mabadiliko ya kisaikologia  ya timu yake baada ya kuzindua kampeni yao ya Ligi Kuu ya FKF ya 2025/26 kwa ushindi mnono wa 2-1 dhidi ya Mathare United Uwanja wa Kasarani Annex Jumatatu jioni. Wana barua hawa  ambao waliponea chupuchupu kushushwa daraja msimu uliopita baada ya kuilaza […]

RUTO: KUNA UBAGUZI KATIKA MSAADA HAITI

Utepetevu wa mataifa na ukosefu wa kujitolea kutimiza ahadi za kurejesha utulivu nchini Haiti ndicho kikwazo kikubwa katika kufanikisha operesheni hiyo inayoongozwa na polisi wa Kenya. Ndiyo kauli ya Rais William Ruto akizungumza nchini Marekani, ambapo ameyalaumu kutokana na alichokitaja kuwa kurejesha nyuma harakati za kuleta amani katika taifa hilo la Karibia. Hata hivyo, amekariri […]

MACHIFU MANDERA KUPEWA BUNDUKI, MURKOMEN

Serikali imetoa hakikisho la usalama katika eneo la Border One kwenye mpaka wa Kenya na Somalia baada ya kuibuka hofu mapema mwezi huu kuhusu uwepo wa vikosi vya wanajeshi wa Jubaland nchini Somalia. Akizungumza alipozuru kaunti ya Mandera, Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen, amesema usalama wa ndani umerejeshwa na kwamba machafuko kwenye mataifa […]

RAILA ADOKEZA KUGOMBEA URAIS 2027

Kinara wa ODM Raila Odinga amekana kuhusu uwepo wa makubaliano ya chama hicho kushirikiana na UDA kwenye uchaguzi wa urais ujao, akiwaonya wabunge wa ODM kukoma kueneza porojo kuhusu madai hayo. Odinga amesema kuwa ODM bado haijatoa mwelekeo kuhusu uwaniaji wa urais, huku akidokeza kuhusu uwezekano wa kumwasilisha mgombeaji wa urais kumenyana na rais William […]

SERIKALI YATANGAZA MSAADA MAENEO KAME

Ni afueni kwa zaidi ya watu milioni 1.7 wanaokabiliwa na uhaba wa chakula katika maeneo kame baada ya serikali kutangaza mpango wa dharura wa kusambaza chakula kwa wakazi wa maeneo hayo. Hii ni baada ya Waziri wa utumishi wa umma Geoffrey Ruku kufanya mkutano na makamishna wa kaunti kame 23 na washikadau wengine ili kupanga […]

MAHANGAIKO YA SHA SIKU YA PILI

Wagonjwa katika hospitali za kibinafsi zilizo chini ya muungano wa RUPHA watalazimika kulipia huduma za matibabu kwa pesa taslimu kwa siku ya 2 sasa baada ya hospitali hizo kutangaza kufutilia mbali matumizi ya bima ya afya ya SHA. Kulingana na muungano huo, serikali ina deni la zaidi ya shilingi bilioni 10 la hospitali hizo ambalo […]