POLISI WAANZA MSAKO DHIDI YA WALIOKOSEA HESHIMA BENDERA

Tukio la vijana wawili raia wa Somalia kuidhihaki bendera ya Kenya wakati wa mechi ya soka katika uwanja wa Nyayo wikendi iliyopita limechukua mkondo wa kidiplomasia, ubalozi wa Somalia humu nchini ukilazimika kuomba msamaha. Kwenye tukio hilo ambalo limetawala mijadala kwenye mitandao ya kijamii, vijana hao walinaswa kwenye video wakiikanyaga bendera ya Kenya na kuirusha […]

MUSYOKA ATAKA POLISI WAONDOLEWE HAITI

Ni wakati wa serikali ya Kenya kukiri kwamba imelemewa na operesheni ya kurejesha utulivu nchini Haiti na kuwarejesha nchini maafisa wake wa polisi. Ni kauli ya kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka, ambaye amekosoa serikali kwa madai ya kupotoshwa kuhusiana na kuwatuma maafisa wake nchini humo, hasa baada ya kubainika kuwa maafisa 3 wamefariki kufikia sasa. […]

ODM YAMTEUA MWANIAJI WA UBUNGE KASIPUL

Boyd Were, mwanawe aliyekuwa mbunge wa Kasipul Ong’ondo Were, ndiye atakayepeperusha bendera ya chama cha ODM kwenye uchaguzi mdogo eneo hilo kupata mrithi wa babake. Hii ni baada yake kuibuka mshindi kwenye uchaguzi wa mchujo hapo jana kwa kura 18, 210, mpinzani wake wa karibu Newton Ogada kwa mbali akiwa na kura 3,037 huku waliosalia […]

WAHADHIRI WALAUMU VYUO VIKUU KWA MGOMO

Mgomo wa wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma umeendelea kutatiza masomo kwa wiki ya pili sasa licha ya serikali kuonya kuwachukulia hatua za kinidhamu wahadhiri walio kwenye mgomo ambao serikali inasema ulifutiliwa mbali na mahakama. Katika chuo kikuu cha Dedan Kimathi, wahadhiri chuoni humo wamedai kukandamizwa na usimamizi wa chuo hicho, wakisema umekataa kuwapa haki […]

DENI LA KENYA LINALIPA MISHAHARA SI MAENDELEO, DATA YA HAZINA YAFICHUA

Sehemu kubwa ya fedha zilizokopwa za Kenya zilizotengwa kwa miradi ya maendeleo imeshuka hadi kiwango cha chini kabisa katika kipindi cha mwongo mmoja, na hivyo kufichua ongezeko la matumizi ya deni ili kulipia gharama za kawaida kama vile mishahara na pensheni. Takwimu za Hazina ya fedha zinaonyesha kuwa katika mwaka wa fedha wa 2024-2025, shilingi bilioni 582.9 ambayo ni asilimia 56.4 zilitumika kwa […]

CHELSEA WAZAMISHA LINCOLN

Baada ya kua ana weekend ngumu kwa ligi ya premia kilabu ya Chelsea ilijizatiti na kukota mabao mawili katika mashindano ya kombe la carabao jana usiku . mabao mawili ndani ya dakika tano za kwanza za mchezo kuanza tena – kutoka kwa Tyrique George na Facundo Buonanotte – yalinyima timu ya Michael Skubala ya lincoln […]

TIMU YA BASEBALL YAWASILI MEXICO

TIMU ya vijana ya Kenya Baseball5 imetua mjini Nayarit, Mexico, tayari kuwakilisha nchi kwenye Kombe la Dunia la Baseball5, linaloendelea. Timu hiyo, inayojumuisha wachezaji wanane, imetumia mwezi uliopita katika mafunzo ya makazi katika Chuo Kikuu cha Africa Nazarene, kurekebisha ujuzi wao na kujenga kemia ya timu yenye nguvu. Safari ya Kenya katika hafla ya kimataifa […]

NYOTA WA RIADHA WAREJEA NA MBWEMBWE

Nyota wa riadha wa Kenya walipata mapokezi ya kishindo Jumanne alasiri waliporejea kutoka kwa Mashindano ya Riadha ya Dunia yaliyomalizika hivi punde jijini Tokyo, Japan. Wafuasi, maafisa wa serikali na viongozi wa Riadha Kenya walijaa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) kusherehekea ushindi wa Timu ya Kenya. Kenya ilinyakua medali 11 […]

TRUMP: MNAWAZAWADI WANAMGAMBO WA HAMAS

Rais wa Marekani Donald Trump ameyakosoa mataifa ya Ulaya yaliyoitambua Palestine kama taifa huru, katika hatua ambayo imeonekana kama kuitenga Marekani ambayo ianunga mkono Israel katika mapigano yake na Palestine. Akihutubia kikao cha baraza kuu la Umoja wa Mataifa nchini Marekani, Trump ameyataka mataifa yenye nguvu duniani kuangazia mikakati itakayohakikisha kuwa mateka wanaozuilia katika ukanda […]

RUTO AFICHUA AFISA ALIFARIKI HAITI

Familia ya afisa wa polisi Bernard Kabiru aliyeripotiwa kutoweka mwezi Machi nchini Haiti inashinikiza serikali kuweka wazi kilichomfanyikia mwanao, kutokana na kauli ya Rais William Ruto hapo jana kwamba afisa huyo alifariki. Akizungumza katika kikao cha kujadili hali ya usalama nchini Haiti, akiwa jijini New York Marekani, Ruto aliwaomboleza maafisa 3 waliofariki akiwemo Kabiru, ambaye […]