UEFA YAENDELEA

Mechi ya 6 kati ya 8 za ligi ya klabu bingwa bara Ulaya itasakatwa usiku huu ambapo jumla ya mechi 9 zitachezwa katika nyuga mbali mbali. Miongoni mwa mechi kuu ni pambano kati ya Barcelona na Eintracht Frankfurt, na Bayern Munich dhidi ya Sporting na kisha Inter Milan dhidi ya Liverpool. Iwapo Bayern na Inter […]

DROO YA FA RAUNDI YA 3

Droo ya kipute cha FA imekamilika huku klabu za Manchester City, Manchester United, Arsenal na Liverpool zikiwa miongoni mwa klabu 20 za ligi kuu ya Uingereza zilizowafahamu wapinzani wao kwenye raundi ya 3 ambayo pia itazijumuisha klabu 24 za ligi ya Championship. Klabu hizo zitajiunga na klabu nyingine za ligi za chini kama Macclesfield, Weston-Super-Mare […]

TUSKER FC ROHO JUU DISEMBA HII

Kocha mkuu wa klabu ya Tusker FC Charles Okere anaamini kuwa ushindi wa kikosi chake wa bao 1-0 dhidi ya Ulinzi Stars hasa mwanzoni mwa mwezi huu wa Disemba umekiweka kikosi hicho katika mkondo wa kumaliza katika nafasi bora kwenye awamu ya kwanza ya ligi kufikia mwishoni mwa mwaka huu. Tusker walionyesha mchezo mzuri dhidi […]

IEBC: VIJANA HAWAJUI UMUHIMU WA KURA

Idadi ndogo ya wapiga kura wapya waliojitokeza kusajiliwa katika kipindi cha zaidi ya miezi 2 iliyopita imeibua hofu kuhusu kujitolea kwa vijana kushinikiza mageuzi, tume huru ya uchaguzi na mipaka ikisema imewasajili wapiga kura 148,000 pekee. Kwenye ripoti yake, IEBC iliyoandaa jukwaa la kufanya tathmini ya zoezi la chaguzi ndogo zilizopita, imesema vijana bado hawajakumbatia […]

MUSYOKA AKEJELI GUMZO LA SINGAPORE

Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka amependekeza rais William Ruto kubadili mfumo wa utawala wa serikali yake iwapo ananuia kuifanya Kenya kuwa miongoni mwa mataifa yenye nguvu kiuchumi duniani mfano wa Singapore. Akizungumza jijini Nairobi, Musyoka ametolea mfano wa machafuko, ufisadi na kutokujali kama vizingiti kwa azma hiyo, huku akiikosoa serikali kutokana na mfumo wake wa […]

GATHUNGU AKOSOA UKOPAJI WA SERIKALI

Kenya ina uwezo wa kufadhili miradi yake ya maendeleo bila kuhitaji kukopa fedha zaidi nyumbani na katika mashirika ya kimataifa. Haya ni kwa mujibu wa mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Nancy Gathungu, akikariri kuwa ushuru wa juu na ufisadi ndivyo vizingiti vikuu katika juhudi za serikali kufufua uchumi, huku akikosoa kiwango cha juu cha […]

TANZANIA YAHARAMISHA MAANDAMANO

Serikali ya Tanzania imewekwa kwenye darubini ya ulimwengu kuona jinsi itakavyowakabili waandamanaji baada ya kupiga marufuku maandamano ya leo huku taifa hilo likiadhimisha siku ya Uhuru. Maandamano hayo yaliyopangwa na viongozi wa upinzani, yalilenga kupinga uongozi wa taifa hilo na madai ya kufeli kwa serikali, ila vitengo vya usalama vikayataja kuwa jaribio la kuipindua serikali […]

POLISI ZAIDI WAWASILI HAITI

Operesheni ya kurejesha utulivu nchini Haiti inayoongozwa na polisi wa Kenya imepigwa jeki baada kikosi maalum cha 5 chenye maafisa 230 kuwasili nchini humo hapo jana kujumuika kwenye operesheni hiyo. Kikosi hicho kiliwasili hapo jana huku maafisa wenginme 100 wakiondoka baada ya kukamilisha muda wao wa kuhudumu, wengine zaidi wakitarajiwa kuondoka baada ya kikosi kipya […]

WETANG’ULA, JEN. MUHOOZI WAZUNGUMZIA MIGINGO

Suala la kuhangaishwa kwa wavuvi wa Kenya katika kisiwa cha Migingo Ziwani Victoria na vikosi vya usalama vya Uganda limepewa kipaumbele katika mkutano wa maspika wa mabunge ya Afrika Mashariki na mkuu wa jeshi la Uganda Jenerali Muhoozi Kainerugaba. Haya ni kwa mujibu wa spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang’ula, akisema Jenerali Muhoozi amekiri […]

TANZANIA YAWATAKA RAIA KUSALIA NYUMBANI

Serikali ya Tanzania imewahimiza raia wake wasio watoaji wa huduma muhimu kusalia nyumbani wakati wa maadhimisho ya siku ya uhuru itakayoadhimisha hapo kesho nchini humo. Katika taarifa ya msemaji wa serikali hiyo Mussa Azzan Zungu amewataka wafanyakazi wa huduma za dharura pekee kuripoti katika maeneo yao ya kazi. Maadhimisho hayo yanajiri huku wito ukisheheni mitandaoni […]